SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imeeleza Mpango wake wa kujenga Uwanja wa ndege wa Kimataifa kisiawani Pemba utakaoruhusu ndege kubwa kutua kisiwani humo moja kwa moja ili kikifunga kiswa hicho kwa Utalii.
Aidha, imetaja azma ya kuzifungua barabara kubwa zenye hadhi ya juu kutoka Wete hadi Chake na kutoka Chake hadi Mkoani mwishoni mwa mwaka huu ili kukikuza kisiwa Cha Pemba kibiashara na uwekezaji.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi aliyasema hayo Hotel “the mora” alipozindua jina jipya la hoteli hiyo kutoka la zamani la “Emarald” huko Matemwe, Mkoa wa Kasakazini Unguja.
Dk. Mwinyi amesema tayari Serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa Uwanja wa ndege wa Pemba ili ndege za kimataifa zitue kisiwani humo.
Akizungumzia maboresho makubwa ya uwanja wa Ndege wa Kimaifa wa Abeid Aman Karume Rais Dk. Mwinyi amesema mara baada ya kukamikila kwa hatua kubwa ya jengo namba 3 ambalo kwasasa linafanya vizuri kimataifa, Serikali pia inafanya matengenezo makubwa kwa “Terminal 1 & 2 na ujenzi mpya wa (terminal 4) ili kuboresha mazingira ya uwekezaji na Utalii nchini.
Pia, Rais Dk. Mwinyi ametaja faida za uwekezaji nchini, nakueleza kuwa umechangia asilimia kubwa ya maendeleo ya nchi kutokana na kodi wanazolipa wawekezaji kwa Serikali ambazo hutumiwa kuboresha huduma za jamii ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara na mawasiliano, ujenzi wa skuli mpya, hospitali, masoko, pamoja na kusambazwa kwa maji safi na Salama.
Rais Dk. Mwinyi pia, alieleza jinsi uwekezaji unavyofungua fursa nyingi kwa wazawa wakiwemo wakulima, wafugaji, wavuvi na wafanyabiashara kupata soko la uhakika la bidhaa zao kupitia mahoteli mbalimbali yaliopo nchini.
Alisema, Serikali huwalazimisha wawekezaji wa maeneo yote kuboresha huduma za jamii maeneo yote yaliyopitiwa na uwekezaji ikiwemo kujenga vituo vya afya, ujenzi wa vituo vya watoto yatima pamoja na mahitaji husika ya maeneo hayo.
Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi alimwagiza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi na Uwekezaji, Sharif Ali Sharif kuwasimamia wawekezaji wote kununua mahitaji yote yanayozalishwa nchini kabla ya kuagiza nchi ya nchi ili kutanua fursa kwa wajasiriamali wazawa na wafanyabiashara wa ndani.
Akizungumzia uwekezaji wa “Hotel the mora” Rais Dk. Mwinyi amesema imeekeza zaidi ya dola za Kimarekani milioni 600 pamoja na kutoa ajira 600 kwa wazawa na wenyeji nchini.
Akisifia uzuri na haiba ya kisiwa cha Zanzibar, Mkugenzi Mwendeshaji wa kampuni ya “Tui Group, wamiliki wa “Hotel the mora” Sebastian Abel amesema Zanzibar ni kisiwa chenye hadithi nyingi nzuri zenye kumvutia kila mgeni anaetembelea pia ni zawadi na sehemu salama ya uwekezaji na biashara ndio maana wamevutiwa na kuwekeza nchini.
Naye, Waziri Sharif aliwahakikishia ushirikiano wa hali ya juu wawekezaji wote waliopo nchini pia amesema maendeleo makubwa kwenye sekta ya uwekezaji ni juhudi za Rais Dk. Hussein Ali Mwinyi.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mkurugenzi Mamlaka ya kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) Saleh Saad Mohamed, amesema “Hoteli the mora” yenye hadhi ya nyota tano inamilikiwa na kampuni ya “Tui Group” ambayo tayari imewekeza nchi zaidi ya dola za kimarekani milioni 500 kwenye sekta ya Utalii kupitia hoteli zake za ‘RIU” iliopo Nungwi, “ TUI BLUE” ya Mangapwani na “the mora” ya Matemwe.
Alisema, kampuni ya “Tui Group” pia inatarajia kutambulisha jina lake jengine la “ Robinson” ambalo tayari ZIPA imelipatia chei cha uwekezaji wa mdadi mkubwa wenye thamani za dola za kimarekani milioni 50, kupitia kampuni ya “Blackstone Limited”
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini, Unguja Rashid Hadid amsema mkoa huo una hoteli 316 kati ya hizo 18 zina hadhi ya nyota tano kwa ujumla wake zinachangia asilimia 61 za pato la taifa kutoka kwenye sekta ya Utalii mkoani humo, aidha ameeleza juu ya mkoa wao unavyotumia utalii wa fukwe kukuza sekta hiyo kupitia Sera ya Uchumi wa Buluu.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
25-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
25-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
25-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
25-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
25-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
25-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
25-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
25-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
25-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
25-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
25-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
25-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
25-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
25-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
25-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
25-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
25-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
25-05-2026