Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025, imeweka Sera na Mikakati mbali mbali pamoja na kuchukua hatua za kuwawezesha watu wenye ulemavu kuweza kukamilisha malengo yao na kuweza kutoa mchango katika kuliendesha Taifa.
Ameyasema hayo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan katika kufunga Maadhimisho ya Miaka kumi na Tano (15)ya Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA) uliofanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip uwanja wa ndege Zanzibar.
Mhe. Rais Dkt Samia amesema kwa kutambua mchango mkubwa unaotolewa na watu wenye Ulemavu Serikali imeweza kutoa nafasi za uongozi kwa watu wenye ulemavu katika Wizara mbali mbali nchini ambapo wanaendelea kufanya vizuri katika majuku yao siku hadi siku.
Amesema kuwa Serikali imeanzisha Mabaraza ya Watu wenye Ulemavu kwa wilaya zote za Unguja na Pemba ambayo yanasaidi upatikanaji wa ujumuishwaji wa masuala ya watu wenye Ulemavu katika Taasisi zote za Umma na kuleta haki na fursa za watu wenye ulemavu nchini.
Aidha Serikali imeanzisha Mfumo wa Maendeleo ya watu wenye Ulemavu ambao katika mwaka wa fedha 2023-2024, Serikali imetenga Bajeti ya Shilingi milioni mia mbili(200, 000,000) kwa lengo la kuwanufaisha watu wenye Ulemavu kujiendeleza Kiuchumi.
Sambamba na hayo Rais Dkt Samia amesema Serikali inaendelea kutoa Mikopo kwa wajasiriamali na kwa kuweka kipaumbele kwa watu wenye Ulemavu kupitia fedha za ahueni ya UVIKO 19, fedha za mapato yatokanayo na Serikali pamoja na Mfuko wa Khalifa Foundation Fund kupitia wakala wa uwezeshaji wananchi kiuchumi Zanzibar.
Amefahamisha kuwa Serikali imejenga Skuli mbili (2) za Dahalia kwa watu wenye Ulemavu Unguja na Pemba kwa lengo la kuhakikisha watu wenye Uemavu wanaendelea kupata fursa sawa za elimu kama watu wengine sambamba na kutunga Sheria ya watu wenye Ulemavu Nam.(8) ya mwaka 2022 kwa lengo la kuwalinda na kutetea haki na fursa za watu wenye Ulemavu wakiwemo wanawake.
Dkt Samia amesema Serikali imekuwa ikiwawezesha watu wenye ulemavu kushiriki katika mashindano ya Kimataifa yaliyofanyika katika nchi mbali mbali Duniani sambamba na kushiriki katika Warsha iliyoshirikisha Mataifa Kumi na Tano(15) yenye lengo la kutoa Mafunzo na kutayarisha wataalamu wa Michezo Jumuishi itakayowajumuisha watu wenye ulemavu na wasio na ulemavu bila ya kuwa na Utengano wa aina yoyote.
Rais Dkt Samia ametoa wito kwa Taasisi za Serikali, Sekta binafsi na washirika wa Maendeleo kuiunga mkono JUWAUZA na Taasisi nyengine za watu wenye Ulemavu pamoja na kuitaka jamii kuendelea kutoa mashirikiano kwa watu wenye Ulemavu ili waweze kushiriki katika Ujenzi wa Taifa.
Mapema kaimu waziri wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais ambae pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera, Uratib na Baraza la Wawakilishi Mhe. Hamza Hassan Juma amesema JUWAUZA ni Taasisi ya kupigiwa mfano na kuigwa kwa namna wanavyoisaidia Serikali katika kupambania haki za wanawake na wasichanya wenye ulemavu Zanzibar kwa kuona kuwa wanathaminiwa na kupewa kipaumbele katika shuhli mbali mbali za Kimaendeleo.
Amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuthamini michango inaotolewa na Jumuiya ya JUWAUZA na kuahidi kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendela kushirikiana nao katika kufikia adhma na malengo ya jumuiya hio yanafikiwa.
Nae Mwenyekiti wa Bodi ya Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar Ndugu Abdulwakil Haji Hafidh amesema JUWAUZA Inasimamia haki za wanawake na wasichana wenye Ulemavu kwa kuwapatia elimu, ushirikishwaji katika mambo mbali mbali ya kijamii, kiuchumi na Kisiasa.
Amezishukuru serikali zote mbili kwa kuwaamini na kuwathamini wanawake kutoka jumuiya ya wanawake wenye ulemavu JUWAUZA kwa kuwapa nafasi mbali mbali za uongozi katika serikali pamoja na mihimili ya kutunga sheria nchini, na kufanya vizuri siku hadi siku katika kulilitea taima maendeleo.
Mwakilishi Mkaazi kutoka UN Bwana ZLATAN MILISIC amesema watu wenye uemavu hasa wanawake na watoto wanastahili kuthaminiwa na kuheshimiwa kwa kupatiwa haki zote stahiki sawa na wengine ili waweze kufanikisha malengo yao waliojiwekea.
Pia ameziomba serikali zote mbili kushirikiana na JUWAUZA kuhakikisha watu wenye Ulemavu hasa wanawake na wasichana wanapatiwa Elimu, Ujuzi, Nyenzo na maarifa kwa kuweza kufanya kazi katika Taasisi Mabali mabali, kushirikishwa katinga ngazi za maamuzi na katika kutunga Sera na Mipango ya Maendeleo ya Nchi.
Amesema wakati umefika wa Jamii, wazazi na walezi kuwakubali na kuwapa mashirikiano watu wenye Ulemavu, kuwashajihisha kwa kuwashirikisha katika shuhuli mbali mbali zinazofanyika katika jamii ili na wao wajione wana mchango katika jamii na Taifa sawa na wengine.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
02-04-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
02-04-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
02-04-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
02-04-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
02-04-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
02-04-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
02-04-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
02-04-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
02-04-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
02-04-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
02-04-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
02-04-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
02-04-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
02-04-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
02-04-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
02-04-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
02-04-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
02-04-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
02-04-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
02-04-2026