Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


ANAYESEMA SERIKALI YA CCM HAIJAFANYA KAZI HUWENDA MTU HUYO ANA TATIZO LA KISAIKOLOJIA - DKT. NCHIMBI

alternative

" Tunao watu katika jamii ambao hao wasiposingizia au kusema uongo wanakosa usingizi, lazima watu kama hao tuwashauri na kuna wakati inabidi watu kama hao kupewa ushauri wa daktari wa kisaikolojia...unakuta mtu anasema tuu CCM haijafanya kazi yoyote unagundua huyu ana tatizo la kisaikolojia "

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa CCM Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi wakati akizungumza kwenye Mkutano wa hadhara Wilayani Mpanda.

Pia, Balozi Dkt. Nchimbi amehimiza na kusisitza kujenga chama katika misingi ya haki na uswa.

" Hatupendi CCM kuwa kama vyama vya hao wengine ambao kazi yao ni kutukana watu tu, niwaombe wana CCM msiruhusu watu hao wakawachonganisha lazima muoneshe ukomavu kwa vitendo na mjibu kwa hoja wala msitukanane nao na hatuna sababu ya kuwa na vigugumizi ."

Aidha, Katibu Mkuu Dkt. Nchimbi amesistiza kuendelea kuunga mkono serikali ya CCM inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwakuwa inatanguliza maslahi ya Taifa kwa ujumla.

Sambamba na hilo,katika kuendelea kuweka misingi imara ya kulinda Taifa letu la Tanzania, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewataka Watanzania wote pasipo kujali itikadi ya vyama vyao, kabila wala dini.

"Amani na utulivu sio zawadi iliyoanguka bali ni jambo lililofanyiwa kazi kuanzia Hayati Baba wa Taifa Rais Mwl. Nyerere hadi leo hii kwa Rais Dkt. Samia alipofikia, Marais wote katika hili wametimiza kiapo chao."

"Niwahikishie kwa uongoz wa Rais Dkt. Samia nchi yetu itaendelea kuwa na amani na nawaomba tuunge mkono amani na utulivu huu kuepukana na kuwasapoti baadhi wanaotaka kuhatarisha amani hii, nyinyi baadhi mnaishi mipakani na mnajua nchi bila amani inavyokuwa"

Balozi Dkt. Emmanuel  Nchimbi
Katibu Mkuu wa CCM

🗓️ 13 Aprili, 2024
📍 Mpanda - Katavi

alternative alternative alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi