Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa wito kwa nchi wanachama za Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa bara la Afrika, SADC, kuona haja za kuziimarisha taasisi zao zinazosimamia utawala bora zikiwemo Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
Pia, Rais Dk. Mwinyi alizishauri taasisi hizo kuona umuhimu wa kufanya ziara za kimafunzo na kujengeana uwezo kwa kujifunza mbinu bora za kisasa kwenye utekelezaji wa majukumu yao, sambamba na kuendelea kutoa mafunzo zaidi.
Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip, Uwanja wandege Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magaharibi, alipofungua Mkutano wa Mafunzo kwa Wajumbe na Wataalamu wa Kamati za SADCOPAC katika kupambana na rushwa, kuhamasisha uwazi na uwajibikaji kwa usimamizi wa mali zisizo rejesheka kwa kamati hizo.
Alisema, Mkutano huo kwa Zanzibar ni fursa nzuri kwa Wataalamu wa ndani pamoja na Mabunge ya nchi wanachama wa SADC kubadilishana uzoefu na kujifunza mbinu za kukabiliana na rushwa, kuongeza uwazi na uwajibikaji kutoka nchi nyengine za mataifa ya Afrika hasa ukanda wa Kusini mwa Afrika.
Pia alieleza Mafunzo hayo kufanyika Zanzibar ni fursa ya kuitangaza Tanzania na kuwawezesha wageni kupata nafasi adhimu ya kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii, zikiwemo fukwe nzuri na Mji Mkongwe wa Zanzibar wenye hadhi ya urithi wa Dunia.
Akizungumzia suala la mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa, kuwepo kwa uwazi katika matumizi ya rasilimali za umma na kuhimiza uwajibikaji kwenye utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika kukuza uchumi wa mataifa ya Afrika na kuimarisha huduma za jamii, Rais Dk. Mwinyi alisema ni mambo ya misingi na yenye mchango muhimu kwa kuchochea kasi ya maendeleo ya mataifa hayo.
Alisema, rasilimali zilizomo Afrika ni vyanzo muhimu vya kukuza uchumi wa mataifa yao, ikiwa vitasimamiwa vyema na kutumika kwa misingi ya sheria, uwazi na uwajibikaji. Alisistiza kuwa taasisi za utawala bora zikiwemo Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Mamlaka za kuzuwia Rushwa na Uhujumu Uchumi na Mabunge kwa nchi wanachama wa SADC yana mchango mkubwa wa kuyafikia matarajio ya mataifa yao.
Alisema, Serikali zote mbili za SMZ na SMZ zimejitahidi kuchukua hatua mbalimbali ili kukabiliana na vitendo vya rushwa na kuhimiza uwazi na uwajibikaji ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 – 2025 pamoja na mipango mingine ya maendeleo.
Akitaja hatua hizo Rais Dk. Mwinyi alieleza ni pamoja na kuzijengea uwezo taasisi zake kwa mafunzo ili kuzipatia weledi, kuzipatia vifaa vya kufanyia kazi na kuzijengea miundombinu bora ili zifanye kazi zao kwa ufanisi zaidi.
Kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi alisema, inaendelea kupambana na rushwa, kuhimiza uwajibikaji na uwazi kwa kuanzisha mifumo mbalimbali ya huduma zikiwemo za kifedha.
Aliongeza, kuanzisha utaratibu wa kusomwa kwa taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali hadharani kwa kujadiliwa kwa kina na uwazi kwenye Baraza la Wawakilishi.
Alieleza, hatua hiyo imeimarisha Mamlaka ya Kupambana na Rushwa na Uhujumu Uchumi na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka zimesaidia sana kufikia malengo ya nchi kwa kuimarisha utawala bora.
Akiizungumzia sheria ya Ukaguzi wa Mapato na Matumizi ya Umma nambari 7 ya mwaka 2023 ya Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi alieleza imeleta mafanikio makubwa kwenye kujenga uwelewa kwa wananchi juu ya matumizi ya fedha za Umma.
Kuhusu mafanikio hayo Rais Dk. Mwinyi alieleza ni pamoja na kutumia mifumo, kuokoa fedha za Serikali kwa asilimia 86.3, kutekeleza miradi ya maendeleo kwa uwazi kwa asilimia 96, kuongezeka kwa uelewa wa usimamizi wa fedha za umma (mapato na matumizi) kwa asilimia 96, Matumizi ya mifumo kwenye shughuli za Serikali pia yameongezeka kutoka asilimia 48 na kufikia 92.4
Mafanikio mengine yaliyopatikana kutokana na kuimarika kwa utendaji huo Rais Dk. Mwinyi alieleza Serikali ya Zanzibar kupitia Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali kupewa kazi ya kusimamia na kufuatilia matumizi ya miradi ya maendeleo kupitia USAID na ADB ambapo awali kazi hio ilifanywa na taasisi binafsi.
Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi alisema, Zanzibar inajitahidi kutekeleza kwa ukamilifu makubaliano yaliyofikiwa baina ya nchi wanachama wa kamati za SADCOPAC.
“Siku siku zote tutajitahidi kuwa kinara katika utekelezaji ili malengo na mipango yetu iweze kufanikiwa kama sote tunavyotarajia” alibainisha Rais Dk. Mwinyi.Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi alizitaka kamati za Mabunge ya nchi wanachama wa SADC, kuendelea kudumisha ushirikiano na Tanzania hasa Zanzibar.
Mafunzo hayo yaliandaliwa na Wizara zinazosimamia sheria na utawala bora Tanzania, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Zanzibar pamoja na Uongozi na Sekretarieti ya SADCOPAC.
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐓𝐇𝐈𝐁𝐈𝐓𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐇𝐔𝐃𝐔𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐘𝐀𝐌𝐀 𝐓𝐀𝐖𝐀𝐋𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
22-07-2026
𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐌𝐏𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
🚆 𝐓𝐔𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐄 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
ZIARA YA RAIS WA MISRI-TANZANIA
22-07-2026
🔰 CCM NA ACT-WAZALENDO WASAINI MARIDHIANO YA PAMOJA YA KISIASA ZANZIBAR
22-07-2026
🎉 𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀, 𝐃𝐊𝐓. 𝐀𝐒𝐇𝐀-𝐑𝐎𝐒𝐄 𝐌𝐈𝐆𝐈𝐑𝐎! 🔰
22-07-2026
🔰𝐍𝐀𝐈𝐁𝐔 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐁𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐇𝐀𝐋𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐔𝐑𝐈 𝐊𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐙𝐀
22-07-2026
🔰𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈𝐌𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝟐𝟎𝟐𝟔!
22-07-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
22-07-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
22-07-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
22-07-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
22-07-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026