Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano uliopo baina ya Zanzibar na Jamhuri ya watu wa China kwa maslahi mapana ya wananchi wa pande zote mbili .
Ameyasema hayo wakati alipofanya mazungumzo na Naibu Gavana wa Jimbo la ZHEJIANG Bwana. YANG QINGJIU na ujumbe wake waliofika ofisini kwake Vuga kumtembelea.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inathamini na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Jamuhuri ya watu wa China katika kuisaidia Zanzibar kupitia nyanja mbali mbali ikiwemo sekta ya Afya, Kilimo, Elimu na Habari pamoja na miradi mbali mbali ya kimkakati jambo lililopelekea kuimarika kwa huduma katika sekta hizo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameishukuru Serikali ya Jamuhuri ya watu wa china kwa kuendelea kuisaidia Zanzibar kupitia Nyanja mbali mbali ikiwemo kupokea madaktari Bingwa kutoka nchini China ambao husaidia kutoa huduma za tiba na ushauri kwa wagonjwa wanaofika katika hospitali mbali mbali ndani ya Visiwa vya Unguja na Pemba.
Aidha, Mhe. Hemed amemueleza kuwa kipaombele cha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni Uchumi wa Buluu ambao unajumuisha mambo mbali mbali ikiwemo Sekta ya Utalii ambayo imekuwa ikiichangia pato kubwa la Serikali kutokana na ongezeko la wageni wengi wanaoitembelea Zanzibar.
Sambamba na hayo, Mhe.Hemed ameikaribisha Serikali ya Jamuhuri ya watu wa China kupitia uongozi huo wa Jimbo la ZHEJIANG kuja kuekeza Zanzibar na kuzitumia fursa mbali mbali zilizopo nchini ikiwemo uchumi wa buluu.
Nae Naibu Gavana kutoka Jimbo la ZHEJIANG nchini China Bwana. YANG QINGJIU amesema wameamua kuja Zanzibar kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili hasa katika masuala ya maendeleo.
Bwana. YANG QINGJIU amesema China imekuwa ikishirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sekta ya uchumi, Utamaduni na elimu kwa kuwapatia wazanzibari ufadhili wa masomo ya muda mrefu na mafunzo ya muda mfupi hasa katika kada mbali mbali kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuwaongezea maarifa watumishi wa umma.
Amesema Jimbo la ZHEJIANG limepiga hatua kubwa sana katika masuala ya biashara hivyo kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wanawawekea mazingira mazuri kwa wafanyabiashara wa pande zote mbili.
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
21-01-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
21-01-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
21-01-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
21-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
21-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
21-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
21-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
21-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
21-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
21-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
21-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
21-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
21-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
21-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
21-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
21-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
21-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
21-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
21-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
21-01-2026