Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe, Hemed Suleiman Abdulla amewataka washiriki wa Mkutano wa 14 wa Mawaziri wa Biashara wa eneo huru la Biashara la Afrika kuhakikisha wanaweka mikakati imara itakayosaidia kuliunganisha Bara la Afrika katika kukuza biashara za ndani pamoja na kuimarisha nafasi ya Afrika katika Biashara za Kimataifa.
Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 14 wa Mawaziri wa Biashara wa eneo huru la Biashara la Afrika uliofanyika katika Ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
Amesema ili kuweza kufikia malengo ya Agenda 2063 ya Afrika mipango na mikakati madhubuti inahitajika ikiwemo kuboresha miundombinu ya Barabara, Reli na Viwanja vya ndege ili kurahisisha Biashara na huduma nzuri zaid.
Mhe. Hemed amesisitiza kuwezesha biashara ndogo na za kati ziweze kushiriki kikamilifu katika Biashara za kikanda na Kimataifa pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa mikopo nafuu, elimu ya biashara na masoko.
Makamu wa pili wa Rais Zanzibar amesema suala la kuwajengea uwezo watu kwa kuwekeza katika Sekta ya Elimu, Afya na mafunzo ya kiufundi ni muhimu ili kuhakikisha wanakuwa na nguvu kazi yenye ujuzi na uwezo wa kushindana katika Soko la Kimataifa.
Aidha Mhe. Hemed amewataka washiriki wa Mkutano huo kuboresha mazingira ya Uwekezaji kwa kupunguza rasimu, kuimarisha utawala bora na kuhakikisha usalama wa mitaji na mali za wawekezaji jambo ambalo litasaidia kuwavutia wawekezaji nkutoka nchi mbali mbali.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iko tayari kushirikiana na nchi wanachama wa eneo Huru la Biashara la Afrika kwa kuhakikksha kuwa biashara na Uwekezaji Barani Afrika vinaimarika na kuleta maendeleo chanya kwa wananchi wake.
Nae Waziri wa Biashara na Viwanda Zanzibar Mhe. OMAR SAID SHAABAN amesema Mkutano wa Eneo huru la Biashara la Afrika utajadili masuala muhimu katika biashara ndani ya Afrika ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa na mapinduzi ya Kijani ya Maendeleo ya Viwanda Afrika, sambamba na kuangalia kwa kina uzalishaji wa vipuri vya magari ili kuweze kunufaika na biashara katika Sekta yamagari ambayo inakua kwa kasi zaidi Barani Afrika.
Amesema kuwa eneo huru la Biashara la Afrika limeanza kuonesha matunda ambapo biashara baina ya nchi za Afrika kwa kutumia taratibu na vigezo vya AFCFTA imeanza kuongezeka na yatakapomalizika majadiliano katika masuala yaliyobakia wataweza kufanya biashara zaidi ndani ya Afrika chini ya Mkataba wa AFCFTA.
Mpema akitoa taarifa ya Shirika la Eneo huria Ulimwenguni Dkt. Samir Hamroun amesema Ili kufikia katika Afrika yenye maendeleo endelevu ni lazima nchi wanachama wa Eneo huru la Biashara la Afrika kujikita katika Teknolojia, Uvumbuzi wa mbinu na nyenzo mpya za kuimarisha biashara sambamba na kuwa na maridhiano na makubaliano ya pamoja katika ngazi za maamuzi kwa kuzingatia Mkataba wa Umoja huo.
Dkt. Samir amesema Serikali kupitia Taasisi husika ziongeze juhudi katika ukusanyaji wa mapato ya ndani, kuweka Sera rafiki za Biashara na kupunguza madeni mambo ambayo yatawasaidia katika kuimarisha Biashara, kukuza uchumi wa Taifa na Afrika kwa ujumla.
Amesema kwa kipindi ambacho Eneo huru la Biashara la Afrika lipo katika mikakati ya kuimarisha na kukuza biashara Barani Afrika inapaswa kuziangalia changamoto kama ni fursa chanya ya kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
26-01-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
26-01-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
26-01-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
26-01-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
26-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
26-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
26-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
26-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
26-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
26-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
26-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
26-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
26-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
26-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
26-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
26-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
26-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
26-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
26-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
26-01-2026