Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


CCM TUNA JUKUMU LA KUHAKIKISHA KAZI ZA RAIS ZINAJULIKANA NA WANAOKWAMISHA WANACHUKULIWA HATUA - MWENEZI MAKONDA

alternative

Apokelewa Wilayani Rorya Mkoani Mara

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Paul Makonda amesema Chama Cha Mapinduzi kina jukumu la kuhakikisha kazi za Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, zinajulikana kila kona ya Nchi, Kuwashughulikia wanaokwamisha jitiahada za Serikali na kuwapa Imani Watanzania kuendelea kukiamini Chama.

Mwenezi Makonda amesema katika mkoa mmojawapo ambao wakisema wapo pamoja na wewe basi wanamaanisha ni pamoja na mkoa wa Mara ambapo ameeleza hata kipindi akigombea nafasi ya Uongozi watu wa Mara walimuhakikishia kumuunga mkono na hawakuyumba katika hilo.

Pia, Mwenezi Makonda amesema "Watoa taarifa ni kuwakimbia sababu kila siku wana matatizo, hawana sera wala mipango maana yake hawana dira, mfano sisi CCM sera yetu ya Elimu ni kutoa Elimu bure sasa waulizeni wao sera yao ya Elimu ni ipi? Wakisema kuna mchango shule fulani basi Sisi tunatuma watu watafuatilia na tutatatua changamoto hiyo kwahiyo ni Watoa taarifa tuu ambapo wakati mwingine si za kweli hivyo msiwaamini"

Aidha, Wananchi wa Rorya wamemzawadia Mwenezi Makonda zawadi ya Ngo'mbe.

alternative alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi