CCM HAITAKI UONGOZI WA KUGAWANYA WATU KWAKUWA UNAPELEKEA MPASUKO WA NDANI YA CHAMA NA KUKWAMISHA MAENDELEO KWA WANANCHI - BALOZI DKT. NCHIMBI
"Chama Cha Mapinduzi hakitaki na kinakemea tabia ya Uongozi wa kugwanya watu kwakuwa unapelekea mpasuko ndani ya Chama na kukwamisha maendeleo kwa Watanzana." hiyo ni kauli ya Katibu Mkuu Dkt. Nchimbi wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa CCM kuanzia Mashina hadi Mkoa, Viongozi wa Serikali, Taasisi zisizo za kiserikali, Viongozi wa dini na Wazee.
Katibu Mkuu Dkt. Nchimbi amesema Chama chochote cha siasa lazima kiwe na chaguzi za kweli na hizo zinatokana na uwepo wa Haki ambayo ndiyo yenye kupelekea ushindani wa kweli.
Balozi Dkt. Nchimbi amebainisha kuwa moja ya changamoto kubwa iliyopo ndani ya CCM ni tabia ya baadhi ya viongozi wanaoshindwa na wanaoshinda kutokukubali matokeo miyoyoni mwao na matokeo yake pamoja na uchache wao lakini wanakuwa na madhara makubwa na kusema tabia hiyo iachwe mara moja kwakuwa ni ujinga na sio misingi ya demokrasia.
" Unakuta mtu kagombea na kashida lakini akimaliza kushinda anaanza kutafuta nani hakumuunga mkono ili apambane nae na kumkandamiza, hiyo ni tabia ya kijinga na haiungwi mkono, tuache mara moja " Alisema Balozi Dkt. Nchimbi
Pia, Balozi Dkt. Nchimbi ameendelea kuhimiza juu ya misingi ya haki na wajibu na kusema mti yeyote anapoingia kwenye uchaguzi anatakiwa kufahamu kila mtu ana haki sawa na mwengine hivyo ni lazia uwe na dhamira ya utumishi na wakati mwingine usipochaguliwa unatakiwa kuhisi kwamba mzigo mkubwa umekuepukia.
"Vyama vidogo vinapokataa matokeo ni wanaiiga CCM kwa kuona baadhi wa wagombea ndani ya CCM wanavyopinga matokeo ya ndani, tuache tabia hiyo mara moja"
"Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema 'Mimi nanga'atuka lakini naendelea kuamini kuwa bila CCM madhubuti nchi hii itayumba' Hivyo niwaambie ndugu zangu mtu asiyeitakia mema nchi hii atatamani kuona CCM inapasuka."
"...Tujue kwamba CCM madhubuti inaongozwa na misingi ya demokrasia na kiongozi wa kweli ni yule ambaye anakubali matokeo bila vita, mimi nilishawahi kugombeaga mara 28 na mara 4 nilishindwa lakini naelewa kuna kushinda na kushindwa na matokeo nikakubali."
"Wana CCM nchi nzima tueshimu utaratibu wa kidemorsia ndan ya CCM, tufanye chaguzi kwa haki na tukubali matokeo, kiongozi wa kweli ni mnyenyekevu na habagui, waonganishe watu wote kwa usawa sio utume vikosi vya upererezi."
ποΈ 13 Aprili, 2024
π Mpanda - Katavi
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025