NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amewataka viongozi wa chama na jumuiya wanaohusika na masuala ya uenezi,itikadi na mafunzo kwenda na wakati wa mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanayoleta tija katika ushindani wa kisiasa nchini
Wito huo ameutoa wakati akifungua mafunzo kwa makatibu wa siasa,uenezi,itikadi,hamasa na chipukizi pamoja na elimu na malezi wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya zake ngazi za majimbo,wilaya na mikoa minne ya CCM Unguja yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Fuji Bububu Zanzibar.
Dkt.Dimwa, ameeleza kuwa viongozi hao wana jukumu kubwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi kwani wanatakiwa kufafanua sera na miongozo,kuhamasisha,kueneza uetekelezaji wa ilani,kutoa mafunzo kwa wanachama pamoja na kujibu hoja mbalimbali za upotoshaji zinazotolewa na vyama vya upinzani kwa dhamira ya kuchafua na kuhujumu mambo mema yanayotekelezwa na Chama za serikali zake.
Alisema siasa za zama za sasa zinafanyika sana katika mitandao ya kijamii na zinasambaa kwa kasi kubwa kuliko katika majukwaa ya kisiasa ya kawaida na kwamba ni lazima viongozi hao waende sambamba na kasi hiyo katika kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi kuamini kuwa CCM ndio chama pekee chenye dhamira ya dhati ya kuwaletea maendeleo endelevu.
Katika maelezo yake amewasisitiza viongozi hao kuendeleza utamaduni wa kujibu hoja za wapinzani na kufafanua kwa undani utekelezaji wa ilani katika maeneo yao panapotokea jambo lolote la upotoshaji hasa kwa ngazi za majimbo,wilaya na mikoa na kuacha tabia za kusubiri kazi hizo zifanywe na ngazi za kitaifa pekee.
“Nasaha zangu kwenu fanyeni kazi kwa mujibu wa majukumu yenu jibuni hoja kwa hoja sio matusi wala ubabaishaji kwani chama chetu kinatekeleza majukumu yake kwa uhalisia zaidi kwa kila nyanja.
Tangazeni utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 namna ilivyofanyika katika maeneo yenu ili wananchi na wanachama wa chama cha mapinduzi, ambao ndio mtaji wetu wa kisiasa waelewe ili waweze kufanya maamuzi ya kuwapigia kura za ndio wagombea wetu katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025”.alisema Dkt.Dimwa.
Kupitia hafla hiyo Dkt.Dimwa, alisisitiza viongozi hao kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uandikishaji wa daftari la wapiga kura kwa awamu ya pili ili kupata watu wenye sifa za kuwapigia kura wagombea wa CCM.
Aliwataka viongozi hao kuepuka makundi yasiofaa ya kutumiwa kwa maslahi binafsi na baadhi ya viongozi na wanachama ndani kwa dhamira ya kutengeneza migogoro isiyofaa ndani ya taasisi hiyo.
Pamoja na hayo alibainisha kuwa Chama Cha Mapinduzi kinahitaji wabunge,wawakilishi na madiwani imara wanaofanya kazi kwa ufanisi ya kuwahudumia na kwamba kiongozi yeyote asiyetekeleza majukumu yake chama hakitompa nafasi ya kuongozakatika uchaguzi mkuu ujao.
Alifafanua kuwa ibara ya 246 (e) katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 inaeleza umuhimu wa mafunzo ya makada na viongozi wa chama kwa kudumisha na kuandaa mafunzo ili kuendeleza na kukuza elimu ya itikadi na uzalendo kwa viongozi wa CCM.
Alisema CCM inaendelea na maandalizi ya kutekeleza ibara 5 ya katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo la mwaka 2022 inayoelekeza kuwa ushindi wa CCM ni lazima kwa ngazi zote katika uchaguzi wa serikali za mitaa pamoja pamoja na uchaguzi mkuu wa wa dola.
Naye Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya itikadi,uenezi na mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwaandaa na kuwajengea uwezo makatibu hao wakafanye kazi zao kwa ufanisi ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya upatikanaji wa ushindi mwaka 2025.
“Tunaposema hakuna mbadala wa Dk.Mwinyi 20125 tunaimanisha na sasa tunatesti mitambo yetu kwa kuandaa kimafunzo jeshi letu la kisiasa kwani mwaka mwezi octoba mwaka 2025 tunaingia katika vita ya kidemokrasia ambayo kwa tathimini zetu mpaka sasa kupitia kazi kubwa ya utekelezaji wa Ilani iliyofanywa na Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi tuna uhakika wa kupata ushindi wa zaidi ya asilimia 90”.alifafanua Mbeto.
Aliwashauri viongozi wa baadhi ya vyama vya upinzani nchini kuacha chokochoko zinazoashiria kuingiza Zanzibar katika machafuko badala yake nao watumie ruzuku wanazopata serikali kufanya maendeleo kuwepo kwa ushindaji wa kisera na kwamba maneno ya majukwaani hayana tija kwa wananchi.
Kuptia mafunzo hayo ziliwasilishwa mada nne zikiwemo mahusiano na vyombo vya habari,umuhimu wa matumuzi ya mitandao ya kijamii,wajibu na maadili ya viongozi wa Chama na Jumuiya(Maandalizi ya Daftari la kudumu la wapiga kura) na maandalizi ya Mikutano.
KIPINDI MAALUMU
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
09-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
09-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
09-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
09-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
09-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
09-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
09-06-2026