BALOZI NCHIMBI ACHANGISHA SH. 950 MILIONI KWA MATIBABU YA WAGONJWA WA MGUU KIFUNDO
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amefanikisha uchangishaji wa shilingi milioni 950 kwa ajili ya matibabu ya watoto wapatao 400 wanaougua ugonjwa wa mguu kifundo.
Kiasi hicho cha fedha kimepatikana kupitia ahadi za wadau mbalimbali walioshiriki hafla ya futari maalum kwa harambee hiyo, iliyofanyika Machi 14, 2025, katika Ukumbi wa Super Dome, Dar es Salaam. Harambee hiyo ililenga kukusanya shilingi milioni 600 kwa ajili ya matibabu hayo.
Akifungua hafla hiyo kama mgeni rasmi, Balozi Nchimbi alisema tukio hilo ni sehemu ya kumuunga mkono Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameleta mafanikio makubwa katika sekta ya afya.
“Siku chache zilizopita, Rais Dkt. Samia alitangazwa mshindi wa tuzo ya kimataifa kwa juhudi zake za kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto, na kuwa Rais wa kwanza barani Afrika kupata nishani hiyo,” alisema Balozi Nchimbi.
“Shughuli yetu ya leo ni ishara ya kuunga mkono kazi kubwa anayoifanya kwa taifa letu, ambayo imetambuliwa kimataifa,” aliongeza.
Aidha, Balozi Nchimbi alifichua kuwa baada ya kumtaarifu Rais Dkt. Samia kuhusu harambee hiyo—iliyodhaminiwa na Taasisi ya GSM kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Klabu ya Yanga, na Hospitali ya CCBRT—Rais alielekeza CCM ichangie shilingi milioni 50 kwa ajili ya kusaidia matibabu hayo.
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
26-01-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
26-01-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
26-01-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
26-01-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
26-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
26-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
26-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
26-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
26-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
26-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
26-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
26-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
26-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
26-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
26-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
26-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
26-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
26-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
26-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
26-01-2026