KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, amewasihi wananchi kuwa na tahadhari dhidi ya vyama vya upinzani vinavyoendeleza siasa za choko choko,fitna na uchochezi huku wakikosa sifa ya kupigania maendeleo na kukosa ujasiri wa kutetea maslahi ya umma.
Amesema njia pekee ya kuweka nchi katika hali za Udiwani,Ubunge, Uwakilishi na Urais ili viendelee kuwa wasindikizaji na wapiga porojo katika vijiwe na maskani zao.
Wito huo aliutoa wakati akitoa akichambua masuala mbali mbali ya kisiasa nchini, alieleza kuwa wapo baadhi ya viongozi wa kisiasa wameku mstari wa mbele kutoa kauli za kuingiza nchi katika machafuko ili waweze kuonekana ni majasiri mbele ya wafuasi wao na kusahau kuwa Zanzibar inaongozwa na utawala wa kisheria.
Mbeto,alisema wananchi hawapaswi kuviunga mkono vyama vya upinzani kwakuwa havina sera wala ajenda ya kupigania maendeleo pia hawana uchungu na si watetezi wa rasilimali za Taifa huku akiwataka ACT-Wazalendo kuacha siasa za kuwachonganisha wananchi dhidi ya Serikali yao.
Alisema Chama cha ACT-Wazalendo wamekuwa wakimchafua na kumdhihaki Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kupitia mitandao yao ya kijamii huku wakimtaka atimize matakwa yao ya maridhiano ya kisiasa hali inayoonyesha kuwa viongozi hao hawana chembe ya utu,busara na nidhamu za uongozi.
“Hao jamaa kwa sasa wamechanganyikiwa kwani hawana tena cha kwenda kuwambia wafuasi wao 2025, mambo yote tayari Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi kashamaliza utekelezaji wake.
Kwa sasa wanachofanya ni kuzunguka kila kona kutukana na kutoa kauli zisizofaa kwa serikali na viongozi wake yaani wanatoboa jahazi ambalo nao ni wasafiri.”, alisema Mbeto.
Akitoa ufafanuzi juu ya zabuni mbali mbali zinazotangazwa na Serikali kuwa zote zinafuata taratibu zote za kisheria na makampuni yanayoshinda zabuni hizo ndio yanayopewa.
Alisema kitendo cha ACT-Wazalendo kudai kuwa kampuni zinazoshinda zinakuwa na mkono wa Viongozi wa Serikali ni upotoshaji unayotakiwa kupuuzwa vikali kwani madhara yake ni makubwa.
Mbeto, akizungumzia juu ya kauli za ubaguzi wa ukanda na ukabila zinazotolewa wazi na baadhi ya Viongozi wa ACT-Wazalendo kupitia mikutano yao inayoendelea hivi sasa na kusisitiza kuwa siasa za aina hiyo zimepitwa na wakati toka mwaka 1964.
"Kiongozi wa kisiasa unasema hadharani eti watu fulani warudi kwao wawaachie Zanzibar yenu je nyie mnazijua vizuri asili zenu na sisi tuanze kuchimbua mlikotoka?, wenzetu mnatoka katika mstari badala ya kufanya siasa za mleta kauli za mipasho, sisi tutawajibu kwa vitendo kwani tuna kazi ya kujenga nchi.
Aliyekuwa Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya juu ya dhambi za ubaguzi leo tunaanza kubaguana kwa wenyewe kwa wenyewe ni hatari kubwa."alihoji Mbeto.
Alieleza kuwa kauli za wapinzani haziwezi kuzuia kadi ya Serikali katika utoaji wa huduma bora za wananchi.
Alibainisha kuwa CCM inaamini katika maridhiano ya kisiasa lakini sio kwa shinikizo la kauli za kibabe,uchochezi na udalali wa kisiasa na kwamba siasa za aina hiyo hazina dhamira njema ya kuivusha salama Zanzibar.
Katibu huyo wa NEC Mbeto, alieleza kuwa Chama Cha Mapinduzi kitaendeleza siasa za uvumilivu,ustaarabu huku kikinadi sera zake kwa kueleza kwa kina mafanikio na mikakati endelevu ya kuwatumikia wananchi.
Katika maelezo yake Katibu huyo, aliwasihi wanachama,viongozi na watendaji wa CCM kufanya kazi zao kwa ufanisi huku wakiongeza ubunifu katika ufutiliaji wa utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 ili iendelee kutoa majawabu chanya ya utatuzi wa changamoto za wananchi.
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
19-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
19-06-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
19-06-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
19-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
19-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
19-06-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
19-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀!!
19-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐊𝐔𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐃𝐇𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐓𝐄𝐍𝐃𝐎
19-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐀𝐕𝐔𝐌𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐔𝐙𝐄𝐌𝐁𝐄, 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐈𝐊𝐄 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐍𝐆𝐀𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈
19-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀𝐀𝐀, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐀𝐍𝐙𝐈𝐀 𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈!
19-06-2026
𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐘𝐀 𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝟏𝟎% 𝐘𝐀𝐂𝐇𝐎𝐂𝐇𝐄𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌
19-06-2026
𝐍𝐃𝐆 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐑𝐔𝐕𝐔𝐌𝐀, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐃𝐈𝐎 𝐍𝐆𝐔𝐕𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌
19-06-2026
𝐊𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐌𝐀𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
19-06-2026
𝐌𝐇𝐄. 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐀𝐍𝐀𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐃𝐀 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀, 𝐖𝐀𝐓𝐔𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐔𝐌𝐌𝐀 𝐓𝐈𝐌𝐈𝐙𝐄𝐍𝐈 𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐄𝐍𝐔 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐌𝐈𝐋𝐈𝐅𝐔: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
19-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐎𝐑𝐔𝐃𝐈 𝐍𝐘𝐔𝐌𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐒𝐋𝐀𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐋𝐈𝐌𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐎𝐑𝐎𝐒𝐇𝐎: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
19-06-2026
𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
19-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐒𝐈𝐀𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐓𝐀𝐀𝐑𝐀𝐁𝐔 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔𝐋𝐈𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐂𝐇𝐈
19-06-2026
𝐕𝐈𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐕𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐀𝐌𝐈𝐈 𝐋𝐈𝐍𝐃𝐈 𝐕Y𝐀𝐌𝐒𝐇𝐔𝐊𝐔𝐑𝐔 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐈𝐒𝐈𝐘𝐎 𝐍𝐀 𝐑𝐈𝐁𝐀
19-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐈𝐍𝐀𝐓𝐇𝐀𝐌𝐈𝐍𝐈 𝐉𝐀𝐒𝐇𝐎 𝐋𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐀 𝐌𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀
19-06-2026