NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amesema chama hicho kitaendelea kuthamini na kuendeleza kwa vitendo mahusiano mema ya kisiasa,kijamii na kiplomasia baina yake na chama cha kikomunisti cha China (CPC).
Hayo ameyasema wakati akizungumza na ujumbe wa Viongozi wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) wa Kanda ya Afrika waliofika Afisi Kuu ya CCM Zanzibar , ambapo mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha ushirikiano baina ya vyama hivyo viwili vya kisiasa.
Dkt. Dimwa alisisitiza kwamba CCM itaendelea kusimamia kwa vitendo mahusiano yake na CPC, akieleza kuwa ushirikiano huu utasaidia kuimarisha nyanja za kijamii, kisiasa, na kidiplomasia kwa maslahi ya wananchi wa pande zote mbili.
Aliendelea na kusisitiza kuwa ushirikiano wa CCM na CPC utaleta manufaa kwa maendeleo ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
"CCM itaendeleza na kusimamia kikamilifu mahusiano yetu na CPC ili kuimarisha maendeleo katika nyanja za kijamii, kisiasa, na kidiplomasia, na kuhakikisha kuwa wananchi wa pande zote mbili wanapata faida ya ushirikiano huu," alisema Dkt. Dimwa.
Aidha, Dkt. Dimwa aliomba CPC kuangalia uwezekano wa kusaidia CCM Zanzibar katika kujenga chuo cha kisasa cha uongozi cha Vijana kilichopo katika kijiji cha Tunguu, akisisitiza kuwa chuo hicho kitakuwa na mchango mkubwa katika kukuza uongozi wa vijana na kuwaandaa kuwa viongozi wa baadaye.
Aliongeza kuwa kupitia ziara hii, pande zote mbili zitabadilishana uzoefu na mawazo kuhusu ushirikiano wa kibiashara, ambapo Zanzibar itakuwa na fursa ya kuuza bidhaa zake kama karafuu na viungo (Spaces) nchini China, huku China nayo ikileta bidhaa zake Zanzibar.
Dkt. Dimwa pia alizungumzia maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, akisema kuwa CCM imejipanga vyema na itapata ushindi mkubwa kutokana na utekelezaji mzuri wa ilani yake, ambayo imekidhi mahitaji ya wananchi.
Aliomba CPC kuendelea kutoa msaada katika kuendeleza programu za kuwajengea uwezo wa kitaaluma na ujuzi viongozi na watendaji wa CCM ili waweze kuendana na mahitaji ya kisiasa ya zama za sasa.
Akizungumzia mchango wa China kwa Zanzibar, Dkt. Dimwa alikumbuka mchango wa Rais wa China, Mao Zedong, ambaye alifanya kazi kwa karibu na Rais wa kwanza wa Zanzibar, Marehemu Abeid Amani Karume, katika kuijenga Zanzibar na kutambua Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.
Aliongeza kuwa serikali ya China imekuwa ikisaidia katika sekta za elimu, afya, uvuvi, miundombinu, na kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo wadogo kupitia mafunzo na zana za kisasa.
Pia, alitoa shukrani kwa China kwa msaada wake katika ujenzi wa Chuo cha Kisasa cha Uongozi cha Mwl. Nyerere cha Kibaha, kinachotoa mafunzo ya elimu ya juu ya masuala ya uongozi na fani mbalimbali kwa watendaji wa Chama,Serikali,sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.
Dkt. Dimwa alisisitiza kuwa dhamira ya serikali ya Zanzibar chini ya Rais Dkt. Hussein Mwinyi ni kuhakikisha kila mwananchi anapata maisha bora na kwamba kasi ya ukuaji wa uchumi wa Zanzibar inaendelea kuimarika kwa nguvu.
Naye Naibu Mkuu wa Ofisi ya Kanda ya Afrika katika Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara na Kiongozi wa Idara ya Kimataifa ya Kamati Kuu ya CPC, Cde. Liang Anping, alisema kuwa CPC na China wanajivunia kuwa na mahusiano imara na serikali ya Tanzania na Zanzibar.
Alisisitiza kuwa CPC itaendelea kutoa ushirikiano wa dhati kwa Zanzibar kupitia Tanzania, hasa katika kuimarisha mafunzo ya uongozi na mipango endelevu ya kukuza uchumi wa Zanzibar.
Cde. Liang alieleza kuwa serikali ya China imejizatiti kuunga mkono juhudi za maendeleo za nchi za Afrika, hasa Tanzania, na kuhakikisha zinajitegemea kiuchumi.
Aliongeza kuwa China inaridhishwa na maendeleo ya Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais Dkt. Hussein Mwinyi, ambao wamefungua milango ya uwekezaji na diplomasia kwa manufaa ya nchi zote mbili.
"China itaendelea kutoa fursa za kubadilishana ujuzi na uzoefu kwa wataalamu wa fani mbalimbali. Mapendekezo, ushauri, na maombi yaliyowasilishwa yatafanyiwa kazi kwa vitendo," alisisitiza Cde. Liang.
Aidha, Cde. Liang aliongeza kuwa Zanzibar ina mazingira mazuri ya uwekezaji na inavutia wawekezaji kutokana na sera za China kiuchumi, na kwamba baada ya ziara hii, wanatarajia kuimarisha ushirikiano na Zanzibar kwa manufaa ya pande zote mbili.
🔰 𝐀𝐆𝐎𝐒𝐓𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎, 𝐔𝐉𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀 𝐍𝐀 𝐔𝐎𝐍𝐆𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀!
01-08-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀: 𝐌𝐀𝐑𝐈𝐃𝐇𝐈𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐁𝐎𝐑𝐄𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐀
01-08-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈𝐌𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐒𝐇𝐔𝐉𝐀𝐀 𝐃𝐎𝐃𝐎𝐌𝐀
01-08-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐓𝐇𝐈𝐁𝐈𝐓𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐇𝐔𝐃𝐔𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐘𝐀𝐌𝐀 𝐓𝐀𝐖𝐀𝐋𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
01-08-2026
𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐌𝐏𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
01-08-2026
🚆 𝐓𝐔𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐄 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
01-08-2026
ZIARA YA RAIS WA MISRI-TANZANIA
01-08-2026
🔰 CCM NA ACT-WAZALENDO WASAINI MARIDHIANO YA PAMOJA YA KISIASA ZANZIBAR
01-08-2026
🎉 𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀, 𝐃𝐊𝐓. 𝐀𝐒𝐇𝐀-𝐑𝐎𝐒𝐄 𝐌𝐈𝐆𝐈𝐑𝐎! 🔰
01-08-2026
🔰𝐍𝐀𝐈𝐁𝐔 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐁𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐇𝐀𝐋𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐔𝐑𝐈 𝐊𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐙𝐀
01-08-2026
🔰𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈𝐌𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝟐𝟎𝟐𝟔!
01-08-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
01-08-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
01-08-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
01-08-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
01-08-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
01-08-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
01-08-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
01-08-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
01-08-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
01-08-2026