BALOZI NCHIMBI: MALEZI YA WALIMU NI MUHIMU KATIKA UJENZI WA TAIFA IMARA
Atoa wito kwa viongozi wa dini kuiombea Tanzania dhidi ya vurugu
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesema malezi na mafunzo wanayopata wanafunzi shuleni, hasa yanayosisitiza nidhamu na uwajibikaji, ni msingi muhimu katika kujenga taifa imara lenye uzalendo.
Aidha, ametoa wito kwa viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali kuendelea kuiombea Tanzania ili iendelee kuwa na amani na kuepuka athari za watu wanaotaka kuingiza nchi katika vurugu.
Balozi Nchimbi aliyasema hayo wakati wa kikao cha umoja wa wanafunzi waliosoma Shule ya Sekondari ya Uru Seminari, kilichofanyika Moshi, mkoani Kilimanjaro, baada ya ibada na mazishi ya aliyewahi kuwa Baba Gombera wa seminari hiyo, Padri Canute Mkwe Shirima AJ, mnamo Machi 20, 2025.
“Hakuna aliyesoma Uru Seminari asiyetambua mchango wa kipekee wa Padri Shirima. Tulifundishwa nidhamu, uwajibikaji, bidii kazini, na umuhimu wa kufuatilia mambo kwa umakini. Mafundisho hayo yametufanya kuwa watumishi bora katika nyanja mbalimbali za maisha,” alisema Balozi Nchimbi.
Aliongeza kuwa malezi ya walimu yana mchango mkubwa katika kujenga jamii yenye maadili na uzalendo, akisisitiza kuwa Taifa linapaswa kuthamini juhudi za walimu katika kujenga kizazi chenye maadili.
Katika kuendeleza maadili na mshikamano wa kitaifa, Balozi Nchimbi aliwasihi viongozi wa dini waendelee kuliombea Taifa na viongozi wake ili Tanzania iendelee kuwa nchi yenye utulivu.
“Nawaomba viongozi wa dini muendelee kuikabidhi nchi yetu kwa Mungu. Tuendelee kuiombea Tanzania, viongozi wake wa Serikali, CCM, na hata wa upinzani, ili Mungu aendelee kutuongoza. Kuna watu wenye nia ya kusababisha vurugu, hivyo ni muhimu sana tukaendelea kuilinda amani yetu,” alisema.
Aidha, alitoa pongezi kwa umoja wa wanafunzi waliosoma Uru Seminari kwa mshikamano waliouonyesha katika msiba wa Padri Canute, akiwahimiza kuendeleza umoja huo kwa manufaa ya jamii na Taifa kwa ujumla.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
15-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
15-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
15-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
15-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
15-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
15-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
15-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
15-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
15-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
15-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
15-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
15-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
15-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
15-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
15-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
15-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
15-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
15-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
15-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
15-03-2026