BALOZI DK NCHIMBI: MFUMO WA ELIMU UTAWASAIDIA WATANZANIA KUSHINDANA KIMATAIFA
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, amesema mageuzi makubwa ya mfumo wa elimu ya Tanzania yanayofanywa na Serikali ya CCM chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan yataweka msingi imara wa mabadiliko yatakayowasaidia vijana wa Kitanzania kushindana duniani.
Balozi Nchimbi amesema msingi huo kupitia elimu, pia utawasaidia vijana wa Kitanzania kumudu changamoto za kuwa raia wa ulimwengu ambao unazidi kuunganishwa na kuwekwa karibu au kuwa kitu kimoja kupitia changamoto au fursa mbalimbali, kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kidiplomasia.
Katibu Mkuu Balozi Nchimbi amesema hayo alipowahutubia wanafunzi, wazazi na Jumuiya ya Shule ya Dar Es Salaam International Academy (DIA), alipokuwa mgeni rasmi wa mahafali ya wahitimu wa kidato cha sita wa shule hiyo, yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita, jijini Dar Es Salaam.
“Katika ulimwengu unaozidi kuunganishwa na masuala mbalimbali, ambapo tunakutana na jamii na tamaduni tofauti kila siku, elimu ni mojawapo ya nyenzo muhimu katika kutusaidia na kuwajengea msingi imara vijana wetu hasa wanapopambana kenye hii dhana ya raia wa kimataifa…ulimwengu umekuwa mahali padogo na kuzidi kutufanya sisi kuwa raia wa dunia katika nyanja tofauti tofauti. Tunapaswa kuwa sehemu ya washiriki washindani sio kujitenga.
“Chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, Tanzania inafanya mabadiliko makubwa ya mfumo wa elimu kuendana na mahitaji ya kimataifa, ili kuweka mkazo katika mahitaji ya nyakati za sasa na mbele zaidi ili vijana wetu washindane kimataifa. Maendeleo ya ulimwengu yametuonesha ukweli kuwa uraia wa nchi yoyote kwa sasa, hauwezi kuepuka kukamilishwa na uraia wa kimataifa, kwa maana ya kuelewa jinsi ulimwengu unavyofanya kazi, kuthamini utofauti, na kushirikiana kutafuta majawabu ya changamoto na kutumia fursa mbalimbali zilizopo kila mahali,” amesema Balozi Nchimbi.
Aidha, Balozi Nchimbi alisisitiza pamoja na Tanzania kuweka maandalizi ya msingi imara kwa ajili ya watu wake kuwa na uwezo wa kushindana kimataifa, kwa kupitia nyanja mbalimbali, pia imejidhatiti kuendelea kuenzi, kuthamini na kulinda mila, desturi na tamaduni ambazo zimekuwa tunu na utambulisho wa Tanzania na Watanzania katika majukwaa mbalimbali ya kimataifa, ikiwemo katika kushindania fursa mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya nchi na watu wake.
Mbali na mahafali ya wanafunzi wa kidato cha sita, Shule ya DIA pia mwaka huu inasherehekea miaka 20 tangu ilipoanzishwa kuwa mojawapo ya taasisi zinazotoa elimu nchini, ikiwa imejikita katika mtaala wa IB (International Baccalaureate).
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
16-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
16-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
16-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
16-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
16-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
16-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
16-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
16-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
16-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
16-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
16-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
16-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
16-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
16-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
16-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
16-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
16-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
16-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
16-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
16-11-2025