SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR IMELISHUKURU SHIRIKA LA MAENDELEO LAUMOJA WA MATAIFA (UNDP) KWA JITIHADA ZAKE ZA KUENDELEA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI KUPITIA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema UNDP limekua msaada mkubwa kwa SMZ hasa kwa kuendelea kushirikiana kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kuiongezea nguvu na kuiwezesha kifedha Taasisi ya Ufuatiliaji na Usimamizi Utendaji Kazi Serikalini (PDB), Zanzibar ili kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
Dk. Mwinyi amesema hayo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika hilo, nchini Shigeki Komatsubara aliefika kumtembelea. Alisema, SMZ na UNDP zimekua na ushirikiano wa karibu kwa miaka mingi na wamekua wakiungamkono Serikali kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.
Rais Dk. Mwinyi alimueleza mgeni wake huyo, Sera kuu ya Uchumi wa Zanzibar ni Uchumi wa Buluu, hivyo alimueleza kuangalia fursa zaidi za kuungamkono eneo hilo pamoja na Sekta ya Utalii. Dk. Mwinyi pia alilipongeza Shirika la UNDP kwa juhudi zake za kusaidia vyombo vya Sheria nchini ikiwemo Bunge kwa Tanzania Bara, Baraza la Wawakilishi na Mahakama kwa kuzijengea uwezo taasisi hizo.
Naye, Bw. Shigeki Komatsubara, alimuahidi Rais Dk. Mwinyi kwamba UNDP itaendeleza Ushirikiano kwa kuendelea kufanyakazi pamoja na SMZ kupitia Sekta ya Uchumi wa Buluu pamoja na kuendelea kuiungamkono PDB kupitia miradi mbalimbali ya Serikali.
Akizungumza baada ya hafla hiyo, Naibu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Ufuatiliaji na Usimamizi Utendaji Kazi Serikalini (PDB) Zanzibar, Dk. Josephine Rogate Kimaro alilishukuru Shirika la UNDP kwa ushirikiano mkubwa wanaoipatia PDB ikiwemo kuwajengea uwezo kwenye utendajikazi wao.
Alisema, UNDP limekua likiungamkono masuala mbalimbali ya maaendeleo ya taasisi hiyo hasa kwenye usimamizi na utekelezaji wa miradi ya kimkakati na kuweka mifumo ya utekeleza wa miradi ya vipaombele pamoja na kuisaidia taasisi hiyo kwenye ushajihishaji wa rasilimali zake.
Shirika la UNDP linatekeleza miradi sita barani Afrika, ikiwemo mitatu kwa Tanzania ambapo Zanzibar wanashirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutekeleza miradi ya kupambana na matukio ya Uhalifu Zanzibar kwa
kusirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka chini ya ufadhili wa Serikali ya Uingereza na Umoja wa Ulaya (EU).
Mradi mwengine unaotekelezwa na UNDP ni uwezeshaji kwenye masuala ya utawala wa kisheria ambapo mradi unaangazia juu ya haki na wajibu kwenye masuala ya jinsia ikiwemo masuala ya wanawake na watoto.
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
30-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
30-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
30-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
30-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
30-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
30-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
30-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
30-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
30-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
30-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
30-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
30-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
30-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
30-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
30-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
30-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
30-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
30-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
30-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
30-05-2026