JAJI WARIOBA: NAPONGEZA CCM KWA HATUA ZAKE DHIDI YA RUSHWA
Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba, amepongeza hatua zilizoanza kuchukuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mapambano dhidi ya rushwa kwenye uchaguzi.
Jaji Warioba ametoa pongezi hizo akirejea mabadiliko ya Katiba ya CCM yaliyofanywa na Mkutano Mkuu Maalum wa CCM, yakiwemo marekebisho ya namna ya kupata wagombea wa udiwani, uwakilishi na ubunge, kwa kuongeza idadi ya wapiga kura wa vikao vya kura za maoni.
Amesema kwa kuwa vita dhidi ya rushwa si ya siku moja, CCM haina budi kuhakikisha mapambano ya kumshinda adui huyo yanakuwa endelevu kwa kusimamia misingi ya kuanzishwa kwa chama hicho.
Mhe. Warioba, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Mstaafu, amesema hayo katika mazungumzo yake na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, leo Alhamisi, tarehe 20 Februari 2025, baada ya Balozi Nchimbi kumtembelea nyumbani kwake, jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kumjulia hali.
Aidha, Jaji Warioba, mbali na kukumbusha kuhusu misingi ya CCM, alisisitiza sifa na miiko ya uongozi ilivyoainishwa kwenye Katiba ya CCM, akisema chama kina wajibu wa kuendelea kuwapatia matumaini Watanzania kwa kutoa uongozi bora kwa mwelekeo sahihi wa nchi.
“Hivi mlivyoanza ni safi, in the long run (hatimaye huko mbele) tutakuwa na mwanga wa mapambano dhidi ya rushwa. Nilikuwa very interested (na hamu kubwa) kujua mabadiliko hayo kwenye Katiba ya Chama, nilivyoshindwa kuwepo kwenye Mkutano Mkuu Maalum. Ni muhimu sana CCM iendelee kusimamia misingi yake, ikiwemo ahadi za mwanachama.
“Vita hii si ya siku moja, ni muhimu muda wote chama kitafute njia za kuzuia rushwa kwa kusimamia misingi yake. Watu wazungumzie sifa na miiko ya uongozi. Wazungumzie sera, si hela. Kihistoria, CCM ni chama cha itikadi, sera na ilani. Kina wajibu wa kuonesha matumaini wapi tunawapeleka watu,” alisema Jaji Warioba na kuongeza:
“Hivi mlivyoanza kupambana na rushwa itasaidia… mmeanza… naomba tu msikate tamaa. Jingine muhimu ni hili suala la kutoa mafunzo, pia ni muhimu sana. Wanachama na viongozi ni muhimu wakijue chama vizuri, hadi huko chini kabisa kwa wananchi. CCM ni tofauti na vyama vingine. Tunao wajibu wa kufanya kwa watu.”
Aidha, alisema vyama vya siasa nchini vinapaswa kutofautiana kwa sera na dira ya namna ya kuwatumikia watu, badala ya kutumia muda mwingi kuzungumzia namna ya kupata madaraka.
Jaji Warioba alisisitiza pia umuhimu wa CCM kuendeleza na kuimarisha utamaduni wake wa kupokea mawazo mapya ili kujiimarisha zaidi katika maisha na hali ya watu, huku kikitumia utaratibu wake wa miaka mingi katika kuandaa viongozi bora kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania.
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
12-01-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
12-01-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
12-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
12-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
12-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
12-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
12-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
12-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
12-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
12-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
12-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
12-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
12-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
12-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
12-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
12-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
12-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
12-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
12-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
12-01-2026