RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, AL HAJJ DK. HUSSEIN ALI MWINYI, AMEENDELEA KUIHIMIZA JAMII JUU YA UMUHIMU WA KUDUMISHA AMANI
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameendelea kuihimiza jamii juu ya umuhimu wa kudumisha amani na kubeba imani ya dhati ndani ya mioyo yao kwa mustakbali wa taifa na ustawi wa jamii bora kwa maendeleo ya uchumi endelevu nchini.
Al hajj Dk. Mwinyi, alitoa nasaha hizo kwenye Msikiti Mabuluu Mfereji wa Wima, Mkoa wa Mjini Magharibi, alikojumuika pamoja na waumini wa dini ya Kiislamu kwenye ibada ya sala ya Ijumaa.
Rais, Al hajj Mwinyi, aliieleza Imani na amani ni vitu viwili vinavyokwenda sambamba na kutegemeana wakati wote, hivyo aliisihi jamii kadri wanapokusanyika pamoja kwenye maisha yao ya kila siku, wasichoke kuamini na kuendelea kuhimiza amani ya nchi na kuidumisha muda wote katika kuyaendea mazuri yote kwa ustawi wa jamii njema na taifa kwa ujumla.
“Imani na amani vinakwenda sambamba, amani ndio dini yetu, Uislamu unatutaka tueneze amani wakati wote, amani ikikosekana mambo mengine yote hayawezekani na hili tunalijua kutokana na wenzetu wanayoyapitia huko kwenye mataifa ya wenzetu, tunaona sehemu zenye vita hata ibada hazifanyiki, ili ipatikane amani lazima tuwe na Imani ndani ya nyoyo zetu” alisisitiza Al hajj Mwinyi.
Al hajj Dk Mwinyi alieleza, kila mmoja anawajibu wa kuitunza na kueneza amani kwa mustakbali wa taifa na ustawi wa jamii iliyobora.
Pia, aliwahimiza waumini hao kuendelea kuliombea taifa na viongozi kwa ujumla ili kuendelea kuwaongoza vyema na kuyatekeleza yote waliyowaahidi wananchi.
Rais Al Hajj Mwinyi alieleza, viongozi wanamajukumu makubwa na kubeba dhima kubwa hivyo, aliwasihi wanaumini hao na jamii kwa ujumla wasichoke kuwaombea mazuri na kuzidi kuwaombea kheir kwa Mwenyezi Mungu (S. W).
Akitoa nasaha za Ijumaa, Katibu Mtendaji kutoka Ofisi ya Mufti Zanzibar, Sheikh Khalid Ali Mfaume, alisifu juhudi za Rais Al Hajj Dk. Mwinyi kwa Imani aliyoijenga kwa waumini wa dini ya kiislamu na taifa kwa ujumla ikiwemo kujumuika nao pamoja kwenye ibada katika misikiti mbalimbali nchini sambamba na kuwaboresha ustawi wa maendeleo na uchumi wananchi wote.
Alisema juhudi zote hizo ni Imani yake kwa Wazanzibari na taifa lote, hasa jitihada za kuendelea kuimarisha huduma za jamii, uchumi na maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu imara na kuboresha mawasiliano.
Naye, Khatibu wa sala ya Ijumaa msikitini hapo, Sheikh Abdul Karim Said Abdulla aliihusia jamii kuendelea kupendana na kutendeana mema kwa kujizuia kuudhiana na kutendea mabaya.
Aliwashajihisha waumini hao kuendeleza mshikamo kwa kudumisha amani, umoja na upendo baina yao kwa ustawi wa jamii iliyo njema.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025