Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


RAIS WA ZANZIBAR DKHUSSEIN ALIMWINYIAMEKUTANA NA UJUMBEKUTOKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA ELIMU SAYANSI NA UTAMADUNI (UNESCO) KUJADILI MASUALA YA UTUNZAJI WA HIFADHI YA MJI MKONGWE

alternative

Dk. Mwinyi alikutana na ujumbe huo Ikulu, Zanzibar ukiambata na Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Simai Mohammed Said pamoja na maafisa wa Wizara hiyo.Alisema, licha ya maendeleo makubwa yaliyofikiwa na Zanzibar bado Urithi wa hifadhi ya kimataifa ya Mji Mkongwe unaendelea kulindwa na kuenziwa kwa mujibu wa taratibu na kanuni zilizowekwa. Rais Dk. Mwinyi aliueleza ujumbe huo kwamba, Selikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
imechukua hatua mbalimbali za kuutunza urithi ikiwemo kuondosha msongamano wa maegesho ya vyombo vya moto kwenye maeneo yote ya Mji Mkonge wa Zanzibar, ili kuenzi haiba ya mji huo kuendelea kuwa kivutio mashuhuri cha watalii
na wageni wanaoutembelea mji huo. Aidha, alisema katika kutekeleza hatua hiyo, Serikali imeamua kujenga maegesho ya vyombo vya moto eneo la Darajani ikiwa njia mbadala ya kuondosha msongamano wa magari kwenye maegesho ya Mji Mkongwe.

Pia Dk. Mwinyi, aliueleza Ujumbe huo kwamba hatua nyengine iliyochukuliwa na Serikali ni kushirikiana na sekta binafsi kuutunza Urithi huo hasa kuyaendeleza majengo yaliyochakaa kwa kuyakarabati kwa mujibu wa kanuni na taratibu za kuyaenzi majengo hayo kuyarudisha kwenye uhalisia wake. Alisema, Serikali inasimamia kwa karibu na kuhakikisha thamani na mali zote za asili zilizokuwemo kwenye majengo hayo zinarudishwa sehemu husika baada ya ukarabati.

Akizungumzia jengo la Beit el Ajaaib na la People’s Palace, Rais Dk. Mwinyi aliueleza ujumbe wa UNESCO kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ushirikiano na Serikali ya Oman wanaendelea kusimamia ujenzi wa majengo hayo. Hata hivyo, Dk. Mwinyi alieleza Beit el Ajaaib na la People’s Palace ni alama muhimu inayoitambulisha Zanzibar duniani kote.
Nao, Ujumbe huo wa UNESCO, uliitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kuendelea kuuenzi na kuutunza urithi huo ili kuunusuru na athari za mabadiliko ya teknolojia ikiwemo kukua kwa maendeleo ya nyanja mbalimbali nchini ambayo kwa namna moja ama nyengine itakua sababu ya kubadili mandhari halisi na mwonekano wa mji huo.

alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi