SAMIA: CCM ITALETA WAGOMBEA WANAOKUBALIKA
Mwenyekiti wa CCM aahidi mchujo wa haki kwa wagombea 2025
Mawazo ya wananchi kuzingatiwa ili kuimarisha ushindi kwa chama
Dodoma, tarehe 5 Februari 2025
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuwa CCM italeta wagombea wanaokubalika na wananchi katika Uchaguzi Mkuu wa 2025, ili kurahisisha uchaguzi wa diwani, mbunge na rais kutoka chama hicho.
Akizungumza leo katika kilele cha sherehe za miaka 48 ya CCM, zilizofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, Dkt. Samia alisisitiza kuwa mchakato wa kupata wagombea utazingatia haki na uwazi, kwa kushirikiana na viongozi wenzake ndani ya chama.
“Nawahakikishia wana-CCM na Watanzania kwa ujumla kuwa, tutahakikisha haki inatendeka katika mchakato wa kupata wagombea wa CCM. Lengo letu ni kuleta wagombea wanaokubalika, ili kuwapunguzia wananchi changamoto ya kuchagua mafiga matatu—diwani, mbunge, na rais,” alisema huku akishangiliwa na maelfu ya wananchi.
Kwa upande wa Zanzibar, alieleza kuwa mwelekeo huo utahakikisha upatikanaji wa diwani, mjumbe wa Baraza la Wawakilishi, na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa mujibu wa taratibu za chama.
Aidha, Dkt. Samia aliwataka wanachama wa CCM kujipanga kikamilifu kwa uchaguzi wa 2025 na kuepuka kubweteka, akiwahimiza kushiriki kikamilifu katika kampeni za chama na kutowabeza wapinzani.
Katika hotuba yake, pia aliwahimiza vijana na wananchi wote kuhakikisha wanajiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili waweze kushiriki katika uchaguzi.
Akihitimisha, Dkt. Samia aliwashukuru wana-CCM kwa imani waliyoonesha kwake, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, na Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa kuwachagua kupeperusha bendera ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2025, akisisitiza kuwa chama kitaendelea kuwa chaguo la wananchi kwa misingi yake ya haki na utumishi wa watu.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
19-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
19-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
19-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
19-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
19-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
19-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
19-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
19-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
19-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
19-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
19-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
19-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
19-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
19-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
19-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
19-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
19-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
19-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
19-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
19-03-2026