Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa wito kwa nchi wanachama za Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa bara la Afrika, SADC, kuona haja za kuziimarisha taasisi zao zinazosimamia utawala bora zikiwemo Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
Pia, Rais Dk. Mwinyi alizishauri taasisi hizo kuona umuhimu wa kufanya ziara za kimafunzo na kujengeana uwezo kwa kujifunza mbinu bora za kisasa kwenye utekelezaji wa majukumu yao, sambamba na kuendelea kutoa mafunzo zaidi.
Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip, Uwanja wandege Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magaharibi, alipofungua Mkutano wa Mafunzo kwa Wajumbe na Wataalamu wa Kamati za SADCOPAC katika kupambana na rushwa, kuhamasisha uwazi na uwajibikaji kwa usimamizi wa mali zisizo rejesheka kwa kamati hizo.
Alisema, Mkutano huo kwa Zanzibar ni fursa nzuri kwa Wataalamu wa ndani pamoja na Mabunge ya nchi wanachama wa SADC kubadilishana uzoefu na kujifunza mbinu za kukabiliana na rushwa, kuongeza uwazi na uwajibikaji kutoka nchi nyengine za mataifa ya Afrika hasa ukanda wa Kusini mwa Afrika.
Pia alieleza Mafunzo hayo kufanyika Zanzibar ni fursa ya kuitangaza Tanzania na kuwawezesha wageni kupata nafasi adhimu ya kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii, zikiwemo fukwe nzuri na Mji Mkongwe wa Zanzibar wenye hadhi ya urithi wa Dunia.
Akizungumzia suala la mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa, kuwepo kwa uwazi katika matumizi ya rasilimali za umma na kuhimiza uwajibikaji kwenye utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika kukuza uchumi wa mataifa ya Afrika na kuimarisha huduma za jamii, Rais Dk. Mwinyi alisema ni mambo ya misingi na yenye mchango muhimu kwa kuchochea kasi ya maendeleo ya mataifa hayo.
Alisema, rasilimali zilizomo Afrika ni vyanzo muhimu vya kukuza uchumi wa mataifa yao, ikiwa vitasimamiwa vyema na kutumika kwa misingi ya sheria, uwazi na uwajibikaji. Alisistiza kuwa taasisi za utawala bora zikiwemo Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Mamlaka za kuzuwia Rushwa na Uhujumu Uchumi na Mabunge kwa nchi wanachama wa SADC yana mchango mkubwa wa kuyafikia matarajio ya mataifa yao.
Alisema, Serikali zote mbili za SMZ na SMZ zimejitahidi kuchukua hatua mbalimbali ili kukabiliana na vitendo vya rushwa na kuhimiza uwazi na uwajibikaji ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 – 2025 pamoja na mipango mingine ya maendeleo.
Akitaja hatua hizo Rais Dk. Mwinyi alieleza ni pamoja na kuzijengea uwezo taasisi zake kwa mafunzo ili kuzipatia weledi, kuzipatia vifaa vya kufanyia kazi na kuzijengea miundombinu bora ili zifanye kazi zao kwa ufanisi zaidi.
Kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi alisema, inaendelea kupambana na rushwa, kuhimiza uwajibikaji na uwazi kwa kuanzisha mifumo mbalimbali ya huduma zikiwemo za kifedha.
Aliongeza, kuanzisha utaratibu wa kusomwa kwa taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali hadharani kwa kujadiliwa kwa kina na uwazi kwenye Baraza la Wawakilishi.
Alieleza, hatua hiyo imeimarisha Mamlaka ya Kupambana na Rushwa na Uhujumu Uchumi na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka zimesaidia sana kufikia malengo ya nchi kwa kuimarisha utawala bora.
Akiizungumzia sheria ya Ukaguzi wa Mapato na Matumizi ya Umma nambari 7 ya mwaka 2023 ya Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi alieleza imeleta mafanikio makubwa kwenye kujenga uwelewa kwa wananchi juu ya matumizi ya fedha za Umma.
Kuhusu mafanikio hayo Rais Dk. Mwinyi alieleza ni pamoja na kutumia mifumo, kuokoa fedha za Serikali kwa asilimia 86.3, kutekeleza miradi ya maendeleo kwa uwazi kwa asilimia 96, kuongezeka kwa uelewa wa usimamizi wa fedha za umma (mapato na matumizi) kwa asilimia 96, Matumizi ya mifumo kwenye shughuli za Serikali pia yameongezeka kutoka asilimia 48 na kufikia 92.4
Mafanikio mengine yaliyopatikana kutokana na kuimarika kwa utendaji huo Rais Dk. Mwinyi alieleza Serikali ya Zanzibar kupitia Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali kupewa kazi ya kusimamia na kufuatilia matumizi ya miradi ya maendeleo kupitia USAID na ADB ambapo awali kazi hio ilifanywa na taasisi binafsi.
Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi alisema, Zanzibar inajitahidi kutekeleza kwa ukamilifu makubaliano yaliyofikiwa baina ya nchi wanachama wa kamati za SADCOPAC.
“Siku siku zote tutajitahidi kuwa kinara katika utekelezaji ili malengo na mipango yetu iweze kufanikiwa kama sote tunavyotarajia” alibainisha Rais Dk. Mwinyi.Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi alizitaka kamati za Mabunge ya nchi wanachama wa SADC, kuendelea kudumisha ushirikiano na Tanzania hasa Zanzibar.
Mafunzo hayo yaliandaliwa na Wizara zinazosimamia sheria na utawala bora Tanzania, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Zanzibar pamoja na Uongozi na Sekretarieti ya SADCOPAC.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
18-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
18-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
18-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
18-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
18-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
18-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
18-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
18-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
18-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
18-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
18-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
18-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
18-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
18-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
18-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
18-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
18-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
18-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
18-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
18-11-2025