RAIS WA ZANZIBAR DKHUSSEIN ALIMWINYIAMEKUTANA NA UJUMBEKUTOKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA ELIMU SAYANSI NA UTAMADUNI (UNESCO) KUJADILI MASUALA YA UTUNZAJI WA HIFADHI YA MJI MKONGWE
Dk. Mwinyi alikutana na ujumbe huo Ikulu, Zanzibar ukiambata na Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Simai Mohammed Said pamoja na maafisa wa Wizara hiyo.Alisema, licha ya maendeleo makubwa yaliyofikiwa na Zanzibar bado Urithi wa hifadhi ya kimataifa ya Mji Mkongwe unaendelea kulindwa na kuenziwa kwa mujibu wa taratibu na kanuni zilizowekwa. Rais Dk. Mwinyi aliueleza ujumbe huo kwamba, Selikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
imechukua hatua mbalimbali za kuutunza urithi ikiwemo kuondosha msongamano wa maegesho ya vyombo vya moto kwenye maeneo yote ya Mji Mkonge wa Zanzibar, ili kuenzi haiba ya mji huo kuendelea kuwa kivutio mashuhuri cha watalii
na wageni wanaoutembelea mji huo. Aidha, alisema katika kutekeleza hatua hiyo, Serikali imeamua kujenga maegesho ya vyombo vya moto eneo la Darajani ikiwa njia mbadala ya kuondosha msongamano wa magari kwenye maegesho ya Mji Mkongwe.
Pia Dk. Mwinyi, aliueleza Ujumbe huo kwamba hatua nyengine iliyochukuliwa na Serikali ni kushirikiana na sekta binafsi kuutunza Urithi huo hasa kuyaendeleza majengo yaliyochakaa kwa kuyakarabati kwa mujibu wa kanuni na taratibu za kuyaenzi majengo hayo kuyarudisha kwenye uhalisia wake. Alisema, Serikali inasimamia kwa karibu na kuhakikisha thamani na mali zote za asili zilizokuwemo kwenye majengo hayo zinarudishwa sehemu husika baada ya ukarabati.
Akizungumzia jengo la Beit el Ajaaib na la People’s Palace, Rais Dk. Mwinyi aliueleza ujumbe wa UNESCO kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ushirikiano na Serikali ya Oman wanaendelea kusimamia ujenzi wa majengo hayo. Hata hivyo, Dk. Mwinyi alieleza Beit el Ajaaib na la People’s Palace ni alama muhimu inayoitambulisha Zanzibar duniani kote.
Nao, Ujumbe huo wa UNESCO, uliitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kuendelea kuuenzi na kuutunza urithi huo ili kuunusuru na athari za mabadiliko ya teknolojia ikiwemo kukua kwa maendeleo ya nyanja mbalimbali nchini ambayo kwa namna moja ama nyengine itakua sababu ya kubadili mandhari halisi na mwonekano wa mji huo.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
25-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
25-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
25-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
25-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
25-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
25-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
25-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
25-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
25-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
25-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
25-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
25-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
25-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
25-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
25-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
25-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
25-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
25-05-2026