MITANO TENA NI KWA DK. SAMIA TU, WENGINE SUBIRINI KUCHUJWA - WASIRA
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, ‘Mitano Tena’ ni kwa mgombea urais, Dk. Samia Suluhu Hassan na Mgombea Mwenza wake, Dk. Emmanuel Nchimbi, lakini wabunge na madiwani wasubiri kuchujwa kupitia vikao vya Chama.
Ameeleza hayo leo Juni 11, 2025 alipokuwa akizungumza katika kikao cha ndani kilichohusisha viongozi wa CCM Wilaya ya Nyasa, katika mji wa Mbamba Bay mkoani Ruvuma ambako anaendelea na ziara ya kuimarisha Chama.
“Niwaambie wana CCM wenzangu tunaposema mitano tena ni kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa nafasi ya urais na mgombea mwenza wake Dk. Emmanuel Nchimbi lakini kwa wabunge na madiwani wasubiri mchujo ndani ya Chama na mwaka huu tumeongeza idadi ya wapiga kura. Kwa mfano hapa Nyasa walikuwa wapigakura za maoni 900 lakini sasa wako 1,3000.”
Wasira alisema kupata wagombea safi ndani ya Chama wa udiwani na ubunge ni vema wakachaguliwa kwa utaratibu wa haki huku akisisitiza ‘mitano tena’ sio kwa watu wote ”Sio kila mtu ni mitano tena bali mitano tena ni kwa Rais Samia, wengine tunachujana.”
Akifafanua zaidi, Wasira alisema mabalozi wa CCM wana kazi ya kuchagua wagombea safi kupitia kura za maoni ambao watauzika mbele ya wananchi na sio wagombea ambao wanatokana na kununua kura.
“Heshima ya wajumbe ni anayesikiliza watu walionyuma yake, ni kupiga kura kwa mtu ambaye wananchi wanamtaka na katika majina matatu ambayo yatapendekezwa kupitia kura za maoni atapatikana mmoja ambaye atakuwa diwani au mbunge kwa miaka mitano.
“Kuna diwani amesema hapa kuwa wamefanya kazi nzuri na wanaomba ruhusa waendelee. Hakuna mtu anakataa ruksa lakini ruhusa haitolewi na mimi bali inatolewa na wananchi waliokupigia kura. Mimi nikimaliza (ziara) naondoka lakini wapigakura wanabaki na ndio watasema diwani amefanya kazi nzuri tunataka arudi na wale wapigakura wa kata yako watasema hivyo ndivyo.”
Katika ziara hiyo Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Tanzania Bara Stephen Wasira amekagua maendeeo ya Ujenzi wa bandari ya Mbambabay iliyoko wilayani Nyasa mkoani Ruvuma ambayo Serikali imepeleka fedha ili kuiboresha.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025