NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amewataka viongozi wa chama na jumuiya wanaohusika na masuala ya uenezi,itikadi na mafunzo kwenda na wakati wa mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanayoleta tija katika ushindani wa kisiasa nchini
Wito huo ameutoa wakati akifungua mafunzo kwa makatibu wa siasa,uenezi,itikadi,hamasa na chipukizi pamoja na elimu na malezi wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya zake ngazi za majimbo,wilaya na mikoa minne ya CCM Unguja yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Fuji Bububu Zanzibar.
Dkt.Dimwa, ameeleza kuwa viongozi hao wana jukumu kubwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi kwani wanatakiwa kufafanua sera na miongozo,kuhamasisha,kueneza uetekelezaji wa ilani,kutoa mafunzo kwa wanachama pamoja na kujibu hoja mbalimbali za upotoshaji zinazotolewa na vyama vya upinzani kwa dhamira ya kuchafua na kuhujumu mambo mema yanayotekelezwa na Chama za serikali zake.
Alisema siasa za zama za sasa zinafanyika sana katika mitandao ya kijamii na zinasambaa kwa kasi kubwa kuliko katika majukwaa ya kisiasa ya kawaida na kwamba ni lazima viongozi hao waende sambamba na kasi hiyo katika kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi kuamini kuwa CCM ndio chama pekee chenye dhamira ya dhati ya kuwaletea maendeleo endelevu.
Katika maelezo yake amewasisitiza viongozi hao kuendeleza utamaduni wa kujibu hoja za wapinzani na kufafanua kwa undani utekelezaji wa ilani katika maeneo yao panapotokea jambo lolote la upotoshaji hasa kwa ngazi za majimbo,wilaya na mikoa na kuacha tabia za kusubiri kazi hizo zifanywe na ngazi za kitaifa pekee.
“Nasaha zangu kwenu fanyeni kazi kwa mujibu wa majukumu yenu jibuni hoja kwa hoja sio matusi wala ubabaishaji kwani chama chetu kinatekeleza majukumu yake kwa uhalisia zaidi kwa kila nyanja.
Tangazeni utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 namna ilivyofanyika katika maeneo yenu ili wananchi na wanachama wa chama cha mapinduzi, ambao ndio mtaji wetu wa kisiasa waelewe ili waweze kufanya maamuzi ya kuwapigia kura za ndio wagombea wetu katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025”.alisema Dkt.Dimwa.
Kupitia hafla hiyo Dkt.Dimwa, alisisitiza viongozi hao kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uandikishaji wa daftari la wapiga kura kwa awamu ya pili ili kupata watu wenye sifa za kuwapigia kura wagombea wa CCM.
Aliwataka viongozi hao kuepuka makundi yasiofaa ya kutumiwa kwa maslahi binafsi na baadhi ya viongozi na wanachama ndani kwa dhamira ya kutengeneza migogoro isiyofaa ndani ya taasisi hiyo.
Pamoja na hayo alibainisha kuwa Chama Cha Mapinduzi kinahitaji wabunge,wawakilishi na madiwani imara wanaofanya kazi kwa ufanisi ya kuwahudumia na kwamba kiongozi yeyote asiyetekeleza majukumu yake chama hakitompa nafasi ya kuongozakatika uchaguzi mkuu ujao.
Alifafanua kuwa ibara ya 246 (e) katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 inaeleza umuhimu wa mafunzo ya makada na viongozi wa chama kwa kudumisha na kuandaa mafunzo ili kuendeleza na kukuza elimu ya itikadi na uzalendo kwa viongozi wa CCM.
Alisema CCM inaendelea na maandalizi ya kutekeleza ibara 5 ya katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo la mwaka 2022 inayoelekeza kuwa ushindi wa CCM ni lazima kwa ngazi zote katika uchaguzi wa serikali za mitaa pamoja pamoja na uchaguzi mkuu wa wa dola.
Naye Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya itikadi,uenezi na mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwaandaa na kuwajengea uwezo makatibu hao wakafanye kazi zao kwa ufanisi ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya upatikanaji wa ushindi mwaka 2025.
“Tunaposema hakuna mbadala wa Dk.Mwinyi 20125 tunaimanisha na sasa tunatesti mitambo yetu kwa kuandaa kimafunzo jeshi letu la kisiasa kwani mwaka mwezi octoba mwaka 2025 tunaingia katika vita ya kidemokrasia ambayo kwa tathimini zetu mpaka sasa kupitia kazi kubwa ya utekelezaji wa Ilani iliyofanywa na Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi tuna uhakika wa kupata ushindi wa zaidi ya asilimia 90”.alifafanua Mbeto.
Aliwashauri viongozi wa baadhi ya vyama vya upinzani nchini kuacha chokochoko zinazoashiria kuingiza Zanzibar katika machafuko badala yake nao watumie ruzuku wanazopata serikali kufanya maendeleo kuwepo kwa ushindaji wa kisera na kwamba maneno ya majukwaani hayana tija kwa wananchi.
Kuptia mafunzo hayo ziliwasilishwa mada nne zikiwemo mahusiano na vyombo vya habari,umuhimu wa matumuzi ya mitandao ya kijamii,wajibu na maadili ya viongozi wa Chama na Jumuiya(Maandalizi ya Daftari la kudumu la wapiga kura) na maandalizi ya Mikutano.
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
24-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
24-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
24-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
24-06-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
24-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
24-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
24-06-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
24-06-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
24-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
24-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
24-06-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
24-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀!!
24-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐊𝐔𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐃𝐇𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐓𝐄𝐍𝐃𝐎
24-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐀𝐕𝐔𝐌𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐔𝐙𝐄𝐌𝐁𝐄, 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐈𝐊𝐄 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐍𝐆𝐀𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈
24-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀𝐀𝐀, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐀𝐍𝐙𝐈𝐀 𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈!
24-06-2026
𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐘𝐀 𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝟏𝟎% 𝐘𝐀𝐂𝐇𝐎𝐂𝐇𝐄𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌
24-06-2026
𝐍𝐃𝐆 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐑𝐔𝐕𝐔𝐌𝐀, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐃𝐈𝐎 𝐍𝐆𝐔𝐕𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌
24-06-2026
𝐊𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐌𝐀𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
24-06-2026
𝐌𝐇𝐄. 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐀𝐍𝐀𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐃𝐀 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀, 𝐖𝐀𝐓𝐔𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐔𝐌𝐌𝐀 𝐓𝐈𝐌𝐈𝐙𝐄𝐍𝐈 𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐄𝐍𝐔 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐌𝐈𝐋𝐈𝐅𝐔: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
24-06-2026