Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar Alhaj Dkt.Mohamed Said Dimwa,amewasihi waumini wa dini mbalimbali nchini kufuata falsafa na maoni ya aliyekuwa Rais wa awamu ya pili ya jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja na Rais wa awamu ya tatu ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Marehemu Ali Hassan Mwinyi.
Wito huo ameutoa wakati akizungumza katika hitma ya kumuombea marehemu Mzee Mwinyi iliyofanyika katika msikiti wa Donge Pangamaua Jimbo la Donge,amesema kiongozi huyo enzi za uhai wake amekuwa ni mfano wa kuigwa katika maisha yake ya uongozi na baada ya kustaafu kwa kuishi katika misingi ya maadili,uadilifu na ucha Mungu.
Alhaj Dkt.Dimwa,alisema Mzee Mwinyi atabaki katika kumbukumbu na historia ya kipekee katika kulinda,kutetea na kuendeleza misingi ya uongozi bora wenye kufuata matakwa ya kidemokrasia kwa wananchi na alipinga tabia za ubaguzi wa kidini,kikabila na kisiasa.
“Zawadi kubwa ya kumpatia Mzee wetu huko aliko ni kumuombea dua kwa wingi ili Mwenyezi Mungu amjaalie mema,nasi tuendeleze pale alipotuachia kwa kuhakikisha tunaishi katika misingi ya maadili mema ya ushirikiano,upendo na kudumisha amani na utulivu”, alisema Dkt.Dimwa.
Aliwasihi waumini hao na wananchi kwa ujumla kuwarithisha watoto wao misingi ya maadili mema katika malezi yao ya kila siku ili kupata viongozi bora wa sasa na baadae.
Katika maelezo yake Naibu Katibu Mkuu huyo Dkt.Dimwa,alieleza kuwa kila mwananchi ana jambo la kujifunza juu ya maisha ya Mzee Mwinyi harakati za kiungozi,kidini,kitamaduni na kisiasa.
Kupitia hitma hiyo Dkt.Dimwa,alitoa salamu za Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi kuwa anawashukru wananchi wa Jimbo la Donge na majimbo jirani wanaofanya hitma na dua mbalimbali za kumuombea kiongozi huyo Mzee Ali Mwinyi aliyeongoza Serikali zote mbili ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar kwa ujumla.
Katika hitma hiyo iliyoandaliwa na Jimbo la Donge iliudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mwakilishi wa Jimbo hilo Dkt.Khalid Salum Mohamed,Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Rashid Hadid pamoja na Madiwani na wananchi wa jimbo hilo.
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
03-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
03-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
03-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
03-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
03-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
03-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
03-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
03-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
03-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
03-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
03-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
03-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
03-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
03-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
03-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
03-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
03-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
03-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
03-03-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
03-03-2026