SAMIA: CCM ITALETA WAGOMBEA WANAOKUBALIKA
Mwenyekiti wa CCM aahidi mchujo wa haki kwa wagombea 2025
Mawazo ya wananchi kuzingatiwa ili kuimarisha ushindi kwa chama
Dodoma, tarehe 5 Februari 2025
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuwa CCM italeta wagombea wanaokubalika na wananchi katika Uchaguzi Mkuu wa 2025, ili kurahisisha uchaguzi wa diwani, mbunge na rais kutoka chama hicho.
Akizungumza leo katika kilele cha sherehe za miaka 48 ya CCM, zilizofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, Dkt. Samia alisisitiza kuwa mchakato wa kupata wagombea utazingatia haki na uwazi, kwa kushirikiana na viongozi wenzake ndani ya chama.
“Nawahakikishia wana-CCM na Watanzania kwa ujumla kuwa, tutahakikisha haki inatendeka katika mchakato wa kupata wagombea wa CCM. Lengo letu ni kuleta wagombea wanaokubalika, ili kuwapunguzia wananchi changamoto ya kuchagua mafiga matatu—diwani, mbunge, na rais,” alisema huku akishangiliwa na maelfu ya wananchi.
Kwa upande wa Zanzibar, alieleza kuwa mwelekeo huo utahakikisha upatikanaji wa diwani, mjumbe wa Baraza la Wawakilishi, na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa mujibu wa taratibu za chama.
Aidha, Dkt. Samia aliwataka wanachama wa CCM kujipanga kikamilifu kwa uchaguzi wa 2025 na kuepuka kubweteka, akiwahimiza kushiriki kikamilifu katika kampeni za chama na kutowabeza wapinzani.
Katika hotuba yake, pia aliwahimiza vijana na wananchi wote kuhakikisha wanajiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili waweze kushiriki katika uchaguzi.
Akihitimisha, Dkt. Samia aliwashukuru wana-CCM kwa imani waliyoonesha kwake, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, na Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa kuwachagua kupeperusha bendera ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2025, akisisitiza kuwa chama kitaendelea kuwa chaguo la wananchi kwa misingi yake ya haki na utumishi wa watu.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
08-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
08-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
08-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
08-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
08-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
08-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
08-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
08-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
08-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
08-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
08-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
08-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
08-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
08-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
08-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
08-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
08-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
08-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
08-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
08-12-2025