SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema ina nia ya kulibadilisha eneo la Dimani kua la biashara la Kimataifa na kubadili taswira halisi ya eneo hilo kuwa la mvuto wa uwekezaji.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo alipofungua maonesho ya 10 ya biashara ya kimataifa, Dimani Wilaya ya Magaharbi B, Mkoa wa Mjini Maharibi, ikiwa ni mwendelezo wa shamrashamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Amesema Serikali imedhamiria kujenga majengo mengi ya kisasa ya biashara ya kimataifa kwa kuanza na eneo la Nyamanzi ambalo tayari kashakabidhiwa mfano wa ramani ya mji mpya wa biashara na uwekezaji wa eneo hilo na Waziri wa Biashara na Maendeleo ya viwanda wa Zanzibar.
Dk. Mwinyi alisema mpango huo utatoa fursa ya kukuza biashara na uwekezaji na kuitangaza Zanzibar kimataifa. Aidha, alieleza maonesho ya biashara ya kimataifa ya Dimani yana lengo la kukuza na kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini kuzitangaza na kuzitafutia masoko ya kimataifa. Sambamba na kutangaza fursa za biashara na uwekezaji kwenye nyanja za Kimataifa, kwa kuonesha biashara na bidhaa zinazozalishwa na wazawa wa ndani pamoja na kutoa upeo mkubwa duniani kuonesha bidhaa hizo nje ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
Rais Dk.Mwinyi pia alieleza, maonesho hayo ya Kimataifa yameboresha taswira mpya ya eneo la Dimani na kuliweka kwenye mvuto wa biashara. Dk. Mwinyi pia alizitaka taasisi za Umma na binafsi kulitumia eneo hilo la biashara kwa shughuli zao mbalimbali ili kuendelea kulitangaza kiuchumi ndani na nje ya nchi, pamoja na kuwataka wajasiriamali wadogo na wakubwa, wafanyabiashara na wadau wengine kuzalisha bidhaa zenye ubora ili kuendana sambamba na hadhi ya Kimataifa.
Vilevile Rais Dk. Mwinyi alitoa rai kwa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Zanzibar kuandaa mwongozo maalumu na mifumo wezeshi ya uendeshaji bora wa maonesho hayo kwa teknolojia ya hali ya juu. Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi aliahidi kuanzisha taasisi maalumu yenye taaluma na wataalamu watakaosimamia na kuendesha maonesho hayo kwa utaalamu wa hali ya juu ili kuweka ufanishi na lengo halisi la kuanzishwa kwa eneo la kudumu la maonesho hayo ya kimataifa.
Naye, Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Omar Said Shaaban alisema eneo hilo la biashara la Kimataifa ni fursa ya kukuza na kuendeleza biashara na uwekezaji nchini. Alitoa wito kwa taasisi za Serikali na binafsi kulitumia eneo la kumbi za mikutano
liliopo hapo kwa kazi zao na sherehe za aina mbalimbali ili kuendelea kulitangaza zaidi. Alisema kuwekwa maonesho hayo kwa kutumia mashamiana maalumu ni wazo lililotolewa na Rais Dk. Mwinyi, yametoa mchango mkubwa wa kuyafanikisha maonesho hayo.
Pia, Waziri Shaaban ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutoa eneo la kudumu la maonesho ya kimataifa ya biashara Zanzibar na kuongeza ni njia moja ya kuitangaza Zanzibar kibiashara katika nyanja za Kimataifa. Alisema, Wizara ina mpango wa kufanya mengi mazuri kwaajili ya usimamizi wa uwanja na matukio ya maonesho ya biashara viwanjani hapo ili kubadilisha eneo hilo la biashara kuwa la kijani kwa kupanda miti ya asili itakayopamba mandhari halisi ya viwanja hivyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Ali Khamis Juma alisema, ujenzi wa eneo hilo la biashara ulianza mwezi Mei mwaka jana na uligharimu shilingi bilioni 8.2 ambalo limejumuisha ujenzi wa miundombinu ya barabara zote za eneo hilo ikiwemo sehemu za maegesho ya magari, ujenzi wa miundombinu ya maji safi, umeme, mawasiliano, uwekaji wa vigae kuzuia athari za mvua na tope na mitaro ya maji machafu.
Aidha, alisema eneo hilo pia linajumuisha mashamiana 10 yenye ukubwa wa mita 50 na mawili yenye ukubwa wa mita 2500 ambayo yanatumika kwa ukumbi wa mikutano pamoja na mengine madogo 10 ambayo yametoa vibanda vya wafanyabiashara na wajasiriamali 4,010 sambamba na block za vyoo vyenye matundu 144 na viwanja vya kufurahishia watoto. Alisema bado ujenzi wa eneo hilo unaendelea kwa kukamilisha hatua nyengine ikiwemo ujenzi wa msikiti na ofisi za huduma nyengine.
Maonesho hayo ya kimataifa yenye kaulimbiu “Biashara mtandao kwa maendeleo ya biashara na uwekezaji” yamepewa jina la “Zanzibar Internationa Trade Fair” yanajumisha wafanyabiashara zaidi ya 4,000 kutoka ndani na nje ya Tanzania ikiwemo Zambia, Burundi, Misri na Uganda yanajumuisha wafanyabiashara wakubwa, wadogo, taasisi za umma na binafsi, kampuni mbalimbali pamoja na wajasiriamali.
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
03-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
03-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
03-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
03-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆’-𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀
03-06-2026
𝐍𝐈 𝐍𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀!
03-06-2026
🔰𝐀𝐒𝐀𝐍𝐓𝐄𝐍𝐈 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎!
03-06-2026
𝐒𝐇𝐔𝐋𝐄 𝐘𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐌𝐄𝐓𝐀 𝟏𝟐 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈
03-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀𝐍𝐈 𝐇𝐀𝐈, 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
03-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
03-06-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
03-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
03-06-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
03-06-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
03-06-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
03-06-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
03-06-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
03-06-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
03-06-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
03-06-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
03-06-2026