CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimempongeza kwa dhati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Mwinyi kwa kuendelea kujali na kuwajengea mazingira rafiki wafanyakazi nchini kwa kuanza kutoa posho ya nauli ya kuwapeleka kazini pamoja na kuongeza posho ya likizo.
Pongezi hizo zimetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, katika mahojiano maalum huko Afsini kwake Kisiwandui.
Alisema Chama Cha Mapinduzi kimeridhishwa na uamuzi huo wa busara,hekima,utu na mapenzi ya dhati kwa wafanyakazi nchini yatakayoongeza ari,ufanisi na uwajibikaji wenye viwango katika sehemu za kazi.
Katika maelezo yake Katibu huyo Mbeto, alisema Rais Dkt.Mwinyi ameendelea kuenzi kwa vitendo dhamira ya CCM ya kuhakikisha wananchi wa makundi mbalimbali wanaendelea kupata maendeleo endelevu bila ya kujali tofauti za kisiasa,kidini na kikabila.
“Tunampongeza sana Rais wetu Dkt.Hussein Ali Mwinyi kwa kazi kubwa anayofanya ya kuinua maslahi ya makundi mbalimbali hivyo nasaha zangu naomba tuendelee kumuamini na kumuunga mkono”, alisema Mbeto.
Alisema uongozi wa Dk.Mwinyi unaendelea kuandika historia kubwa na iliyotukuka nchini kwa kuchukuwa hatua, kuanza kutoa Posho la nauli za kwenda kazini na kurudi nyumbani ya TZS. 50,000 kwa watumishi wote wanaostahiki kulipwa posho na Jumla ya TZS. 34,099,500,000 zimetengwa na Serikali kwa ajili ya posho la usafiri.
Sambamba na hilo Rais wa Zanzibar Mwinyi ameeleza dhamira yake ya kuhakikisha serikali inaongeza fedha kwa ajili ya posho ya likizo ya jumla ya TZS. 2,523,814,700 zimetengwa na Serikali kwa ajili ya likizo katika bajeti mpya ya mwaka wa fedha 2024/2025.
Katibu huyo wa Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar Mbeto, amesema kupitia hotuba ya Dk.Mwinyi,ameelezea hatua zilizopigwa na serikali katika kutimiza malengo ya kufikia ajira 300,000 zilizotajwa katika Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 ambapo kwa sasa tayari amefikia jumla ya ajira 187,651 sawa na asilimia 104 ya lengo la ajira 180,000 katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.
Mbeto, alisema mafanikio yanayoendelea kupatikana katika sekta mbalimbali nchini yanatokana na matunda ya utekelezaji mzuri wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025.
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
29-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
29-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
29-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
29-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
29-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
29-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
29-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
29-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
29-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
29-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
29-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
29-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
29-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
29-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
29-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
29-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
29-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
29-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
29-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
29-05-2026