NCHIMBI ATUA MWANZA NA MAAGIZO WIZARA YA UJENZI
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ameielekeza Wizara ya Ujenzi kuharakisha mchakato wa kumpata Mkandarasi mpya atakayejenga Barabara ya kutoka Sengerema hadi Nyehunge, jimboni Bushosa yenye urefu wa Kilometa 54.5, ili kazi ya ujenzi ianze mapema.
Aidha ameitaka Wizara hiyo, kuimarisha mchakato wa kukagua Wakandarasi ili wapatikane Wakandarasi wenye uwezo.
Balozi Dokta Nchimbi amesema hayo Agosti 13, 2024, alipokuwa akizungumza na wananchi wa Nyehunge Jimboni Buchosa wilayani Sengerema,mara baada ya kuwasili Jijini Mwanza kuanza ziara yake ya siku 2 mkoani humo.
Balozi Nchimbi ameelekeza mchakato ufanyike haraka ili Mkandarasi apatikane na kazi ianze ya ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha Lami.
Kuhusu kuimarisha uwezo wa kubaini Wakandarasi wenye uwezo, Balozi Dokta Nchimbi amesema hiyo itasaidia kwani wako Wakandarasi ambao wana historia ya kuharibu kila sehemu,na wanakimbilia Tanzania.
Amesema kamwe watu wasipewe kazi kwa majaribio.
Awali Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya amesema Mkandarasi huyo wa kituruki pia alipewa kazi Kyela mkoani Mbeya ambako ndiko alikoanza,lakini akaanza kusuasua.
Mhandisi Kasekenya amesema baada ya kuona Mkandarasi huyo anasuasua Kyela,Serikali ilifuatilia na ikaona uwezo wake ni mdogo.
Amesema kutokana na kubaini hilo,Serikali iliamua kusitisha Mkataba licha ya kwamba alikua ameshakabidhiwa hiyo Barabara.
Amesema Serikali ilitambua uwezo wa Mkandarasi huyo ni mdogo na amefafanua kwa sasa Serikali inakamilisha taratibu za kuvunja huo Mkataba ambao ni mkataba wa kimataifa.
Mhandisi Kasekenya amesema baada ya hapo,Serikali itatafuta Mkandarasi mwingine na kusema kama sheria itaruhusu, aliyekua wa pili apewe Kandarasi.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025