WASIRA: UCHAGUZI MKUU UTAFANYIKA, WANA-CCM, WANANCHI JIANDAENI.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema uchaguzi mkuu wa mwaka huu utafanyika kama ulivyopangwa kwa taratibu za kisheria, na kwamba hakuna chombo cha serikali wala chama cha siasa chenye mamlaka ya kuuahirisha.
Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Stephen Wasira, leo Februari 11, 2025 alipohutubia mkutano mkutano katika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.
Wasira amesema watu wanaotoa hoja kwamba uchaguzi mkuu hautafanyika hadi yawepo mabadiliko ya Katiba wanajisumbua kwa kuwa makubaliano yalishafanyika kuwa mabadiliko ya Katiba yatafanyika baada ya uchaguzi mkuu, hivyo hakuna anayeweza kuahirisha kufanyika kwa uchaguzi mkuu kwa namna yoyote.
“Tumekubaliana tumalize uchaguzi, zile sheria za uchaguzi zifanyiwe marekebisho, wabunge wanajua Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani imepitishwa na Bunge, Sheria ya Vyama vya Siasa imefanyiwa marekebisho na imepitishwa na Bunge.
“Chadema wamekuwa na msemo wao maarufu ‘no reform no election’ (kama hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi), sasa mimi hapa nasema leo uchaguzi mkuu utafanyika. Wanaosema uchaguzi hautafanyika mpaka mabadiliko yafanyike wanajisumbua, uchaguzi utafanya na Watanzania wajiandae.
“Sisi ni Chama cha siasa lazima tufanye uchaguzi ili tuendelee kuleta maendeleo ya Watanzania. Tumewaambia hakuna tunachoogopa kwa sababu hata Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 wameshindwa kuweka wagombea. Halafu wakishindwa wanasingizia CCM,” amesema Wasira.
Amesisitiza kuwa kwa taratibu za kisheria, si chombo cha serikali wala chama cha siasa kina uwezo wa kuahirisha uchaguzi mkuu, huku akifafanua kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kisheria inalo jukumu la kutangaza tarehe ya uchaguzi, lakini haina uwezo wa kuahirisha.
“Na kama kutakuwa sababu ya uchaguzi mkuu kusogezwa mbele au kuahirishwa basi ni kwa sababu ya uwepo wa vita lakini kwa bahati nzuri nchi yetu haina vita, iko salama na kazi ya kuleta maendeleo inaendelea. Hivyo hakuna chama cha siasa kinaweza kuahirisha uchaguzi na suala la mabadiliko ya Katiba ni la kisheria.
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
14-02-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
14-02-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
14-02-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
14-02-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
14-02-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
14-02-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
14-02-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
14-02-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
14-02-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
14-02-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
14-02-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
14-02-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
14-02-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
14-02-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
14-02-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
14-02-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
14-02-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
14-02-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
14-02-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
14-02-2026