SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema ina nia ya kulibadilisha eneo la Dimani kua la biashara la Kimataifa na kubadili taswira halisi ya eneo hilo kuwa la mvuto wa uwekezaji.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo alipofungua maonesho ya 10 ya biashara ya kimataifa, Dimani Wilaya ya Magaharbi B, Mkoa wa Mjini Maharibi, ikiwa ni mwendelezo wa shamrashamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Amesema Serikali imedhamiria kujenga majengo mengi ya kisasa ya biashara ya kimataifa kwa kuanza na eneo la Nyamanzi ambalo tayari kashakabidhiwa mfano wa ramani ya mji mpya wa biashara na uwekezaji wa eneo hilo na Waziri wa Biashara na Maendeleo ya viwanda wa Zanzibar.
Dk. Mwinyi alisema mpango huo utatoa fursa ya kukuza biashara na uwekezaji na kuitangaza Zanzibar kimataifa. Aidha, alieleza maonesho ya biashara ya kimataifa ya Dimani yana lengo la kukuza na kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini kuzitangaza na kuzitafutia masoko ya kimataifa. Sambamba na kutangaza fursa za biashara na uwekezaji kwenye nyanja za Kimataifa, kwa kuonesha biashara na bidhaa zinazozalishwa na wazawa wa ndani pamoja na kutoa upeo mkubwa duniani kuonesha bidhaa hizo nje ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
Rais Dk.Mwinyi pia alieleza, maonesho hayo ya Kimataifa yameboresha taswira mpya ya eneo la Dimani na kuliweka kwenye mvuto wa biashara. Dk. Mwinyi pia alizitaka taasisi za Umma na binafsi kulitumia eneo hilo la biashara kwa shughuli zao mbalimbali ili kuendelea kulitangaza kiuchumi ndani na nje ya nchi, pamoja na kuwataka wajasiriamali wadogo na wakubwa, wafanyabiashara na wadau wengine kuzalisha bidhaa zenye ubora ili kuendana sambamba na hadhi ya Kimataifa.
Vilevile Rais Dk. Mwinyi alitoa rai kwa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Zanzibar kuandaa mwongozo maalumu na mifumo wezeshi ya uendeshaji bora wa maonesho hayo kwa teknolojia ya hali ya juu. Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi aliahidi kuanzisha taasisi maalumu yenye taaluma na wataalamu watakaosimamia na kuendesha maonesho hayo kwa utaalamu wa hali ya juu ili kuweka ufanishi na lengo halisi la kuanzishwa kwa eneo la kudumu la maonesho hayo ya kimataifa.
Naye, Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Omar Said Shaaban alisema eneo hilo la biashara la Kimataifa ni fursa ya kukuza na kuendeleza biashara na uwekezaji nchini. Alitoa wito kwa taasisi za Serikali na binafsi kulitumia eneo la kumbi za mikutano
liliopo hapo kwa kazi zao na sherehe za aina mbalimbali ili kuendelea kulitangaza zaidi. Alisema kuwekwa maonesho hayo kwa kutumia mashamiana maalumu ni wazo lililotolewa na Rais Dk. Mwinyi, yametoa mchango mkubwa wa kuyafanikisha maonesho hayo.
Pia, Waziri Shaaban ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutoa eneo la kudumu la maonesho ya kimataifa ya biashara Zanzibar na kuongeza ni njia moja ya kuitangaza Zanzibar kibiashara katika nyanja za Kimataifa. Alisema, Wizara ina mpango wa kufanya mengi mazuri kwaajili ya usimamizi wa uwanja na matukio ya maonesho ya biashara viwanjani hapo ili kubadilisha eneo hilo la biashara kuwa la kijani kwa kupanda miti ya asili itakayopamba mandhari halisi ya viwanja hivyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Ali Khamis Juma alisema, ujenzi wa eneo hilo la biashara ulianza mwezi Mei mwaka jana na uligharimu shilingi bilioni 8.2 ambalo limejumuisha ujenzi wa miundombinu ya barabara zote za eneo hilo ikiwemo sehemu za maegesho ya magari, ujenzi wa miundombinu ya maji safi, umeme, mawasiliano, uwekaji wa vigae kuzuia athari za mvua na tope na mitaro ya maji machafu.
Aidha, alisema eneo hilo pia linajumuisha mashamiana 10 yenye ukubwa wa mita 50 na mawili yenye ukubwa wa mita 2500 ambayo yanatumika kwa ukumbi wa mikutano pamoja na mengine madogo 10 ambayo yametoa vibanda vya wafanyabiashara na wajasiriamali 4,010 sambamba na block za vyoo vyenye matundu 144 na viwanja vya kufurahishia watoto. Alisema bado ujenzi wa eneo hilo unaendelea kwa kukamilisha hatua nyengine ikiwemo ujenzi wa msikiti na ofisi za huduma nyengine.
Maonesho hayo ya kimataifa yenye kaulimbiu “Biashara mtandao kwa maendeleo ya biashara na uwekezaji” yamepewa jina la “Zanzibar Internationa Trade Fair” yanajumisha wafanyabiashara zaidi ya 4,000 kutoka ndani na nje ya Tanzania ikiwemo Zambia, Burundi, Misri na Uganda yanajumuisha wafanyabiashara wakubwa, wadogo, taasisi za umma na binafsi, kampuni mbalimbali pamoja na wajasiriamali.
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
31-05-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
31-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
31-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
31-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
31-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
31-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
31-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
31-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
31-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
31-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
31-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
31-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
31-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
31-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
31-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
31-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
31-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
31-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
31-05-2026