Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
Pongezi hizo zimetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo ya CCM Zanzibar, Khamis Mbeto Khamis, wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari katika ofisi za CCM, Kisiwandui, Zanzibar.
Mbeto alisema kuwa Chuo Kikuu cha Zanzibar kimemtunuku Shahada hiyo ya Heshima ya Uchumi kama ishara ya kutambua na kuthamini mchango mkubwa wa Rais Dkt. Mwinyi katika uongozi wake, ambao umeacha alama ya kipekee na historia itakayokumbukwa wakati wote.
Alisisitiza kuwa heshima hii ni ushahidi wa mafanikio makubwa yaliyofikiwa Zanzibar, hasa katika kipindi kifupi cha uongozi wake wa miaka minne, ambapo uchumi wa Zanzibar umeimarika na maendeleo mbalimbali yamepatikana.
"Heshima hii inatokana na juhudi kubwa za Rais Dkt. Mwinyi katika kukuza uchumi, kuboresha huduma za kijamii, na kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi wa Zanzibar. CCM Zanzibar ina furaha kubwa kumpongeza Rais Mwinyi kwa kutambuliwa na Chuo Kikuu cha Zanzibar kwa mchango wake mkubwa," alisema Khamis Mbeto.
Katibu Mbeto alitoa wito kwa wananchi wa Zanzibar kuendelea kumunga mkono Rais Dkt. Mwinyi na serikali yake katika juhudi zao za kukuza uchumi, kuboresha huduma za kijamii, na kuhakikisha Zanzibar inapata maendeleo ya kweli na endelevu.
Hafla ya kutunukiwa Shahada ya Heshima hiyo ilifanyika Disemba 5, mwaka 2024, katika Viwanja vya Chuo Kikuu cha Zanzibar, Tunguu, wakati wa Mahafali ya 22 ya Wahitimu wa mwaka 2024.
Katika hotuba yake, Rais Dkt. Mwinyi alishukuru Chuo Kikuu cha Zanzibar kwa kuthamini kazi anazozifanya kwa ajili ya maendeleo ya nchi.
Alieleza kuwa Shahada hiyo ni ishara ya mafanikio ya serikali yake na wananchi wa Zanzibar kwa ujumla, na itaongeza hamasa ya kufanya kazi zaidi katika kuleta maendeleo endelevu.
Rais Dkt. Mwinyi pia alisisitiza kuwa Shahada hiyo inawakilisha kazi nzuri inayofanywa na serikali anayoiongoza, na itaendelea kumhimiza katika kutimiza malengo ya maendeleo.
"Hii siyo mwisho wa safari, bali ni mwanzo wa hatua kubwa zaidi za maendeleo. Nitaienzi heshima hii na kuendelea kuwatumikia wananchi wangu kwa uwezo wangu wote," alisema Rais Dkt. Mwinyi.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
02-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
02-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
02-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
02-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
02-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
02-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
02-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
02-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
02-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
02-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
02-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
02-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
02-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
02-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
02-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
02-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
02-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
02-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
02-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
02-01-2026