Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


CCM HAITAKI UONGOZI WA KUGAWANYA WATU KWAKUWA UNAPELEKEA MPASUKO WA NDANI YA CHAMA NA KUKWAMISHA MAENDELEO KWA WANANCHI - BALOZI DKT. NCHIMBI

alternative

"Chama Cha Mapinduzi hakitaki na kinakemea tabia ya Uongozi wa kugwanya watu kwakuwa unapelekea mpasuko ndani ya Chama na kukwamisha maendeleo kwa Watanzana."  hiyo ni kauli ya Katibu Mkuu Dkt. Nchimbi wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa CCM kuanzia Mashina hadi Mkoa, Viongozi wa Serikali, Taasisi zisizo za kiserikali, Viongozi wa dini na Wazee.

Katibu Mkuu Dkt. Nchimbi amesema Chama chochote cha siasa lazima kiwe na chaguzi za kweli na hizo zinatokana na uwepo wa Haki ambayo ndiyo yenye kupelekea ushindani wa kweli.

Balozi Dkt. Nchimbi amebainisha kuwa moja ya changamoto kubwa iliyopo ndani ya CCM ni tabia ya baadhi ya viongozi wanaoshindwa na wanaoshinda kutokukubali matokeo miyoyoni mwao na matokeo yake pamoja na uchache wao lakini wanakuwa na madhara makubwa na kusema tabia hiyo iachwe mara moja kwakuwa ni ujinga na sio misingi ya demokrasia.

" Unakuta mtu kagombea na kashida lakini akimaliza kushinda anaanza kutafuta nani hakumuunga mkono ili apambane nae na kumkandamiza, hiyo ni tabia ya kijinga na haiungwi mkono, tuache mara moja " Alisema Balozi Dkt. Nchimbi

Pia, Balozi Dkt. Nchimbi ameendelea kuhimiza juu ya misingi ya haki na wajibu na kusema mti yeyote anapoingia kwenye uchaguzi anatakiwa kufahamu kila mtu ana haki sawa na mwengine hivyo ni lazia uwe na dhamira ya utumishi na wakati mwingine usipochaguliwa unatakiwa kuhisi kwamba mzigo mkubwa umekuepukia.

"Vyama vidogo vinapokataa matokeo ni wanaiiga CCM kwa kuona baadhi wa wagombea ndani ya CCM wanavyopinga matokeo ya ndani, tuache tabia hiyo mara moja"

"Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema 'Mimi nanga'atuka lakini naendelea kuamini kuwa bila CCM madhubuti nchi hii itayumba'  Hivyo niwaambie ndugu zangu mtu asiyeitakia mema nchi hii atatamani kuona CCM inapasuka."

"...Tujue kwamba CCM madhubuti inaongozwa na misingi ya demokrasia na kiongozi wa kweli ni yule ambaye anakubali matokeo bila vita, mimi nilishawahi kugombeaga mara 28 na mara 4 nilishindwa lakini naelewa kuna kushinda na kushindwa na matokeo nikakubali."

"Wana CCM nchi nzima tueshimu utaratibu wa kidemorsia ndan ya CCM, tufanye chaguzi kwa haki na tukubali matokeo, kiongozi wa kweli ni mnyenyekevu na habagui, waonganishe watu wote kwa usawa sio utume vikosi vya upererezi."

🗓️ 13 Aprili, 2024
📍 Mpanda - Katavi

alternative alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi