Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi amesema amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira Bora kwa Taasisi na Mashirika binafsi katika kuhakikisha wanatimiza majukumu yao ya utoaji wa huduma za msaada wa kisheria haapa -nchini.
Ameyasema hayo katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla katika kilele cha maadhimisho ya Tano(5) ya wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar yaliyofanyika katika Ukumbi wa asheikh aidrisa Abdul Wakil Kikwajuni Zanzibar.
Rais Dkt Mwinyi amesema Serikali kwa kushirikiana na Idara ya Katiba na Sheria itaendelea kutekeleza kampeni Kitaifa ya msaada wa Kisheria ya Mama Samia na Kampeni nyenginezo za Kitaifa na Kimataifa kwa lengo la kuwawezesha wananchi katika suala la upatikanaji wa haki zao.
Aidha Dkt Mwinyi amesema watoa huduma za msaada wa Kisheria wamekuwa wakombozi wakubwa kwa jamii katika masuala ya kisheria, kwa kutoa elimu ya kisheria na msaada wa kisheria kwa makundi mbali mbali wakiwemo vijana, wazee, watu wenye Ulemavu na wanafunzi ambapo wameweza kuwafikia wananchi laki nne kumi na tisa elfu mia nne na moja ( 419, 401) kati yao wanawake ni laki mbili ishirini na sita elfu mia moja na sabiini na mbili ( 226, 172) ni wanawake na laki moja tisiini na tatu mia mbili na ishirini na tisa (193, 229) ni wanaume.
Sambamba na hayo Rais Dkt Mwinyi amesema uwepo wa namba maalum itakayowasaidia wananchi katika upatikanaji wa huduma za Msaada wa Kisheria ni hatua muhimu inayohamasisha upatikanaji wa huduma hio na itakuwa kiungo kikubwa baina ya watoa huduma za Msaada wa Kisheria na wananchi ambao wengi wao mjini na vijijini wanamiliki vifaa vya kieletroniki ikiwemo simu za mkononi.
Rais Dkt Mwinyi ametoa wito kwa Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria pamoja na watoa huduma za Msaada wa Kisheria kuendelea kuelimisha wananchi juu ya uwepo wa namba hio maalum ya Huduma za Msaada wa Kisheria pamoja na upatikanaji wa huduma hizo kwa njia ya Teknolojia na kuwataka wananchi kuitumia vyema namba hio kwa utaratibu uliowekwa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Mhe. Haroun Ali Suleiman amesema watoa Msaada wa Kisheria wanafanya kazi kubwa ya kujitolea katika kutoa elimu ya Sheria na Msaada wa kisheria kwa wananchi hivyo ameiomba Serikali kuangalia ni kwa namna gani itawasaidia watoa huduma hao katika kuendelea kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
Waziri Haroon amesema ili kuendelea kuisaidia jamii katika kuwapatia elimu na kutoa Msaada wa Kisheria ni lazima kuwepo na mazingira mazuri ya kufanyia kazi, hivyo amewaomba Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuwapatia ofisi watoaji wa Msaada wa kisheria katika kila Wilaya ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa utulivu na kwa ufanisi mkubwa.
Kwa upande wao wawakilishi wa mashirika ya msaada wakisheria wakiwemo UNDP, LSF na UN WEMEN wamesema wataendela kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na wadau mbali mbali katika kupambana ili kuhakikisha upatikanaji wa haki kwa wahanga wa vitendo vya Ukatili na Udhalilishaji wa kijinsia hasa wanawake na watoto uanpatikana kwa wakati.
Wamesema kusaidia na kupambana kwa hali zote katika harakati mbali mbali za kimaendelo hasa katika kuhakikisha upatikanaji wa haki, haki za Binaadamu zinalindwa na kuhakikisha elimu ya Sheria inawafikia wananchi wote mijini na vijini.
Mapema Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Bi. Hanifa Ramadhan Said amesema Idara ya Katiba imeona ipo haja ya kuanzisha namba maalum ambayo itatumika katika kurahisisha upatikanaji wa Msaada wa kisheria na kuwa kiunganishi kikubwa kati wa Idara , watoa huduma za Msaada wa Kisheria na wananchi.
Mkurugenzi Hanifa amesema Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria itahakikisha inazidisha ushirikiano katika utendaji wa kazi baina yao na watoa huduma za Msaada wa Kisheria ili lengo halisi la upatikanaji wa haki, kutokomeza Ukatili na Unyanyasaji wa kijinsia kwa wananchi liweze kufikiwa .
Amezishukuru Taasisi na Mashirika mbali mbali ikiwemo L.S.F, UNDP, UN WOMEN Mahakama, Polisi na Chuo cha Mafunzo kwa ushirikiano wao mkubwa wanaoendelea kuwapatia ambao unarahisisha katika harakati zao za ufanyaji wa kazi za kila siku.
Nao watoaji Msaada wa kisheria Wameishukuru Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria kwa kuwapatia ushirikiano mkubwa unaowapelekea kufanya kazi zao za uweledi na ufanisi mkubwa sambamba na kuiomba serikali za mikoa na wilaya kuwapatia ofisi za kufanyia kazi zao ili kufikia malengo waliojiwekea
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
28-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
28-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
28-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
28-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
28-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
28-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
28-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
28-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
28-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
28-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
28-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-05-2026