RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amewaagiza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kuendeleza fursa za kuajiri walimu wengi zaidi wa fani zote ili kuondosha changamoto ya walimu Zanzibar.
Dk. Mwinyi ametoa agizo hilo wakati wa ufunguzi wa Skuli ya Msingi ya Hamid Ameir iliopo Donge Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa wa Kaskazini Unguja ikiwa ni shamrashamra za maadhimisho ya sherehe za kutimiza miaka 60 ya Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar.
Alisema, kada ya ualimu ni fani muhimu kuliko zote kwenye sekta za maendeleo, hivyo ameeleza azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuboresha mazingira bora ya Elimu kwa kuweka sawa mazingira wezeshi ya sekta hiyo pamoja na kuimarisha maslahi ya walimu.
Pia, Rais Dk. Mwinyi ameahidi kuongeza uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya elimu kwa kuipa kipaumbele bajeti ijayo ya sekta hiyo ili kuimarisha mazingira bora kutoka ngazi ya maandalizi, msingi hadi Sekondari na kuimarishwa vituo vya amali pamoja na kujenga dahalia za kisasa kabla ya mwaka 2025.
Vilevile, Rais Dk. Mwinyi alisema, nia ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kujenga ghorofa hadi skuli za maandalizi na dahalia ambayo inakwenda kutimia kama ilivyokamilisha skuli ya msingi ya Hamid Ameir kwa kuwa na madara mengi yaliyopindukia idadi, kuwa na wanafunzi chini ya idadi ya 45 pia inashuhudiwa kuwa skuli ya kwanza kuwa na mkondo mmoja tuu.
Alieleza hatua hiyo inatarajiwa kuzaa matunda bora ya matokeo mazuri kwenye kuongeza kasi ya ufaulu mzuri wa wanafunzi.
Rais Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo, kuwasihi wazazi na walezi kuzitumia skuli hizo kwa kuandikisha wanafunzi wengi zaidi pamoja na kuiasa jamii kuyatunza na kuyaenzi majengo hayo ili yadumu muda mrefu.
Akizungumzia miaka 60 ya Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi alisifu hatua za waasisi wa Muungano huo na wote waliojitolea kuutunza na kuuenzi na kueleza kuwa Muungano wa mfano Afrika uliodumu muda mrefu sana.
Naye, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Ali Abdul Gulam Hussein alisifu jitihada za Rais Dk. Mwinyi kwa uwekezaji mkubwa aliowekeza Wizara hiyo.
Alisema, Wizara hiyo tayari imekamilisha magorofa 20 ndani ya kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Dk. Mwinyi na kuahidi kumalizia ujenzi wa skuli za ghorofa kwa majimbo yote ya Unguja na Pemba kama ambavyo Wizara hiyo imekamilisha kwa baadhi ya majimbo zikiwemo skuli tano za Mkokotoni, Bumbwini, Tumbatu na Gamba zinazotarajiwa kukamilika mwezi wa tisa mwaka huu.
Aidha, alieleza Wizara ya Elimu na Mafuzo ya Amali tayari imeingiza makontena 60 ya vifaa vya skuli mpya zikiwemo meza, komputa, projekta, mashine za fotokopi, vitanda kwa dahalia zilizokamilika sambamba na kukamilisha ujenzi wa Dahali tatu kubwa kwa mkoa wa Kaskazini Unguja kwa maeneo ya Donge, Gambana Bumbwini.
Kwa upande wake Mwakilishi wa jimbo la Donge ambae pia ni Waziri wa Ujenzi na Mawasiliano, Dk. Khalid Salum Muhamed alimshukuru Rais Dk. Mwinyi kwa kufanikiwa kupeleka miradi mingi jimboni humo kiliwemo soko la kisasa Donge Mtambile, ujenzi wa Daraja kubwa Donge Chechele, kuboresha barabara za vijini pamoja na kuondosha msongamano mkubwa wa wanafunzi kwa ujenzi wa skuli za kisasa za Ghorofa.
Katibu mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Khamis Abdalla alisema ujenzi wa Skuli ya msingi ghorofa mbili ya Hamid Ameir uligharimu shilingi bilioni 4.5, umejumuisha madarasa 26, ofisi za walimu, ofisi ya mwalimu mkuu, vyoo, maktaba, maabara, chumba cha kompyuta na stoo.
Alisema, skuli hiyo ina wanafunzi 1173 kwa wastani wa wanafunzi 50, na sasa itakuwa na mkondo mmoja kwa wastani wa wanafunzi 41 kila darasa moja.
Akizungmza kwenye ghafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Rashid Hadid Rashid amepongeza juhudi za Rais Dk. Mwinyi kwa kuinua Sekta ya Elimu Zanzibar.
Alisema, Mkoa wa Kaskazini umebahatika majengo matano ya ghorofa ndani ya kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake, yakiwemo majengo ya ghorofa kwa Skuli za Misufini na Makoba kwa Bumbwini Wilaya ya Kaskazini A, Skuli ya Donge, Mkokotoni na Tumbatu kisiwani.
Pia, Hadid alipongeza jitihada za Dk. Mwinyi kusambaza vituo vya sayansi (Hubs) kwa mitaala ya sayansi kwa vituo vya Fukuchani, Mahonda, Kitope, Donge, Bumbwini na Tumbatu pamoja na ujenzi dahalia kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita na ujenzi wa dahalia ya ghorofa maeneo ya Gamba.
Akitoa salamu kutoka Chama Cha Mapinduzi, Katibu wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Idara ya Itikadi Uenezi na mafunzo Zanzibar, Khamis Mbeto Khamis alisema, Ilani ya Chama hicho ya 2020 – 2025 ndio mkataba baina ya Serikali na wananchi kwa kutekeleza had izote kwao.
Alisema ilani hiyo imezungumzia masuala ya elimu kutoka maandalizi hadi vyuo vikuu ambapo kwasasa imepitiliza malengo ya Ilani hiyo kwa kuongeza ufaulu na kujenga madarasa maradufu hasa kwa skuli za vipawa vya juu zikiwemo Lumumba kwa Unguja na Fidel kasro kwa Pemba.
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐓𝐇𝐈𝐁𝐈𝐓𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐇𝐔𝐃𝐔𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐘𝐀𝐌𝐀 𝐓𝐀𝐖𝐀𝐋𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
22-07-2026
𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐌𝐏𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
🚆 𝐓𝐔𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐄 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
ZIARA YA RAIS WA MISRI-TANZANIA
22-07-2026
🔰 CCM NA ACT-WAZALENDO WASAINI MARIDHIANO YA PAMOJA YA KISIASA ZANZIBAR
22-07-2026
🎉 𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀, 𝐃𝐊𝐓. 𝐀𝐒𝐇𝐀-𝐑𝐎𝐒𝐄 𝐌𝐈𝐆𝐈𝐑𝐎! 🔰
22-07-2026
🔰𝐍𝐀𝐈𝐁𝐔 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐁𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐇𝐀𝐋𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐔𝐑𝐈 𝐊𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐙𝐀
22-07-2026
🔰𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈𝐌𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝟐𝟎𝟐𝟔!
22-07-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
22-07-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
22-07-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
22-07-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
22-07-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026