Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR IMEAHIDI KUWAPATIA WAKULIMA PEMBEJEO NA HUDUMA NYENDINE ZA KILIMO ILI KUWAONDOSHEA CHANGAMOTO KUELEKEA MAPINDUZI YA KIJANI KWA UCHUMI ENDELEVU.

alternative

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameyasema hayo kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Nane Nane  kwa mwaka 2023, yanayoendelea Kizimbani, Wilaya ya Magharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi.

Alisema, Serikali inawajibu wa kuwawezesha vijana na wanawake kwenye shughuli zao za kilimo na kuitaka Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo kuandaa utaratibu mzuri wa kuweka takwimu zao kwa lengo la kuhakikisha inapotoa pembejeo ziwafikie wahusika kwa urahisi na kwa wakati muafaka.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi ameiagiza Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kuzitengeneza barabara zote zilizomo kwenye viwanja vya Maonesho ya Nane Nane Kizimbani, kwa kiwango cha lami ili kuyaongezea hadhi Maonesho ya mwakani.

Alisema, Serikali inawajibu wa kuhakikisha ardhi ndogo ya kilimo ilioyopo inatumika kwa ufanisi ili izalishe na kuongeza tija.

“Umefika wakati tuwe na takwimu sahihi ya ukubwa wa ardhi ya kilimo tuliyonayo ili tuweze kuweka mipango mizuri ya kuitumia” Alilisistiza Dk. Mwinyi.

Akizungumzia hali halisi ya uzalishaji kilimo nchini, Rais Dk. Mwinyi alieleza Serikali imeweka jitihada mbalimbali kufanikisha sekta hiyo na kueleza kuwa na matokeo yenye tija. Alieleza ongezeko la uzalishaji wa mboga mboga na matunda nchini kutoka tani 64,820 mwaka 2021 hadi tani 66,304 mwaka 2022, muhogo umeongezeka kutoka tani 181,668 mwaka 2021 hadi tani 202,519 mwaka 2022.

Kwa upande wa mifugo Rais Dk. Mwinyi alisema, ongezeko la ng’ombe waliochinjwa kutoka 25,916 mwaka 2021 hadi 27,326 mwaka 2022, kuku waliochinjwa wameongezeka kutoka 751,073 mwaka 2021 hadi 1,130,591 mwaka 2022 na mayai yaliyozalishwa yameongezeka kutoka 15,723,843 mwaka 2021 hadi 21,659,078 mwaka 2022.

Alisema, hizo ni dalili nzuri za mafanikio katika sekta ya Kilimo na Ufugaji kwa Zanzibar.

Alieleza lengo la Serikali kufanya Maonesho ya Kilimo ni kuhimiza kufanya mapinduzi ya kilimo kwa kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa mbinu bora za kilimo ikiwemo matumizi ya teknolojia ya umwagiliaji maji na zana za kisasa kwa madhumuni ya kuongeza uzalishaji kwa mazao ya chakula na biashara ili kupata tija zaidi na kuwapa faida kubwa wakulima na Taifa kwa jumla na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na washirika wa maendeleo ili kuendeleza sekta ya kilimo pamoja na kuhamasisha uwekezaji wa sekta binafsi

Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi aliwasihi vijana kutumia fursa ya Maonesho hayo kujifunza zaidi ili wahamasike na kujiajiri kwenye sekta ya kilimo kwa lengo la kuwa na uhakika wa chakula katika kupiga hatua za maendeleo yao na taifa kwa ujumla.

Akizungumza kwenye maonesho hayo, Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Shamata Shaame Khamis alisema, wizara inajitahidi kutekeleza kwa vitendo maelekezo ya Serikali katika kuimarisha sekta ya kilimo nchini kama ilivyoainishwa kwenye ibara ya 145 ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2020 – 2025.

Mapema akizungumza kwenye hafla hiyo, Katibu Mkuu Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Seif Shaaban Mwinyi aliwashauri vijana na wanawake kuzitumia fursa zinazopatikana kwenye Mradi wa mashamba makubwa ya pamoja (BBT) ulioanzishwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan ili kujiendeleza kiuchumi na kuyafikia mapinduzi ya kilimo. Uzinduzi wa Maonesho ya Nane Nane kwa mwaka 2023 ulikwenda sambamba uzinduzi wa Mkakati wa kilimo chini ya kaulimbiu isemayoVijana na wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula”

alternative alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi