Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Ndugu.Dkt Hussein Ali Mwinyi amesema Chama cha Mapinduzi kinatambua na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na Jumuiya ya wazazi Tanzania katika kuhakikisha CCM inaendelea kushikilia dola awamu kwa awamu
Ameyasema hayo katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla katika uzinduzi wa sherehe za Wiki ya wazazi Kitaifa zinazofanyika Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi.
Dkt Mwinyi amesema Jumuiya ya wazazi imekuwa ikifanya kazi nzuri katika kusimamia elimu, maadili na malezi bora kwa watoto yenye kufuata utamaduni wa Kitanzania jambo ambalo linaendelea kuiletea heshima kubwa Tanzania.
Amesema kuwa jumuiya ya wazazi imekuwa mstari wa mbele katika kupiga vita vitendo vya ukatili, unyanyasaji na udhalishaji wa kijinsia jambo ambalo linazorotesha nguvu kazi na maendeleo ya Taifa hivyo ni wajibu wa kila mwanajumuiya kuhakikisha anasimama imara katika kupinga vitendo hivi.
Rais Dkt. Mwinyi amesema mtaji wa chama chochote cha siasa ni wanachama hai hivyo ameitaka Jumuiya ya Wazazi kuendelea kuhamasisha wananchi kujiunga na CCM, kuwapa elimu ya kupiga kura pamoja na kuwajenga kuwa na utayari wa kukipigia kura kwa wingi chama cha Mapinduzi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020-2025.
Aidha Makamu Mwenyekiti Mwinyi amewasisitiza viongozi kushuka chini kwa wanachama na kufanya ziara ya kuzitembelea jumuia mbali mbali pamoja na kushika kwa wananchi kusikiliza changamoto zinazowakabili na kuziwasilisha Serikali kupatiwa ufumbuzi kwa maslahi ya chama na serikali.
Rais Dkt Mwinyi amesasisistiza kuwataka Watanzania kuwa Umoja na Mshikamano kwa kuweka mbele maslahi ya CCM hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu ujao ili CCM iendelee kushinda kwa kishindo na kudhikilia madaraka.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa anaefanyia kazi zake Zanzibar Ndugu DOGO IDDI MABROUK amesema Jumiiya ya Wazazi itaendelea kutoa elimu na kuhamasisha juu ya malezi bora ya watoto kwa kutambua tamaduni zao ambazo zinaonekana kutoweka na kusababisha mmong'onyoko wa maadili jambo linalopelekea kuongezeka kwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia hasa kwa wanawake na watoto.
Ndugu DOGO amesema kupitia Jumuiya ya wazazi itahakikisha sera tano muhimu za jumuiya hio zinatiliwa mkazo katika utekelezaji wake ikiwa ni pamoja na elimu, malezi, utamaduni, mazingira na afya ili kuhakikisha CCM inakuwa na wanachama wenye uweledi na wenye kufuata maadili kama sera na miongozi ya chama inavyoongoza.
Akiwasalimia wananchi wa Mkoa wa Katavi Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Mizengo Kayanza Pinda amesisitiza umoja na mshikamano kwa Watanzania wote ambao hujenga upendo miongoni mwao na kupelekea amani na utulivu ambao ndio ngao na muhimili mkubwa wa maendeleo ya Taifa.
Mhe. Pinda amewataka wanakatavi na watanzani wote kuendelea kujiandikisha katika daftari la kupigia kura ili kuweza kupata nafasi ya kukipigia kura kwa wingi chama cha Mapinduzi na kuendelea kukiweka madarakani.
Pinda amesema uhifadhi wa mazingira ni jambo la lazima kwa kila Mtanzania na kuwaomba kuacha tabia ya kukata miti na kuchoma moto kiholela misitu ya hifadhi na badala yake wajenge tabia ya kupanda miti kwa kuhifadhi mazingira.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
08-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
08-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
08-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
08-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
08-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
08-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
08-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
08-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
08-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
08-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
08-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
08-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
08-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
08-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
08-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
08-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
08-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
08-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
08-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
08-11-2025