Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar , imeridhishwa na hatua nzuri ya ujenzi wa skuli za Sekondari za ghorofa ( G+3 ) zinazojengwa na Kampuni ya Simba Developers Ltd katika kijiji cha Bumbwini Makoba na Bumbwini Misufini Wilaya ya Kaskazini “ B” Unguja.
Akikagua maendeleo ya ujenzi wa skuli hizo pamoja na kumbi za Mitihani zinazojengwa katika skuli hizo, Mhe.Hemed amesema wakadarasi kutoka kampuni ya Simba Developers wanaendelea kuipatia heshima kampuni yao sambamba na kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya nane ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.
Amesema kuwa Serikali imekusudia kuondoa changamoto zote zinazowakabili wananchi wa mijini na vijijini ikiwemo chanagamoto ya msongamano wa wanfunzi madarasani na kuingia kwa mikondo miwili ya masomo hivyo ameitaka kampuni ya Simba Developers inayojenga Skuli hizo kuongeza kasi zaidi ili kuweze kumalizika kwa wakati ujenzi huo,
Aidha Mhe. Hemed ameitaka Wizara ya Elimu kukaa pamoja na viongozi wa Jimbo la Bumbwini kuangalia namna watakavyoifanyia ukarabati skuli ya Msingi ya Bumbwini Makoba na kuliangalia kwa umakini suala zima la ajira hasa katika kuajiri walimu wazawa ambao watasaidia kuondosha changamoto ya walimu kuchelewa kufika maskulini na kuzorotesha maendeleo katika Sekta ya Elimu.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais amesema Serikalini ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuzisimamia changamoto zote na kuzitafuta ufumbuzi na kuwaahidi wananchi wa Bumbwini waliotoa maeneo yao kupisha ujenzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo kuwa Serikali itahakikisha inawapatia stahiki zao kwa mujibu wa taratibu na sheria.
Aidha Mhe. Hemed amewataka Wananchi wa Bubwini na wazanzibari kwa ujumla kuendelea kumuunga mkono Rais Dkt Hussen Mwinyi pamoja na Serikali zote mbili katika jitihada wanazozifanya za kuwaletea maendeleo na kuwataka kukipa mashirikiano chama cha Mapinduzi ili kiendele kushikilia dola katika uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020-2025, Sambamba na kuwasisitiza kuendelea kuitunza na kuidumisha amani iliyopo nchini kwani hakuna Taifa lolote litakalopiga hatua za kimaendeleo bila ya kuwa na Amani, Umoja na mshikamano.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Ali Abdulghulam Hussein amesema Mipango ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar ni kuhakikisha ifikapo Januari 2025 wanafunzi wote wa Zanzibar wawe wanaingia skuli kwa mkondo mmoja wa asubuhi pamoja na kuondoa changamoto ya msongamano wa wanafunzi madarasani.
Aidha Mhe. Ghulam amesisitiza kuwa vifaa vyote kwa ajili ya skuli mpya zinazojengwa na zinazofanyiwa ukarabati vipo tayari na hakuna skuli itakayokosa vifaa vya kufundishia na kusomea kwa wanafunzi wote wa Zanzibar.
Mhe. Ghulam amesema Serikali imeongeza Bajeti ya Wizara ya Elimu na kufikia zaidi ya Bilioni 800 kwa mwaka wa fedha 2024-2025 fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kujengea skuli za ghorofa za kisasa, kuzifanyia ukarabati skuli ambazo ni chakavu na kujenga madarasa mapya kwa lengo la kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani.
Kwa upande wake mkandarasi anaenjenga skuli hizo pamoja na kumbi za Mitihani Simba Developers Ltd amesema wapo katika hatua za mwisho za ujenzi na kuahidi kuwa mwishoni mwa mwezi wa saba wanatarajia kuzikabidhi skuli hizo Serikalini ili wanafunzi waweze kuendeleo na masomo yao katika skuli hizo.
Kampuni ya Simba Developers wamemshukuru Rais Dkt Mwinyi kwa kuwaamini na kuwapatia nafasi ya kujenga miradi mbali mbali ya amendeleo hapa Zanzibar na kuahidi kuwa watahakikisha wanajenga kwa ubora na kwa viwango vinavyokubalika ili majengo hayo yaweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu pasipo na changamoto za aina yoyote za kiufundi.
Katika ziara hio Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar ametembelea ujenzi wa skuli ya Ghorofa ya Bumbwini Makoba, na Bumbwini Misufini na kumbi za Mikubtano . katika skuli hizo ,
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐓𝐇𝐈𝐁𝐈𝐓𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐇𝐔𝐃𝐔𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐘𝐀𝐌𝐀 𝐓𝐀𝐖𝐀𝐋𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
26-07-2026
𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐌𝐏𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
26-07-2026
🚆 𝐓𝐔𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐄 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
26-07-2026
ZIARA YA RAIS WA MISRI-TANZANIA
26-07-2026
🔰 CCM NA ACT-WAZALENDO WASAINI MARIDHIANO YA PAMOJA YA KISIASA ZANZIBAR
26-07-2026
🎉 𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀, 𝐃𝐊𝐓. 𝐀𝐒𝐇𝐀-𝐑𝐎𝐒𝐄 𝐌𝐈𝐆𝐈𝐑𝐎! 🔰
26-07-2026
🔰𝐍𝐀𝐈𝐁𝐔 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐁𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐇𝐀𝐋𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐔𝐑𝐈 𝐊𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐙𝐀
26-07-2026
🔰𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈𝐌𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝟐𝟎𝟐𝟔!
26-07-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
26-07-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
26-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
26-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
26-07-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
26-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
26-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
26-07-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
26-07-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
26-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
26-07-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
26-07-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
26-07-2026