Waumini wa dini ya Kiislamu na wazanzibari kwa ujumla wametakiwa kujenga utamaduni wa kuwaombea dua viongozi wakuu wa nchi ili waweze kuleta maendeleo na kuyatekeleza kwa vitendo yale yote waliyoyaahidi kwa wananchi wao
Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla wakati akiwasalimia waumini wa Masjid SUNNI HANAFII MKUNAZINI mara baada ya kumaliza Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Amesema wazanzibari na waumini wa dini zote wana wajibu wa kuwaombea dua viongozi wakuu ili kuzidi kuwatelete maendeleo na kuwatekeleza mambo yote muhimu ambayo wananchi wanastahiki kupatiwa kutoka kwa viongozi wao kama vile anavyotekeleza kwa vitendo Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Braza la Mapinduzi Alhajj Dkt. Hussein Ali Mwinyi
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwa kila mzanzibar na mtanzania anahitaji maendeleo kwenye sekta zote zikiwemo barabara,maji safi na salama,afya na mengineyo jambo ambalo ndio dira ya viongozi wakuu kuwarahisishia wananchi wake wa kupata kila wanachokihitaji kwa ubora na kwa wakati.
Alhajj Hemed amesema serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Mwinyi ipo salama na viongozi wake wanafanya kazi kwa kushirikiana wakiwa na lengo la kuwaletea maendeleo wananchi wake kupitia sekta zikiwemo barabara, maji safi na salama ,elimu na mengineyo bila ya ubaguzi wa aina yoyote kwa faida ya vizazi vya sasa na baadae.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed amewataka wananchi wa Zanzibar na watanzania kwa ujumla kuendelea kuitunza na kudumisha amani na utulivu uliyopo nchini kwa kutambua kuwa amani ndio msingi wa maendeleo katika nchi yoyote duniani, hivyo ni lazima kuendelea kuitunza na kuilinda amani tulinayo ili kuweza kuwavutia wawekezaji kutoka nchi mbali mbali kuja kuekeza nchini.
Mapema akitoa Khutba katika Sala ya Ijumaa, Ustadh MAHSEIN WAHID amewataka waumini wa Dini ya Kiislam kushikamana katika kuitetea dini ya Allah (S.W) na kuirithisha kwa vizazi vyetu jambo ambalo litawasaidia kufikia lile lengo waliloletewa duniani la kumcha Mwenyezimungu.
Amesema kuwa suala la kuhimizana kufanya ibada na kuchuma chumo la halali ni wajibu wa kila muumin wa dini ya kiislamu, na kuwataka kutambua lengo la kuumbwa wanadamu ni kumcha Allah kwa kufuata mazuri yakiyofanywa na mtume Muhamad (S.A.W) ambayo yataongeza mapenzi baina yao.
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆’-𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀
01-06-2026
𝐍𝐈 𝐍𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀!
01-06-2026
🔰𝐀𝐒𝐀𝐍𝐓𝐄𝐍𝐈 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎!
01-06-2026
𝐒𝐇𝐔𝐋𝐄 𝐘𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐌𝐄𝐓𝐀 𝟏𝟐 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀𝐍𝐈 𝐇𝐀𝐈, 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
01-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
01-06-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
01-06-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
01-06-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
01-06-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
01-06-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
01-06-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
01-06-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
01-06-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
01-06-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
01-06-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
01-06-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
01-06-2026