NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amewataka Wajumbe wa Sektetarieti za CCM ngazi za Matawi, Wadi na Jimbo la Kwahani kuendeleza utamaduni wa kufanya kazi za Chama na Jumuiya zake kwa ubunifu na uchapakazi katika majukumu yao ya kila siku.
Nasaha hizo amezitoa wakati akizungumza na wajumbe hao katika ziara yake ya kuimarisha uhai wa Chama Cha Mapinduzi katika Jimbo la Kwahani Unguja, alisema kila mtendaji na kiongozi wa CCM anatakiwa kutekeleza wajibu wake ili kuwa mfano bora na wa kuigwa kwa wanachama na makada wa Chama hicho.
Dkt.Dimwa, alieleza kuwa CCM itaendelea kusimamia wajibu wake wa kuwa daraja la kuwaunganisha wananchi na Serikali zake mbili ili jamii iwe na uelewa mzuri wa kufahamu utekelezaji mkubwa wa kazi za kimaendeleo unaofanywa na Serikali zilizopo madarakani.
Katika maelezo yake Dkt.Dimwa, alisema kasi kubwa ya maendeleo kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 unaofanyika nchini hivi sasa imekuwa ni tishio kwa Vyama vya upinzani na kupelekea kuanza kutoka nje ya mstari kwa kutoa tuhuma sisizokuwa za kweli kwa baadhi ya viongozi wa Serikali na Chama kwa ujumla.
“ Kasi yetu ni ile ile yenye viwango vya siasa za kisayansi mpaka mwaka 2025 hatusimami hadi tutakapohakikisha tunashinda uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Hivyo wito wangu kwenu tekelezeni majukumu yenu ipasavyo kwa mujibu wa miongozo na Katiba yetu ya mwaka 1977 toleo la Disemba 2022, msivunjwe moyo wala kuteteleka kwa mbwembwe na kelele za Wapinzani wanaona CCM imeshajibu hoja zao kwa vitendo na wanaanza kutafuta huruma ya kisiasa kwa kususia uchaguzi mara kudai Katiba mpya sisi tunasonga mbele.”, alieleza Dkt.Dimwa.
Pamoja na hayo alitoa wito kwa wanachama,viongozi na makada wa CCM wa Jimbo la Kwahani kujiandaa Kisaikolojia juu ya kuyafanyia kazi kwa vitendo maelekezo ya Chama na Jumuiya zake wakati yatakaposhushwa kwa ajili ya utekelezaji.
Aidha, aliwasihi wananchi bila kujali tofauti za kisiasa, kidini na kikabila kuendeleza utamaduni wa kulinda amani na utulivu wa nchi ili kupata fursa pana ya kutekeleza majukumu yao ya kujipatia kipato halali kwa wakati.
Kupitia ziara hiyo, aliwapongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Mwinyi, kwa utendaji wao mzuri ulioongeza ufanisi katika uimarishaji wa nyanja za kiuchumi, kijamii, kisiasa na kidiplomasia kwa ujumla.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
19-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
19-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
19-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
19-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
19-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
19-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
19-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
19-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
19-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
19-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
19-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
19-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
19-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
19-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
19-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
19-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
19-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
19-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
19-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
19-03-2026