DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMEZINDUWA MRADI WA KUWAJENGEA UWEZO VIJANA ILI WAWEZE KUJIAJIRI NA KUAJIRIKA KATIKA SEKTA YA UCHUMI WA BULUU
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imeeleza dhamira yake ya kuleta mageuzi makubwa kwenye sekta ya elimu kupitia Wizara yake ya Elimu na Mafunzo ya Amali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi alieleza dhamira hiyo kwenye ufunguzi wa mradi wa kuwajengea uwezo vijana kwa lengo la kuwawezesha kujiajiri na kuajirika kwenye sekta ya uchumi wa buluu huko ukumbi wa Golden Tulip, Uwanja wa ndege, Zanzibar.
Dk. Mwinyi alisema, Serikali inaendeleza jitihada mbali mbali kwa kuhakikisha inatoa elimu bora nchini katika kufikia dhamira hiyo kwa kuchukua hatua za kuboresha miundombinu ya skuli mpya ikiwemo ujenzi wa Skuli mpya za ghorofa kwa Unguja na Pemba na mafunzo kwa walimu.
Hatua nyengine, Rais Dk. Mwinyi alieleza ni kuzipatia huduma muhimu skuli hizo ikiwemo, upatikanaji wa vifaa bora vya kufundishia na kujifunzia, matumizi bora ya TEHAMA na kuwapatia vijana ujuzi na maarifa utakao wawezesha kuyakabili maisha yao na kunyanyua uchumi wa nchi.
“Kama hatutowaandaa vijana wetu, wakawa weledi wa kujua wanachokifanya, hatutofikia dhamira yetu ya kuhakikisha watu wote wakiwemo vijana wanashiriki na kunufaika na Uchumi wa Buluu” aliasa Rais Dk. Mwinyi.
Dk. Mwinyi alitaja sehemu ya ujenzi wa mradi huo ni pamoja na ujenzi wa Chuo cha kisasa cha Ubaharia na majengo utawala, ujenzi wa hosteli ya wanafunzi wa kike kwenye Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Karume yenye ukubwa wa ghorofa tatu na uwezo wa kuhudumia wanafunzi 500 kwa wakati mmoja, ujenzi wa madarasa ya kusomea na karakana zinazohusiana na masomo ya mafuta na gesi.
Aliongeza ujenzi wa vyuo vya mafunzo ya amali na vifaa vyote vinavyohitajika kwa programu zitakazotolewa na vyuo hivyo ambavyo vinatarajiwa kujengwa kwenye Wilaya za Mkoani (Chambani), Wilaya ya Micheweni (Tumbe Mashariki), Wilaya ya Kati (Jendele) na Wilaya ya Kaskazini B (Panga Tupu).
Shughuli nyengine za mradi huo wa SEBEP, Rais Dk. Mwinyi alizitaja ni pamoja kuwajengea uwezo watendaji wa Taasisi zinzozoshiriki kwenye mradi huo kwa kuwapatia nafasi za kuongeza taaluma zao, ujenzi wa kituo cha kuwapa vijana mafunzo ya kuanzisha na kuendeleza biashara zao (incubation centre) na vifaa vyake eneo la Kizimbani Unguja, ambacho kitakuwa chini ya usimamizi wa Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (ZEEA) na taasisi ya SMIDA imepewa jukumu la kuwapatia mafunzo mbalimbali vijana hao.
Rais Dk. Mwinyi alisema hatua hiyo inatoa nafasi kwa Vijana wa Zanzibar kupata fursa ya mafunzo ya amali na ufundi wa fani mbali mbali zikiwemo zinazohusiana na Uchumi wa Buluu.
Pia alitoa wito kwa vijana kuitumia vyema fursa ya mradi huo kujipatia ujuzi ili wanufaike na soko la ajira kwenye sekta ya uchumi wa buluu kwa kuweza kujiari na kupata sifa za kuajiriwa.
Dk. Mwinyi alisema mradi huo utaongeza upatikanaji wa wafanyakazi wenye taaluma kwenye shughuli za Utalii ambayo ni Sekta kiongozi katika uchumi wa Zanzibar pamoja na kuiwezesha Zanzibar kuzitumia vyema rasilimali zake za asili ikiwemo bahari, mafuta na gesi asilia katika kukuza pato la taifa na upatikanaji wa ajira kupitia sekta ya Uchumi wa Buluu.
Mradi wa kuwajengea uwezo vijana kwa lengo la kuwawezesha kujiajiri na kuajirika kwenye sekta ya uchumi wa buluu SEBEP unafadhiliwa kwa asilimia 90 na washirika wa maendeleo (AfDB) na asilimia 10 unafadhiliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, unatarajiwa kutumia dola za Marekani milioni 54 sawa na fedha za Tanzania shilingi bilioni 126.379.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
08-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
08-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
08-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
08-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
08-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
08-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
08-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
08-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
08-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
08-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
08-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
08-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
08-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
08-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
08-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
08-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
08-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
08-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
08-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
08-11-2025