RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Al hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewashukuru Waumini wa dini ya Kiislam wa Mkoa wa Kusini Unguja, kwa nia yao njema ya kumuombea dua na kuliombea dua taifa.
Amesema, utamaduni wa kuiombea dua nchi na viongozi lazima uendelezwe na udumishwe hasa wakati huu ambao dunia imegubikwa na mabalaa mengi yenye athari mbaya. Al hajj Dk. Mwinyi ameyasema hayo kwenye dua maalum iliyoandaliwa na Wazee na
viongozi wa Mkoa wa Kusini Unguja, kwa kumuombea dua yeye na taifa kwa kipindi chote cha uongozi wake. Dua hiyo imefanyika msikiti wa Ijumaa, Makunduchi Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja.
Alisema, hakuna jambo jema kwa wakati uliopo zaidi ya kumuomba Mwenyezi Mungu aiepushe nchi na mabala ya vita, mabadiliko ya taiba nchi na mazingira ikiwemo upepo mkali na mafuriko. Akizungumzia suala la amani, utulivu na mshikamano wa nchi na watu wake, Al Hajj Dk. Mwinyi alisema amani na utulivu wa nchi ndio kila kitu kwa mustakbali mwema wa maendeleo endelevu na ustawi wa taifa na uchumi wake.
Akitolea mfano mataifa ya Urusi, Ukraine, Sriya, Iraq na nchi nyngine duniani zilizogubikwa na vita pamoja na mataifa yaliyoathiriwana ukame ikiwemo Pakistani, Al hajj Dk. Mwinyi alisema dunia imekua kama Kijiji, inashuhudiwa mabalaa mengi ya vita na majanga ya kimaumbile yanavyoiathiri, hali ilizusha taharuki na uchumi wa dunia kutetereka, ikiwemo kupanda kwa gharama za maisha na uchumi wa dunia.
Al hajj Dk. Mwinyi aliongeza hali hiyo pia imeathiri sana mataifa yanayoendelea ikiwemo Tanzania na Zanzibar kwa ujumla, hivyo alilisitiza utamaduni wa kuendelea na kudumisha suala la kuiombea dua nchi na viongozi wake. “Tunawajibu wa kuendelea kumuomba Mwenyezi Mungu atuepushe na mabalaa mbalimbali, mabalaa ya vita na matatizo ya kimaumble, mabadiliko ya mazingira ikiwemo upepo mkali na mafuriko” aliomba Al hajj Dk. Mwinyi.
Akizungumzia maendeleo makubwa yaliyofikia na awamu ya nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Al hajj Dk. Mwinyi alieleza kuwa imeendelea kufanya mengi makubwa ikiwemo kufanikisha miradi mingi ya maendelo na kuimarisha miundombinu ya mawasiliano zikiwemo barabara za kisasa zenye viwango vya hali ya juu, ujenzi na uimarishwaji wa huduma za elimu, afya, miradi mingi ya maji kwa kujengwa skuli na hospitali za kisasa zenye hadhi za hali ya juu.
Pia, aliahidi kuendelea kupeleka miradi mikubwa ya maendeleo mkoani humo na maeneo mengine ya nchi. Akizungumza kwenye dua hiyo, Waziri Nchi Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman aliwasihi wananchi wa Zanzibar kuendelea kumuombea dua Al hajj Dk. Mwinyi kwa maendeleo makubwa anayoyafanya nchini.
Akitoa neno la shuqrani kwa niaba ya masheikh na wazee wa Makunduchi, Shekh Muadhini Jongo ameshukuru Al hajj Dk. Mwinyi kwa kuridhia kufika Makunduchi kujumuika nao kwenye dua hiyo pamoja na kuwashukuru Waislam wote walioshirikiana kuifanikisha.
Dua hiyo, pia ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini wakiongozwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheik Saleh Omar Kaab pamoja na viongozi wa Chama na Serikali.
Pia, Al hajj Dk. Mwinyi alizuru makaburi ya aliekua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Awamu ya nne, Marehemu Sheikh Iddrisa Abdul Wakili na Kaburi la Sheikh Hassan bin Ameir, aliekua mwanazuoni mkubwa Zanzibar.
🔰𝐀𝐒𝐀𝐍𝐓𝐄𝐍𝐈 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎!
01-06-2026
𝐒𝐇𝐔𝐋𝐄 𝐘𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐌𝐄𝐓𝐀 𝟏𝟐 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀𝐍𝐈 𝐇𝐀𝐈, 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
01-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
01-06-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
01-06-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
01-06-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
01-06-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
01-06-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
01-06-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
01-06-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
01-06-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
01-06-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
01-06-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
01-06-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
01-06-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
01-06-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
01-06-2026