Waumini wa Kiislamu wametakiwa kujipanga kwa kuendelea kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum na mayatima, wajane na watu wasiojiweza hasa katika mwezi mtukufu wa Ramadhan unaotarajiwa kuwafikia hivi karibuni.
Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla wakati akiwasalimia waumini wa Masjid NOOR kwa HAJI TUMBO mara baada ya kumaliza Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Amesema ni lazima wazanzibari na waumini wa dini ya kiislamu kuendeleza utamaduni wa kusaidiana pamoja na kuwasaidia watu wasio na uwezo ili kuweka usawa baina yao hasa katika mwezi mtukufu wa ramadhani mwezi ambao una fadhila nyingi sana ndani yake.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesisitiza kuwa mwezi wa Ramadhani umeshakaribia hivyo ni wajibu kwa waumini wa dini ya kiisalmu na wazanzibari kwa ujumla kuuendeleza yale yote ambayo waliokuwa wakiyafanya miezi yote kumi na moja (11) ambayo yanamfurahisha mwenyezimungu ikiwemo kutoa kile ambacho wameruzukiwa na Allah (S.W) kwa wanao hitaji ili kupata fadhila zake.
Alhajj Hemed amewataka waumini na Wazanzibari kuzidisha imani kwa viongozi wao ambao wanawaongoza na kuahidi kuwa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwaenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dkt. Hussein Ali Mwinyi itaendelea kutatua changamoto zote zinazowakabili wananchi wake.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed amewashukuru waumini na wazanzibari wote kwa ujumla kwa kuendelea kuishi kwa amani na utulivu jambo ambalo ndio dira ya maendeleo ya Taifa kwani kufanya hivyo ndio kunakopelekea Serikali kufanya yale yote iliyoyaahidi kwa wanachi wake kwa faida ya vizazi vya sasa na baadae.
Mapema akitoa Khutba katika Sala ya Ijumaa, Ustadh, TWAHIR ALI amewataka waumini wa Dini ya Kiislam kuamini kuwa kila anachokifanya mwanadamu atalitwa kulingana na matendo yake hivyo ni lazima kuzidisha Ibada hasa katika kipindi hichi Cha kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Ustadh Twahir amewasisitiza waumini kuwa na subra kwa kila jambo ambalo muumini linamtokea kwani kufanya hivyo ndio kufata nyayo za mitume wote ambalo walioletwa kuja kuitangaza dini ya mwenyezi mungu sambamba na kuyaacha yale yote ambayo yanamkirihisha Allah (S.W)
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
16-01-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
16-01-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
16-01-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
16-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
16-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
16-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
16-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
16-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
16-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
16-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
16-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
16-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
16-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
16-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
16-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
16-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
16-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
16-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
16-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
16-01-2026