Makamu wa Pili wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amewaasa wanafunzi wa kidato cha sita kuzidisha jitihada katika masomo ili kuweza kupata viongozi bora na weledi wa baadae watakaoliletea heshima Taifa letu
Ameyasema hayo kwakati akikabidhi futari kwa wanafunzi wanaoishi dahalia mbali mbali kisiwani Pemba kwa lengo la kuwarahisishia upatikanaji wa ftari katika kipindi hichi cha mwezi mtukufu wa ramadhani.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt Hussen Mwinyi imeamua kuftari na wanafunzi wanaoishi katika madahalia kwa njia ya kuwapeleka futari kwenye maskuli yao jambo ambalo litawasaidia kukidhi mahitaji yao hasa katika mwezi mtukufu wa ramadhani.
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwa mkakati wa Serikali ya Awamu ya Nane(8) ni kuhakikisha wanafunzi wanaoishi katika madahalia na sehemu nyengine wanasoma kwa utulivu ili Taifa liweze kupata wataalamu bora na viongozi wazuri wa baadae.
Mhe. Hemed amesema Serikali itaendelea kulipa kipao mbele suala la elimu kwa kuimarisha miundombinu ya elimu sambamba na kuboresha mikopo ya elimu ya juu kwa wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu kwa lengo la kuhakikisha Zanzibar inapata matokeo mazuri pamoja na kuzalisha wataalamu wenye uweledi katika kada mbali mbali.
Sambamba na hayo Mhe. Hemed amesema Serikali inaangalia uwezekano wa kujenga dahali ya kisasa katika skuli ya Madungu Sekondari pamoja na kuijenga ya ghorofa skuli ya Sekondari ya Shamiaani ili kupunguza changamoto ya uhaba wa madarasa sambamba na kuweka mazingira bora ya kusomea na kujifundishia kwa wanafunzi skulini hapo.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. LELA MOHAMMED MUSSA amesema kuwa Serikali itaendelea kutoa misaada ya aina mbali mbali kwa wanafunzi kwa lengo la kuwaondolea changamoto wanazokumbana nazo wakiwa maskulini hasa wanafuzi waoishi katika madahalia.
Waziri LELA amemshukuru Makamu wa Pili wa Rais kwa msaada alioutoa kwa wanafunzi hao na kuahidi kuwa utatumika kama ulivyokusudiwa na kuwataka wanafunzi waliopatiwa msaada huo kuongeza bidii katika masomo yao na kupata matokeo mazuri katika mitihani yao ili Taifa liweze kupata wataalamu wazalendo watakaolipigania Tifa lao.
Akitoa shukrani kwaniaba ya wanafunzi wenzake mwanafunzi wa Kidato cha Tano (5) Skuli ya Sekondari ya Fidel Castro OMAR MOHAMMED SHAALI ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwawekea miundombinu mizuri ya kujifunzia sambamba na kuwapatia msaada huo jambo ambalo linapelekea kuondosha changamoto zinazowakabili wakiwa mashuleni hasa kwa wanafunzi wanaoishidahalia.
Aidha mwanafuzi OMAR amemuahidi Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar kuwa watahakikisha wanasoma kwa bidii na maarifa ili waweze kufaulu vizuri katika masomo yao na kutimiza malengo waliojiwekea. .
Miongoni mwa skuli zilizopatiwa ftari hio ni pamoja na Skuli ya madungu sekondari,Fidel Castro, Chuo Cha Kiislamu Kiuyu, Dkt. Amani Micheweni, Idrisa Abdulwakili Kizimbani, Utaani, Wete Sekondari pamoja na kituo cha kulelea yatima Micheweni Pemba.
Wakati huo huo Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar amekabidhi futari kwa wafanyakazi wa Kitengo cha Uratibu wa shuhuli za Chama cha Mapinduzi, Viongozi na watendaji wa Chama hicho katika Mikoa miwili ya kichama.
KIPINDI MAALUMU
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
09-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
09-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
09-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
09-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
09-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
09-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
09-06-2026