Serikali yaja na Helikopta kukabiliana na Majanga ya Moto
Serikali yaja na Helikopta kukabiliana na Majanga ya Moto
Serikali imedhamiria kufanya maboresho makubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ikiwa ni juhudi za kupambana na athari za majanga pindi zitokeapo ajali mbalimbali ikiwemo ajali ya moto ili kuweza kuokoa mali na maisha.Maboresho hayo yanajumuisha ununuzi wa magari ya kuzimia moto yasiyopungua 150,magari 20 ya Kubebea Wagonjwa, Boti za Kisasa 25 za Uokozi na Helikopta Moja Maalumu ya Uokozi.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhandisi Hamad Masauni wakati akizungumza katika Mkutano wa Kuwajengea uwezo Wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara na Makatibu Tawala, ulioandaliwa na Ofisi ya Rais Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI), katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha mkoani Pwani ambapo pia ulihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi, Daniel Chongolo.
“Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii, Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inakwenda kufanya uwekezaji mkubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambapo tutashuhudia magari ya Zimamoto na Uokoaji yasiyopungua 150 yakimwagika, Boti Maalumu za Uokozi zisizopungua 25, Gari Maalumu za Kubebea majeruhi (Ambulance) zisizopungua 20, na Helikopta, lengo ikiwa kuokoa mali na Maisha ya Watanzania pindi yanapotokea majanga” alisema Mhandisi Masauni
Waziri Masauni amewaomba pia Wakuu wa Mikoa kuhakikisha kunakuwepo vituo vya kuchotea maji ambayo yatatumika pindi yatokeapo majanga ya moto huku akitaja maeneo mengine ya vipaumbele kwa Jeshi la Zimamoto kuwa ni kuimarisha vitendea kazi vya Zimamoto na Uokoaji, Ujenzi wa Vituo vya Zimamoto pamoja na Nyumba za Makazi ya Askari wa Jeshi hilo na kuwasiliana na Mamlaka za Maji katika mikoa mbalimbali nchini ili kuweza kusimika mabomba ya kuzimia moto(fire hydrants) huku pia serikali ikitenga kiasi cha shilingi milioni 120 kwa ajili ya ukarabati wa vituo vibovu.
“Serikali imeendelea na Ujenzi wa Vituo vya Zimamoto na Uokoaji katika maeneo mbalimbali nchini lengo ikiwa ni kuboresha huduma za uokoaji katika maeneo hayo na katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 jumla ya Shilingi Bilioni 2 zimetengwa kwa ajili ya Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Saba vya Zimamoto na Uokoaji katika mikoa ya Songwe, Simiyu, Manyara, Kagera, Katavi, Geita na Njombe, vilevile Shilingi Milioni 400 zimetengwa kwa ajili ya Ukarabati wa Nyumba 10 za Makazi ya Askari katika mikoa ya Arusha, Morogoro na Iringa”
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
02-02-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
02-02-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
02-02-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
02-02-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
02-02-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
02-02-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
02-02-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
02-02-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
02-02-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
02-02-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
02-02-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
02-02-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
02-02-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
02-02-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
02-02-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
02-02-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
02-02-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
02-02-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
02-02-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
02-02-2026