BALOZI DKT. NCHIMBI AZURU KABURI LA HAYATI JOHN KOMBA
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, Jumapili, Aprili 21, 2024, amezuru kaburi la Hayati Kepteni (mst) John Damiano Komba na kutoa heshima zake kwenye kaburi hilo kwa kuweka shada la maua.
Dkt. Nchimbi ambaye ameambatana na Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu. Amos Makalla, Katibu wa NEC - Oganaizesheni wa CCM Taifa Ndugu. Issa Haji Gavu pamoja na Katibu wa NEC- Uchumi na Fedha Ndugu Dk. Frank George Haule Hawassi, pia alipata wasaa wa kuwasalimia na kuwapatia pole familia, ndugu, jamaa, marafiki na wananchi wa Kijiji cha Lituhi, alipozikwa Kepteni Komba.
Hayati Komba, ambaye alikuwa mhamasishaji mkuu wa CCM, akiwa pia amefanya kazi kubwa ya nchi, kupitia kazi za sanaa, na aliwahi kuwa Mbunge wa Majimbo ya Mbinga Magharibi na Nyasa, kwa nyakati tofauti, kwa tiketi ya CCM, alifariki dunia mwaka 2015 tarehe 28 mwezi Februari.
Akiwa hapo Lituhi, Dkt. Nchimbi, amekutana na familia na wananchi wa maeneo ya karibu waliojitokeza kuungana nae katika kuzuru kaburi la Komba na kumuombea apumzike kwa amani.
”Kwa niaba ya viongozi wenzangu na wanachama wote wa CCM, tumekuja mahali hapa kuona kaburi la aliyekuwa mkuu wa vikosi vya sanaa vya CCM na ni kwa sababu ya kuthamini na kutambua mchango mkubwa katika kushiriki na kuandaa Taifa, vita ya kuitetea Tanzania dhidi ya Uganda, kutangaza na kutoa elimu juu ya ugonjwa wa Ukimwi, kuimarisha sanaa kwa mziki wa jadi na wa kisasa pamoja na mengine mengi yenye msingi imara kwa Taifa letu. CCM itaendelea kuthamini na kuhakikisha aliyoyaanzisha hayati Kepteni Komba hayapotei bure,” amesema Dkt. Nchimbi.
Naye, Dkt. George John Komba kwa niaba ya familia ya marehemu Komba, amesema;
“Tunatoa shukrani kwa CCM kuanzia kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na viongozi wote wa taifa, mkoa, wilaya , kata, matawi, mashina na wajumbe wote kwa kuedelea kukumbuka kazi ya hayati Kepteni Komba ambaye kwetu ni Baba lakini kwenu ni askari jasiri ambaye amepigana na kushiriki katika kampeni za CCM kupata ushindi wa kishindo katika awamu zote.
”Familia tunawahakikishia tutaendelea kuwa wananchama waadilifu wa CCM sababu mafanikio yetu sote ni yanatokana na CCM na alituachia urithi kwa kusema isitokee hata mmoja akahama kwenda upande tofauti na CCM nasi tunaahidi kukienzi na kuwa wanachama wa hai.”
ποΈ21 Aprili, 2024
πLituhi - Ruvuma
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
27-10-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
27-10-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
27-10-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
27-10-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
27-10-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
27-10-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
27-10-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
27-10-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
27-10-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
27-10-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
27-10-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
27-10-2025
TAARIFA KWA UMMA
27-10-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
27-10-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
27-10-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
27-10-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
27-10-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
27-10-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
27-10-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
27-10-2025