RAIS DK. HUSSEIN ALI MWINYI AMESEMA AMEDHAMIRIA KUENDELEZA MAGEUZI MAKUBWA YA HUDUMA ZA JAMII NCHINI KUPITIA SEKTA MBALIMBALI.
Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye ziara ya kuutembelea mkoa wa Mjini Mgaharibi, kukagua na kuweka mawe ya msingi miradi mbalimbali ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa nyumba za maendeleo kwenye mji mpya wa Dk. Hussein Mwinyi, Mombasa viwanja vya magereza, unaosimamiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), ujenzi wa nyumba za makaazi Kwa mchina unazosimamiwa na Shirika la nyumba Zanzibar, Skuli ya Sekondari Mtopepo na Skuli ya Sekondari Mwembeladu, Wilaya ya Mjini.
Alisema, Serikali ya awamu nane imedhamiria kuendeleza ujenga wa skuli za maghorofa kutoka ngazi ya Chekechea, msingi hadi Sekodari, kuboresha mazingira bora ya walimu ikiwemo maslahi yao, kutoa ajira mpya za walimu, kuboresha mitaala ya elimu, kuongeza ufaulu mzuri pamoja na kuondosha zero kwa wanafunzi wa kidato cha nne na sita. Dk. Mwinyi pia alieleza hatua iliyofikiwa na Serikali sasa imepitiliza ahadi ya ilani ya CCM ya 2020 - 2025 ilipoahidi kujenda mabanda 1500 ya skuli za msingi na sekondani wakati hivi sasa kumejengwa Skuli za ghorofa 64 zenye miundombinu ya kisasa ikiwemo vyoo zaidi ya 50 kwa kila skuli, maktaba tatu tatu, maabara, vyumba vya kompyuta (ICT), ofisi bora za walimu na wakuu wa skuli, stoo, vyumba vya kusalia pamoja na ofisi za walinzi.
Akizungumzia makaazi ya kisasa, Rais Dk. Mwinyi amesema awamu ya nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imedhamiria kuongeza nyumba nyingi zaidi, za kisasa na za gharama nafuu ili kukidhi haja na uwezo wa wananchi wake wa matabaka yote, pamoja na kujenga miji ya kisasa yenye hadhi na wakati uliopo kwa kuboresha maisha bora wa wananchi. Alisema, ni wakati sasa wa kuondokana na makazi ya kiholela na kuzingatia makaazi na mipango bora ya miji kwa kuiagiza Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar kupima na kutoa maeneo yaliyopimwa. Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi alisema Serikali pia imepanga kutoa maeneo mengine zaidi ya ujenzi wa nyumba bora za maendeleo ikiwemo maeneo ya Kwamabata, Chumbuni na maeneo
mengine ya Zanzibar pamoja na kuondosha kodi za ongezeko la thamani kwa wananchi ili kuweka usawa wa watu wake na kumudu kumiliki nyumba hizo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye ziara hiyo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Muhamed Mussa, alisema azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni kuimarisha Sekta ya elimu nchini ambayo kwasasa imepiga hatua kubwa kuliko matarajio iliyojiwekea awali. Alisema, mafanikio ya elimu Zanzibar yanatokana na juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuimarisha mazingira wezeshi wa mfumo bora wa elimu Zanzibar, ushirikiano baina ya watendaji wa wizara, walimu wazazi, wanafunzi na wadau wa elimu nchini.
Naye, Waziri wa Ardhi na Maendelo, Rahma Kassim Ali, alisifu juhudi za Rais Dk. Mwinyi kwenye miradi ya maendeleo ikiwemo kuboreshwa kwa makazi bora ya nyumba za maenedeleo. Ziara ya Rais Dk. Mwinyi Mkoa wa Mjini Magharibi ni mwendelezo wa ziara zake za kukagua miradi ya maendeleo ikiwa ni shamrashamra za kusherekea mafaniko ya miaka mitatu ya uongozi wa awamu ya nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
26-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
26-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
26-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
26-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
26-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
26-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
26-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
26-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
26-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
26-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
26-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
26-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
26-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
26-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
26-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
26-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
26-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
26-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
26-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
26-05-2026