WAKASUVI AMEFIKWA MAUTI KATIKATI YA JUKUMU ZITO: DKT. NCHIMBI
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amesema kuwa kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora Ndugu Hassan Mohamed Wakasuvi ni pigo kubwa, si kwa mkoa huo pekee, bali Chama, Serikali na taifa zima kwa ujumla, ambapo amefikwa na mauti akiwa ni Mwenyekiti wa Kamati Ndogo, iliyopewa jukumu la kuangalia namna ya kukiboresha Chama Cha Mapinduzi.
Dkt. Nchimbi amesema kuwa Komredi Wakasuvi alikuwa mmoja wa viongozi shupavu wa Chama Cha Mapinduzi, kuanzia mkoani kwake, hadi ngazi ya taifa, ambapo kutokana na uwezo na uadilifu wake katika kutimiza majukumu yake kwa ufanisi na ushirikiano tangu alipochanguliwa kuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa CCM, mwaka 2007, aliendelea kuaminiwa hadi kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, nafasi aliyokuwa nayo hadi mauti yalipomfika.
Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Nchimbi amesema hayo alipokuwa akitoa salaam za pole na rambirambi kwenye msiba wa Mzee Wakasuvi, kabla ya mazishi ya kiongozi huyo, Jumamosi Februari 24, 2024, katika Kijiji cha Mabama, Wilaya ya Uyui, mkoani Tabora, uliohudhuriwa pia na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, aliyemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
“Kiwango cha kuaminiwa Mzee Wakasuvi kilikuwa ni kikubwa sana. Mbali ya kuwa Mwenyekiti wa Mkoa na Mjumbe wa NEC ya CCM Taifa, pia alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu. Lakini pia alikuwa Mwenyekiti wa Kamati iliyopewa jukumu la kuangalia namna ya kukiboresha Chama chetu. Makamu wake alikuwa ni Mzee Wassira (Steven).
“Wanauliza watu maswali mbalimbali. Mimi ilikuwa imepangwa niwatembelee na kuonana nao Jumatatu (keshokutwa). Wakaniulize maswali waliyopanga kuniuliza nami nilikuwa nimejiandaa kwenda kujibu maswali hayo,” amesema Dkt. Nchimbi na kuongeza;
“Ameanza uongozi muda mrefu sana tangu Umoja wa Vijana. Wenzake wengine wako hapa akina Mzee Lukuvi (William), Mzee Luhavi (Rajabu) na wengine. Muda wote alikuwa anahamasisha maendeleo ya nchi yetu na kuchochea uimara wa CCM. Chama kimepoteza, Serikali imepoteza na Wananchi kwa ujumla wamepoteza kiongozi mahiri na shupavu. Tuna kila sababu ya kulinda na kuenzi kazi zake, kwa kuendelea kuwa na umoja, kushikamana, amani na utulivu thabiti bila kujali tofauti zetu za kisiasa, dini, kabila wala maeneo.”
Mbali ya salaam hizo, Dkt. Nchimbi pia aliwasilisha salaam za Mwenyekiti wa CCM, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo Katibu Mkuu wa CCM huyo amesema kuwa msiba huo umemgusa Mheshimiwa Rais moja kwa moja lakini hakuweza kuhuduria kutokana na ratiba ya majukumu mengine ya kikazi, nje ya nchi.
“Kama ambavyo imekuwa kawaida kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kila kunapojitokeza jambo kama hili, hapa pia amejitoa kwa uzito mkubwa tangu tu zilipotokea taarifa za msiba huu. Washauri wake wa siasa wote wako hapa. Pia ametutuma sisi wasaidizi wake, Mhe. Waziri Mkuu kwa upande wa Serikali na mimi kwa upande wa Chama kuleta salaam zake za pole kwa wanaCCM wote na Tabora kwa ujumla wenu. Nasi pia tutafikisha salaam na shukrani zenu mlizompatia yeye kwa jinsi alivyojitoa kushiriki katika msiba huu,” amesema Dkt. Nchimbi.
Mzee Hassan Mohamed Wakasuvi alifikwa na mauti siku ya Alhamis, Februari 22, 2024, baada ya kuugua kwa muda mfupi, ambapo pia alikuwa katika maandalizi ya kusafiri kikazi kwenda mkoani Pwani, Jumapili, Februari 25, 2024 kwa ratiba ya majukumu mengine ya kazi za Chama.
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
01-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
01-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
01-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
01-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
01-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
01-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
01-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
01-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
01-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
01-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
01-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
01-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
01-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
01-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
01-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
01-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
01-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
01-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
01-03-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
01-03-2026