MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR MHE HEMED SULEIMAN ABDULLA AMESEMA SERIKALI YA ZANZIBAR INAENDELEA KUWEKA MAZINGIRA BORA ILI KUEPUKANA NA MAGONJWA YA MIRIPUKO NA KUCHUKUA HATUA ZA MATIBABU PINDI MAGONJWA HAYO YATAKAPOJITOKEZA.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuweka mazingira bora ya kuweza kuepukana na magonjwa mbali mbali ya miripuko sambamba na kuchukua hatua za matibabu pindi magonjwa hayo yatakapojitokeza.
Ameyasema hayo katika Uzinduzi wa Kituo cha Mawasiliano ya Magonjwa ya Miripuko (Zanzibar Afya Call Center) katika Viwanja vya Magomeni - Sogea Zanzibar.
Mhe. Hemed amesema Sekta ya Afya Zanzibar imekuwa ikichukua hatua mbali mbali katika kuboresha upatikanaji na utowaji wa huduma bora pamoja na kudhibiti magonjwa ya miripuko ambayo yalikuwa na changamoto kubwa kutokana na kutokuwa na njia bora za mawasiliano kutoka kwa mwananchi kwenda katika Mifumo ya Afya ili kuweza kupatiwa suluhisho la chanamoto hio.
Amefahamisha kuwa Zanzibar ni miongoni mwa nchi zilizokumbwa na Janga la COVID 19 ambalo lilipoteza maisha ya watu wengi na kuathiri mifumo ya uchumi kutokana na ugumu uliokuwepo wa kusambaza taarifa kutoka kwa wananchi kwenda Serikalini juu ya ugonjwa huo.
Amesema kuwa uzinduzi wa kituo hicho cha mawasiliano kitakuwa ni muarubaini utakaorahisisha upatikanaji wa mawasiliano baina ya wananchi na watoa huduma za Afya pindi magonjwa ya miripuko na dharura yatakapojitokeza sambamba na kuwataka wananchi kukitumia kituo hicho kama kilivyokusudiwa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma bora na kwa wakati husika.
Aidha Mhe Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwepo kwa kituo hicho kitatoa faida nyingi kwa wananchi ikiwa ni pamoja na mgonjwa kuelekezwa sehemu sahihi ya kupata matibabu kulingana na ugonjwa wake kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Wizara ya Afya .
Sambamba na hayo amesema Kituo cha mawasiliano ya magonjwa ya miripuko kitawasaidia wananchi kufahamu juu ya Mfuko wa wa Huduma za Bima ya Afya Zanzibar ikiwemo namna ya kujiunga, masharti, faida na wanufaika wa amfuko huo pamoja na kuwaunganisha watalii na wageni mbali mbali ambao watapatiwa taarifa za huduma za Afya zinazopatikana hapa Zanzibar .
Mheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametoa wito kwa Uongozi wa Wizara ya Afya kuendelea kukitunza kituo hicho kwa kuhakikisha mambo ya msingi yanayohitajika katika kuleta ufanisi wa utowaji wa huduma bora yanapatikana, kuwepo kwa mafundi watakaotoa msaada wa marekebisho pindi watakapohitajika na kuwa na ulinzi wa uhakika kwa masaa ishirini na nne (24) ili kufikia malengo yaliyowekwa na serikali.
Nae Waziri wa Afya Mhe. Nassor Ahmed Mazrui amesema uendeshaji wa kituo hicho unahitaji fedha na nyenzo za kutosha ili kiweze kufanya kazi kwa ufanisi na uweledi wa kuweza kuwahudumia Wazanzibari na wageni wanaoingia nchini kwa wakati.
Mhe. Mazrui amewataka wahudumu wa kituo hicho kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu mkubwa, Ari na kasi zaidi ili kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya nane (8) inayoongozwa na Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kuwatumikia wazanzibar na kutoa huduma bora za afya kwa wote.
Kwa upande wake Mwakilishi kutoka UNICEF Bibi. AWETY ATIE amesema Shirika la UNICEF limekuwa likishirikiana kwa karibu ba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutekeleza miradi mbali mbali ya Maendeleo ikiwemo kukikarabati kituo cha Mawasiliano ya Magonjwa ya Mripuko ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi na kupambana na magonjwa ya mripoko yanatotokea nchini.
Amesema UNICEF itaendelea kutoa misaada na mashirikiano kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kukiendesha kituo hicho kwa muda wa miaka mitano (5) ambacho kitafanya kazi kwa Mfumo wa kidijitali pamoja na kutoa na kupokea taarifa mbali mbali zinazohusiana na masuala ya Afya.
Aidha Bibi. ATIE amewataka wananchi wa Zanziabar kukitumia kituo hicho pale wanapopatwa na dharura ama kutaka kupatiwa ufafanuzi na ufumbuzi juu ya masuala ya Afya kwa kupiga simu bure kwa namba 190 ama kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kupitia namba 30 ili kuweza kupatiwa ufumbuzi juu ya tatizo linalowakabili kwa wakati husika.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
28-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
28-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
28-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
28-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
28-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
28-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
28-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
28-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
28-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
28-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
28-03-2026