SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR IMEAHIDI KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA MICHEZO NCHI NZIMA.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa ahadi hiyo Ikulu, Zanzibar alipojumuika kwenye chakula cha mchana na wachezaji wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 15, Karume Boys, baada ya kunyakua kombe la CECAFA nchini Uganda.
Dk. Mwinyi alisema michezo ni afya, ajira, utalii pia huwaunganisha jamii kwa watu kufurahi pamoja na kuwa kitu kimoja. Aidha, Rais Dk. Mwinyi alisema Zanzibar haitegemei utalii wa urithi pekee unaotokana na hifadhi ya Mji Mkongwe pamoja na fukwe lakini pia michezo ni utalii mkubwa na wakutegemewa.
Alisema Zanzibar inatarajiwa kuwa mwenyeji wa michuano ya AFCON mwaka 2027 hivyo imejipanga kuimarisha miundombinu ya kisasa kwenye sekta ya michezo pamoja na kushajihisha sekta ya utalii hususani hoteli na nyumba za kufikia wageni.
Naye Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Tabia Maulid Mwita alisema Wizara ilipewa dhamana na Serikali ya kuisafirisha timu hiyo ambapo Rais Dk. Mwinyi alitoa usafiri wa ndege kwa Karume Boys kama zawadi wakati wa kurejea nchini.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk. Muhamed Said Dimwa alishauri kupatiwa mafunzo maalumu ya michezo walimu wawili kwa Karume Boys. Kwa upande wake Rais wa ZFA, Suleiman Mahmoud Jabir alisema mafanikio ya ushindi wa Karume Boys yaliyokana na juhudi na ushirikiano wa wadau wengi nchini.
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
17-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
17-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
17-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
17-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
17-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
17-05-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
17-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
17-05-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
17-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
17-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
17-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
17-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
17-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
17-05-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
17-05-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
17-05-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
17-05-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
17-05-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
17-05-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
17-05-2026