RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amesema kuna haja kwa Zanzibar kuongeza vivutio vingi vya utalii kwa kubuni matukio maalumu ya kuwavutia wageni wengi na kuviimarisha vivutio vya asili vilivyomo Tanzania.
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amesema kuna haja kwa Zanzibar kuongeza vivutio vingi vya utalii kwa kubuni matukio maalumu ya kuwavutia wageni wengi na kuviimarisha vivutio vya asili vilivyomo Tanzania.
Akizungumza kwa niaba ya Rais Dk. Samia, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, aliyasema hayo kwenye ufunguzi wa Tamasha la nane la Kizimkazi, huko uwanja wa Paje Mkoa wa Kusini Unguja.
Rais Dk. Mwinyi alisema tamasha hilo linatoa fursa yakuendeleza utalii na kuutangaza mkoa wa kusini kiutalii na Zanzibar kwa ujumla kwa kufungua fursa nyingi za maendeleo ikiwemo biashara, uwekezaji na uchumi.
Alieleza matarajio yake ya baadae kwa tamasha hilo kuweka hitoria nyengine ya mkoa wa Kusini Unguja kwa kuongeza fursa nyingi za Utalii, uwekezaji na maendeleo ya biashara.
Sambamba na kueleza tamasha hilo mbali na kuongeza vivutio vya utalii vya ndani ya mkoa huo kama tukio la asili la ‘mwaka kogwa’ lakini kuendelea kuitangaza Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kwa kuendeleza umoja na mshikamano wa Watanzania kwa pande zote za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuwakutanisha pamoja kwa amani na upendo kupitia Tamasha la Kizimkazi ambako wasanii wengi, wananchi, taasiisi mbalimbali za binafsi, wadau wa maendeleo, wajasiriamali, wenyeji na wageni kukutana na kufurahika kwa pamoja.
Pia alieleza tamasha hilo limeendelea kuezi na kuimarisha utamaduni wa Tanzania kwa kuvienzi vyakula vya asili, kuimarisha makongamano, michezo, burudani na kuwawesha vijana kiuchumi kwa kubuni miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kukuza biashara, aidha, Dk. Mwinyi alieleza fursa za makampuni binafsi kuwekeza miradi mikubwa zikiwemo taasisi binafsi, tasisi za fedha na benki kutanua matawi yao kusini Unguja kutokana na Tamasha la Kizimkazi.
Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi aliipongeza Serikali ya Mkoa wa Kusini Unguja na kamati ya maandalizi ya Tamasha la Kizimkazi kwa kuelendeza juhudi za Rais Dk. Samia kwa kulienzi tamasha hilo.
Akizungumzia fursa za Uchumi wa Buluu na uwekezaji wa biashara, Rais Dk. Mwinyi alisema Mkoa wa Kusini Unguja umebarikiwa bahari na eneo kubwa la wazi kwa wilaya zake zote mbili za Kati na Kusini mwa Mkoa huo na kueleza kupitia Tamasha la Kizimkazi na fursa zinazotoka huko, sekta ya uvuvi itaimarika zaidi kwa kilimo cha kisasa cha mwani na kuongezeka tija kwa fursa nyingi za utalii kuendelea kufunguka.
Akitoa salam za mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Kusini, Unguja Rashid Hadidi aliipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano wanatoa kukuza maendelo ya mkoa huo kwa sekta zote ikiwemo kuimarishwa kwa miundombinu ya barabara za kisasa, ujenzi wa hospitali kubwa za Wilaya zenye mashine na vifaa tiba vya kisasa, skuli za ghorafa pamoja na kukamilika kwa ujenzi wa matangi matatu makubwa ya maji safi yenye uwezo wa kuchukua lita milioni 10 ambayo yatasaidia kusambaza maji kwa mkoa wote wa Kusini Unguja.
Tamasha la Kizimkazi liliasisiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan miaka nane iliyopita likiwa na lengo la kuunganisha umoja, ushirikiano na mshikamo wa Watanzania wa Mkoa wa kusini Unguja na Tanzania yote bila kujali tofauti za asili na siasa zao.
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆’-𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀
01-06-2026
𝐍𝐈 𝐍𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀!
01-06-2026
🔰𝐀𝐒𝐀𝐍𝐓𝐄𝐍𝐈 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎!
01-06-2026
𝐒𝐇𝐔𝐋𝐄 𝐘𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐌𝐄𝐓𝐀 𝟏𝟐 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀𝐍𝐈 𝐇𝐀𝐈, 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
01-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
01-06-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
01-06-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
01-06-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
01-06-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
01-06-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
01-06-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
01-06-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
01-06-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
01-06-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
01-06-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
01-06-2026