KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis,amesema Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuwasimamia Viongozi wa Majimbo hasa Wabunge na Wawakilishi watekeleze kwa ufanisi ahadi walizotoa kwa Wananchi kupitia Uchaguzi Mkuu uliopita.
Hayo ameyasema wakati akikabidhi vitendea kazi vikiwemo mitungi ya Gesi na Pikipiki kwa Viongozi wa jimbo la Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo hilo Mhe.Profesa Makame Mbarawa Mnyaa.
Amesema CCM ipo kwa ajili ya kusimamia maslahi na haki za wananchi kwa kuhakikisha kila kiongozi aliyepewa dhamana ya kuwawakilisha Wananchi katika Vyombo vya maamuzi anatekeleza wajibu wake kwa wananchi.
Katika maelezo yake Mbeto,amefafanua kuwa CCM katika Uchaguzi Mkuu ujao CCM itatoa kipaumbele kwa Viongozi wanaofanya kazi kwa ufanisi na waliokuwa karibu na Wananchi wao.
"Nakupongeza sana Prof.Mbarawa umefanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani ya CCM kwani changamoto kubwa iliyokuwa ikiwakabili Viongozi na Watendaji wengi wa ngazi za Matawi hadi Majimbo ni ukosefu wa usafiri wa kutoka eneo moja kwenda jingine,lakini kwa busara zako leo umewapatia Pikipiki na akina mama kuwapa Gesi salama kwa ajili ya ulinzi wa miundombinu ya mazingira", alisema Mbeto.
Kupitia hafla hiyo ya makabidhiano ya vifaa hivyo Mbeto,aliwataka Viongozi na Wanachama kuhamasisha wananchi kujiunga na CCM kwa wingi.
Akizungumzia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 amesema tayari imetekelezwa kwa zaidi ya asilimia 98 kwa kipindi cha miaka mitatu ya Uongozi wa Rais Dk.Mwinyi.
Pamoja na hayo Mbeto,alimpongeza Mbunge huyo Prof.Mbarawa kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwaletea wananchi maendeleo katika sekta za maji safi na salama,miundombinu ya usafiri,afya,elimu na vikundi vya ujasiriamali na kwamba viongozi wengine waige mfano huo katika kuharakisha maendeleo endelevu ya majimbo.
Naye Mbunge wa Jimbo la Mkoani,Prof.Makame Mbarawa,Amewapongeza wanachama wa CCM kwa kazi kubwa wanayofanya ya kukitumikia Chama kwa kujitoleo.
Alisema leongo la kutoa mitungi ya Gesi ni kuunga mkono kampeni ya mazingira za kuhamasisha matumizi salama ya Gesi majumbani badala ya kuni na mkaa.
Aidha,amesema dhamira ya kutoa Pikipiki kwa Watendaji mbali mbali wa Chama ndani ya Mkoa huo ni kuwarahisishia huduma za usafiri wakati wa utekelezaji wa Majukumu yao ya kila siku.
Katika hafla hiyo Mbunge huyo wa Jimbo la Mikoani ametoa Pikipiki 20 zenye thamani ya shilingi milioni 64 pamoja na mitungi ya Gesi 200 kwa ajili ya Wananchi wa Jimbo hilo.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025