Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


VIKAO VYA CHAMA VIWE KAZI YA KUDUMU NA MSICHOKE - BALOZI DKT. NCHIMBI

alternative

> Awataka wanachama kuhamasishana kuhusu kujitokeza na kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa 

" Chama chochote cha siasa ni wanachama na vikao, endeleeni na utaratibu wa kuitisha na kuitikia miito ya vikao vya kujenga chama chetu, vikao viwe kazi ya kudumu na msichoke...tukikutana mara kwa mara tutatambua kero za wananchi tunaowaongoza na kujadili maendeleo na mafanikio yetu "

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa CCM Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi wakati akizungumza na Mabalozi wa mashina, viongozi wa serikali, Taasisi mbalimbali zisizo za kiserikali, viongozi wa dini, wazee na machifu Wilayani Mbeya Mjini.

Balozi Dkt. Nchimbi amewataka wananchama wote kuhamaishana katika kujiandaa za chaguzi za serikali za mitaa, Pia amekemea tabia ya viongozi kufanya majigambo na badala wachape kazi ambayo itawafanya kuzidi kupata sifa na kuaminika kwa wananchi na chama.

" Hamasishaneni kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa, tuendelee kushiriki kwenye chaguzi na kila mwanachama atambue kuwa ana haki ya kugombea lakini aende na moyo safu wa kutaka kuwatumikia wenzake, utambue uongozi si ubwana mkubwa bali ni utumishi hivyo unatakiwa kuheshimikankwa tabia, maadili na uoendo ili upendwe na wenzako na kuaminiwa na sio kuogopwa "

" Kiongozi huwezi kumkuta anafanya majigambo ya kijinga...ooh unajua mimi ndio mwenyekiti wa tawi hapa wengine nyie ni wajumbe tuu...huo sio uongozi na wengine utawajua tu wasivyojiamini ndio maana kuna wakati unnakuta kiongozi anaingia kwenye kikao anasema mimi ndio mwenyekiti hapa haya tuanze kikao wakati wajumbe wake wote wanatambua kama yeye ni mwenyekiti, huko ni kutokujiamini "

"... anayesambaza maneno kutoka sehemu moja kwenda nyingine tena ya uongo huyo hatufai katika chama chetu na serikali yetu ..."

🗓️17 Aprili, 2024
📍Jijini Mbeya

alternative alternative alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi