‘KAMCHAPE’ YAMSIKITISHA CHONGOLO KATAVI
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Chongolo amewataka Wananchi wa Mkoa wa Katavi kuachana na imani potofu za kishirikina, maarufu kwa jina la ‘kamchape’ kuwa zinafifisha juhudi za kupambana na umaskini ili kukuza maendeleo na ustawi wa watu.
Chongolo ameyasema hayo Jumatatu Oktoba 2, 2023 wakati akizungumza na wana CCM na wananchi katika eneo la Ofisi Kuu ya CCM Mkoa ww Katavi, Mpanda Mjini, baada ya kuwasili mkoani humo kuanza ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020 - 2025, kuhamasisha uhai wa Chama mkoani humo na kusikiliza kero za wananchi.
“Nimeambiwa huku kuna kamchape , hawa jamaa mnawapa nguvu kubwa, mnawapa kichwa, mnawapa fursa ya kufanya mambo yanayokiuka sheria za nchi.
“Imani hizo za kuamini ushirikina ni umasikini na ukitaka kujifunza angalia watu wanaoamini katika ushirikina uone maisha yao. Wanaamini katika ndoto ambazo kutekelezeka kwake ni ngumu.”
“Naombeni sana achaneni na kuendekeza mambo yanayoleta taaswira ya umasikini. Mkoa wa Katavi ni mkubwa na mmeshajenga historia kubwa’
Ndungu Chongolo amesema haiwezekani mpaka leo Mkoa wa Katavi kuendekeza ushirikina kama daraja la kufanikiwa katika mambo yao , hivyo ni lazima watoke katika kufikiri mambo kirahisi,” amesema Ndugu Chongolo.
Amesisitiza maendeleo hayapatikani kwa ndumba, kwa kupuliza, kwa kuagua , kupiga ramli na kutengeneza mambo rahisi bali maendeleo ni mambo yanayotaka kufuata utaratibu wa kanuni za maisha.
“Ukiona watu wa namna hiyo wewe usipate shida angalia maisha yao, mtu anaweza kuwa na ng’ombe 1000 lakini anakula nyama nusu kilo kwa wiki, sababu ya masharti.Achaneni na maisha hayo , afadhali uwe na ng’ombe 10 lakini uwe na uhuru wa kula nyama.
“Ni afadhali uwe na shamba heka tatu lakini uwe na uhuru wa kula mchele wako, achaneni na mila potofu , mila potofu zinawagombanisha , mila potofu zinawatenganisha.
“Mila potofu zinawatengenezea uadui usio na maana , zinawakwamisha kwenye shughuli za maendeleo.Akija mtu kapiga kamchape yake akawaambia ukilima shamba hili hutavuna mwaka huu, unaacha kwasababu unaamini alichosema,” amesema Chongolo.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025