MKANDARASI WA MAJI, UJENZI HOSPITALI SUMBAWANGA DC 'WAMCHEFUA' CHONGOLO, AWATULIZA WALIOMSIMAMISHA NA NDOO ZA MAJI
Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Komredi Daniel Godfrey Chongolo ameonekana kutoridhishwa na hatua ya Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini, ambapo ameagiza Serikali mkoani Rukwa pamoja na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kutuma timu ya uchunguzi ili kubaini kinachokwamisha mradi huo kukamilika, huku ukionekana kutekelezwa chini ya kiwango cha ubora na thamani ya fedha kilichopelekewa hadi sasa.
Mbali na kutoridhishwa na ujenzi huo wa hospitali unavyotekelezwa, Komredi Chongolo pia alionekana kukerwa na mkandarasi wa Mradi wa Maji wa Ilemba, Jimbo la Kwela, ambaye pamoja na RUWASA Mkoa wa Rukwa kumwekea msukumo ili ajenge kwa kasi ya kukamilisha ndani ya muda wa mkataba, bado ameendelea kusuasua huku akitoa visingizio vingi vya kutomaliza kazi hiyo kwa wakati ili wananchi wa Kata ya Ilemba, Vijiji vya Ilemba A na B na Kata ya Kaswepa, wapate maji safi na salama ya kutumia.
“Mkuu wa Wilaya, hakuna kucheka na waliopewa kazi hizi. Tukiacha hali hii, mambo hayataenda na hiyo sio sawa hata kidogo. Hatuwezi kuacha mambo yaende namna hii. Tutakuwa hatutendi haki na tutakuwa hatujitendei haki wenyewe na nafasi zetu za kuwatumikia wananchi. Wananchi wanachotaka ni huduma. Huko aliko anakosema anauguliwa, kuna Mkuu wa Wilaya mwenzako, wasiliana nae upate uhakika na akija aje na Ushahidi wa kuwa alikuwa anauguliwa.
“Vinginevyo ikifika tarehe 30 mwezi huu ambao mkataba wake ulikuwa unakamilika, asiongezewe mkataba. Tusitengeneze mazingira ya watu kucheza na miradi ya maendeleo na fedha za umma kama zao binafsi. Wekeni utaratibu, mwezi mmoja hajamaliza kazi mnavunja mkataba na mtengeneze mbadala kwa kutumia Force Account. Tunataka watu wapate maji, sio vinginevyo,” amesema Chongolo.
Komredi Chongolo ametoa maelekezo hayo Oktoba 10, 2023 akiwa katika Kata ya Mtowisa na Ilemba, mara baada ya kukagua mradi huo wa Maji wa Ilembo wa Tsh. 1.9 bilioni ambao bado uko asilimia 27 na hospitali ya wilaya iliyoanza kujengwa tangu Disemba 2021 na mkandarasi aitwae Kuyella Enterprises, huku ukitakiwa kukamilika Machi 2022, lakini hadi alipofika mahali hapo kuutembelea na kuukagua, ulikuwa haujakamilika.
Katika hatua nyingine msafara wa Katibu Mkuu huyo wa Chama cha Mapinduzi, umesimamishwa maeneo ya Mwela, Mtowisa, Msia, Talanda, Milepa na Kinambo, Milepa akelekea Kioze na Ilemba, ambapo wananchi walitaka awasikilize changamoto zao na kuzitolea maelekezo ya kuzitafutia ufumbuzi.
Katika eneo la Kijiji cha Mwela, Kata ya Mtowisa, watu mbalimbali wakiwemo akina mama na vijana kijiji hicho, kilichopo Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini walisimamisha msafara wakiwa na ndoo za maji, wakitaka awaondolee kero ya uhaba wa maji na namba ya utambulisho wa kijiji hicho.
"Huduma za afya tunazo...umeme tunao...barabara inapitika...hata pembejeo za kilimo tunapata. Hatuna tatizo na huduma zingine Katibu Mkuu wa CCM. Changamoto zetu hapa ni mbili tu, maji haya unavyoyaona si salama wala si safi. Lakini pia tuna changamoto ya namba ya kijiji chetu hiki kutotambuliwa huko wilayani," alisema mwananchi aliyejitambulisha kuwa ni Mwenyekiti wa Wananchi hao.
Kufuatia hali hiyo Komredi Chongolo aliwatuliza wananchi hao kwa kutoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Mhe. Nyakia Ally kuhakikisha changamoto za wanakijiji hao zinatatuliwa ndani ya muda mfupi, ikiwa ni pamoja na kukutana nao kwenye kikao akiwa na timu yake ya wataalam kutoka wilayani, siku ya Ijumaa, wiki hii ili wajadiliane nao namna ya kutatua kero hizo kwa njia shirikishi. Ndugu Chongolo aliahidi kufuatilia suala hilo kwa ukaribu.
Ndugu Chongolo alimwagiza Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, kwa kutumia RUWASA, wapeleke gari la kuchimba kisiama katika kijiji hicho kwa haraka, wakati wakiendelea kutafuta vyanzo vingine vya uhakika, baada ya Meneja wa RUWASA kutoa taarifa kuwa katika mipango yao kijiji hicho kiko ndani ya maeneo ambayo yamepangiwa mradi wa maji utakaogharimu Tsh. 1.3, utakaokuwa mwarobaini wa kero hiyo.
Mbali ya kutembelea miradi hiyo ya Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya, mradi wa Maji Ilemba na kuzungumza na wananchi katika maeneo hayo, pamoja na kwingine alikosimamishwa, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Chongolo pia alitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Kaoze na kuzungumza na wananchi wa kata hiyo, kabla ya hitimisha ziara yake Jimbo la Kwela, kwa kuzungumza na wananchi wa Kata ya Kilyematundu, Sumbawanga Vijijini.
KIPINDI MAALUMU
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
09-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
09-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
09-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
09-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
09-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
09-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
09-06-2026