RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA JUMUIYA YA WASTAAFU NA WAZEE ZANZIBAR (JUWAZA)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amezitaka mamlaka husika zinazoshughulika na masuala ya pechni na penchini jamii kwa wazee, kurekebisha na kuboresha mifumo yao ili zoezi la utoaji wa penchi kwa mwezi Julai mwaka huu kuanza bila ya kikwazo chohote.
Alizitaka mamlaka hizo kujitahidi kumaliza zoezi la usajili na uhakiki wa masuala yote muhimu yanayowahusu wazee hao yakamike ndani ya mwezi huu wa Juni ili ifikapo Julai kusiwe na kasoro zozote zitakazowakosesha wazee kupata haki yao ya pencheni.
“Nisingependa hata kidogo kwa nia njema tuliyokuwa nayo ya kuwasaidia wazee, halafu usikie Julai imefika, huyu hajapata, huyu kakosa kitambulisho, itakua hatuja wasaidia wazee” Alitahadharisha Dk. Mwinyi.
Dk. Mwinyi alitoa maagizo hayo alipozungumza na Jumuiya ya Wazee na Wastaafu, Zanzibar (JUWAZA), Ikulu – Zanzibar waliofika kumpongeza kwa hatua yake ya kuwajali na kuwaongezea pencheni na pencheni jamii.
Akizungumia changamoto ya vitambulisho kwa wazee hao hasa wakati wakupata haki zao za msingi, Rais Dk. Mwinyi alizishauri mamlaka husika kurasimisha baadhi ya vitambulisho kwa wazee hao ili wapate haki zao zote kwa wakati yakiwemo masuala ya jamii.
Alishauri kuwe na utaratibu mzuri kwa wazee hao kupata haki zao kwa wakati kusiwe na urasimu na kuwanyima haki zao za msingi.
“Hakuna ubaya wa kurasimisha vitambulisho, sio lazima vitumike “ZAN ID” au “NIDA” katika kuwapatia wazee haki zao, kama wengine hawana vitambulisho hivyo, kuwe na utaratibu kurasimisha ama kuanzishwe vitambulisho maalumu vya wazee vitakavyowaunganisha na huduma zao zote zikiwemo pensheni, pencheni jamii na masuala ya kijamii ikiwemo usafiri, afya na wepesi wa kupata huduma nyengine” alifafanua Dk. Mwinyi.
Pia Rais Dk. Mwinyi, alizishauri mamlaka zinazosimamia pencheni za wazee kushirikiana na jumuiya hiyo ya Wazee ili kubaini wazee wanaozidi ama kupungua kwenye uhakiki wao.
Alieleza kuna haja ya Taasisi za Serikali zinazoshughulikia masuala ya wazee, kukaa pamoja na kuongeza ushirikiano baina yao na JUWAZA ili kupata takwimu sashihi zinazowahusu wazee wote nchini.
Aidha, aliwaahidi wazee hao kwamba atatoa maagizo kwa uongozi wa Wizara tatu za Serikali zikiwemo Fedha, Ustawi wa Jamii na Afya, ili kwakae pamoja na wazee hao kwa lengo la kujadiliana na kuondoka na mipango mizuri Imarisha ustawi wa wazee hao kwa sasa na baadae.
“Niombe na maelekezo nitatoa, kwa Wizara tatu za Serikali, mukutane na tumu za uongozi wa Wizara ya Fedha, Ustawi wa Jamii na Afya, mjadiliane ili muondoke na mpango mzuri wa kuyafabya haya” Alisisitiza Dk. Mwinyi.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Katibu wa (JUWAZA) Salma Kombo Khamis aliiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwapatia wazee wa Zanzibar daktari maalum atakaeshughulikia masuala ya wazee kwenye hospitali kuu ya Mnazi Mmoja (Geriatrician) pamoja na wauguzi wa masuala ya wazee tu, ili kuwaondoshea usumbufu wazee wengi wanaotibiwa kwa kuondoshwa njiani tu bila ya uangalizi wa kina kwa mujibu wa hali zao.
Aidha, waliiomba Serikali kupitia vyuo vya Afya nchini kuona umuhimu wa kuongezwa kufundishwa kozi maalumu ya kada ya utaalamu wa kuwatibu na kuwashuighulikia wazee na iwe endelevu kwa manufaa ya wazee wa sasa na wabaadae.
Pamoja na kuangalia upya kada ya uzazi ambayo alieleza vyuoni inafundishwa kwa kiwango kidogo sana, hivyo aliziomba mamlaka husika kuona haja ya kuongezewa muda ili kuepusha changamoto zinazowakabili mama wajawazito kwa uchache wa wataalamu.
Pia Katibu huyo aliiomba Serikali kupitia mamlaka husika kuangalia uwezekano wa wazee kuwekwa kwenye mfumo wa mpya wa Afya ambao utawatambua rasmi Wazee, wanawake na watoto ili kuwaepushia kuwakosesha haki zao za msingi ambapo walilaumu kwamba kuna baadhi ya mifumo ya afya haiwatambui wazee hao.
Hata hivyo, wazee hao walimshukuru Dk. Mwinyi kwa uamuzi wake wakuwaongezea pencheni na pencheni Jamii kutoka kima cha chini hadi asilimia 100 na 150 kwa pencheni jamii na wastaafu.
Kwa mujibu wa Jumuiya ya Wazee na Wastaafu, Zanzibar (JUWAZA), ilianzishwa wakati wa awamu ya tano ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na mwaka 2016 ilianzishwa pencheni jamii. Wazee wote tangu mwaka 1960 ni 57,000 na wazee wa penche ni 28,000 kwa mujibu wa jumuiya hiyo.
KIPINDI MAALUMU
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
09-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
09-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
09-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
09-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
09-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
09-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
09-06-2026