CCM KUFADHILI KITABU CHA MZEE SONGAMBELE KUENZI HISTORIA YA NCHI, CHAMA NA SERIKALI
Balozi Nchimbi atoa neno, akimwakilisha Dkt. Samia msibani
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amesema kitabu alichoandika Alhaj Mzee Mohamed Mustafa Songambele kitakuwa mojawapo ya rejea adhimu za historia ya Tanzania.
Balozi Nchimbi amesema kuwa kitabu hicho kiitwacho “Safari ya Karne”, kina utajiri wa maelezo kuhusu mapambano ya kutafuta uhuru wa Tanganyika, kupatikana kwa nchi na taifa la Tanzania na kuundwa kwa CCM.
Dkt. Nchimbi amesema hayo alipokuwa akitoa salaam za pole na rambirambi kwenye msiba wa Hayati Alhaji Mzee Songambele, akimwakilisha Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, mjini Songea, mkoani Ruvuma, leo Jumatatu tarehe 2 Juni 2025.
“Kutokana na heshima na mchango mkubwa wa Mzee Songambele kwa nchi yetu, taifa letu na chama chetu, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuguswa sana na msiba huu, ameniagiza rasmi kumwakilisha na ameagiza Chama na Serikali kuchukua gharama zote za msiba huu.
“Mzee Songambele amefariki akiwa amemaliza kuandika kitabu chake. Hadi mwezi Machi mwaka huu, alikuwa amekiita jina la “Swahiba wa Nyerere”, lakini miezi miwili iliyopita akabadili, nadhani aliona atatimiza miaka 100, akakiita “Safari ya Karne,” amesema Balozi Nchimbi na kuongeza;
“Kutokana na umuhimu wa kitabu hicho, ambacho aliniomba niandike dibaji na niliandika, humo ameelezea mengi kuhusu yeye na Nyerere, harakati za uhuru, utaifa wetu na CCM pia, Chama Cha Mapinduzi kitasimamia ili kitabu hicho kitoke ili Watanzania wapate kujifunza historia vizuri,” alisema Balozi Nchimbi.
Aidha, Balozi Nchimbi alisema Mzee Songambele pia alikuwa mmoja wa viongozi waliotoa mchango mkubwa kwa nchi, taifa, chama na serikali kutokea Mkoa wa Ruvuma, akisisitiza kuwa hilo ni jambo linalostahili kuenziwa na viongozi wa kizazi cha sasa kwa kuwa waadilifu, wanaowajibika, wazalendo kwa nchi na kuwatumikia watu.
Hayati Alhaji Mzee Songambele, mwanasiasa na kiongozi mkongwe nchini, ambaye alifariki usiku wa kuamkia Jumapili ya tarehe 1 Juni, mwaka huu, alizikwa Jumatatu Juni 2, 2025 katika makaburi ya familia yaliyoko Bombambili, mjini Songea.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
08-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
08-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
08-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
08-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
08-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
08-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
08-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
08-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
08-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
08-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
08-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
08-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
08-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
08-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
08-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
08-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
08-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
08-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
08-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
08-12-2025